< Salmos 111 >

1 Alabaré a Jehová con todo el corazón, en la compañía y congregación de los rectos.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 Grandes son las obras de Jehová: buscadas de todos los que las quieren.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 Honra y hermosura es su obra; y su justicia permanece para siempre.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 Hizo memorables sus maravillas: clemente y misericordioso es Jehová.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 Dio mantenimiento a los que le temen: para siempre se acordará de su concierto.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 La fortaleza de sus obras anunció a su pueblo: dándoles la heredad de los Gentiles.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 Las obras de sus manos son verdad y juicio: fieles son todos sus mandamientos;
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 Afirmados por siglo de siglo: hechos en verdad y en rectitud.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 Redención ha enviado a su pueblo; ordenó para siempre su concierto: santo y terrible es su nombre.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 El principio de la sabiduría es el temor de Jehová; entendimiento bueno es a todos los que guardan sus mandamientos: su loor permanece para siempre.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.

< Salmos 111 >