< Proverbios 14 >

1 La mujer sabia edifica su casa: mas la insensata con sus manos la derriba.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 El que camina en su rectitud, teme a Jehová: mas el pervertido en sus caminos, le menosprecia.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 En la boca del insensato está la vara de la soberbia: mas los labios de los sabios los guardarán.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Sin bueyes, el alfolí está limpio: mas por la fuerza del buey hay abundancia de panes.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 El testigo verdadero, no mentirá: mas el testigo falso hablará mentiras.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Buscó el burlador la sabiduría, y no la halló: mas la sabiduría al hombre entendido es fácil.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Vete de delante del hombre insensato: pues no le conociste labios de ciencia.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 La ciencia del cuerdo es entender su camino: mas la insensatez de los fatuos es engaño.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Los insensatos hablan pecado; mas entre los rectos hay amor.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 El corazón conoce la amargura de su alma; y extraño no se entremeterá en su alegría.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 La casa de los impíos será asolada: mas la tienda de los rectos florecerá.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 Hay camino que al hombre le parece derecho: mas su salida es caminos de muerte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Aun en la risa tendrá dolor el corazón; y la salida de la alegría es congoja.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 De sus caminos será harto el apartado de razón; y el hombre de bien se apartará de él.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 El simple cree a toda palabra: mas el entendido entiende sus pasos.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 El sabio teme, y apártase del mal: mas el insensato enójase, y confía.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 El que de presto se enoja, hará locura; y el hombre de malos pensamientos será aborrecido.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Los simples heredarán la insensatez: mas los cuerdos se coronarán de sabiduría.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 Los malos se inclinaron delante de los buenos; y los impíos, a las puertas del justo.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 El pobre es odioso aun a su amigo: mas los que aman al rico, son muchos.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 El pecador menosprecia a su prójimo: mas el que tiene misericordia de los pobres, es bienaventurado.
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 ¿No yerran, los que piensan mal? mas los que piensan bien tendrán misericordia, y verdad.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 En todo trabajo hay abundancia: mas la palabra de los labios solamente empobrece.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 La corona de los sabios es sus riquezas: mas la insensatez de los fatuos su fatuidad.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 El testigo verdadero libra las almas: mas el engañoso hablará mentiras.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 En el temor de Jehová está la fuerte confianza; y allí sus hijos tendrán esperanza.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 El temor de Jehová es manadero de vida, para ser apartado de los lazos de la muerte.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 En la multitud del pueblo está la gloria del rey; y en la falta del pueblo, la flaqueza del príncipe.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 El que tarde se aira, es grande de entendimiento: mas el corto de espíritu, engrandece la locura.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 El corazón blando es vida de las carnes: mas la envidia, pudrimiento de huesos.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 El que oprime al pobre, afrenta a su hacedor: mas el que tiene misericordia del pobre, le honra.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 Por su maldad será lanzado el impío: mas el justo, en su muerte tiene esperanza.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 En el corazón del cuerdo reposará la sabiduría; y en medio de los insensatos es conocida.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 La justicia engrandece la gente: mas el pecado es afrenta de las naciones.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 La benevolencia del rey es para con el siervo entendido: mas el que le avergüenza, es su enojo.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< Proverbios 14 >