< Job 41 >

1 ¿Sacarás tú al Leviatán con el anzuelo; y con la cuerda que le echares en su lengua?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 ¿Pondrás tú garfio en sus narices; y horadarás tú con espina su quijada?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 ¿Multiplicará él ruegos para contigo? ¿hablarte ha él a ti lisonjas?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 ¿Hará concierto contigo para que le tomes por siervo perpetuo?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 ¿Jugarás tú con él, como con pájaro? ¿y atarle has para tus niñas?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 ¿Harán banquete por causa de él los compañeros? ¿partirle han entre los mercaderes?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 ¿Cortarás tú con cuchillo su cuero, y con francado de pescadores su cabeza?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Pon tu mano sobre él: acordarte has de la batalla, y nunca más tornarás.
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 He aquí que tu esperanza será burlada; por que aun a su sola vista se desmayarán.
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Nadie hay tan osado que le despierte: ¿quién pues podrá estar delante de mí?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 ¿Quién me previno para que yo se lo agradezca? todo lo que está debajo del cielo es mío.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 Y no callaré sus miembros, y la cosa de sus fuerzas, y la gracia de su disposición.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 ¿Quién descubrirá la delantera de su vestidura? ¿quién se llegará a él con freno doble?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 ¿Quién abrirá las puertas de su rostro? Los ordenes de sus dientes espantan.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 La gloria de su vestido es escudos fuertes, cerrados entre sí estrechamente.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 El uno se junta con el otro, que viento no entra entre ellos.
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 El uno está pegado con el otro, están trabados entre sí, que no se pueden apartar.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Con sus estornudos enciende lumbre; y sus ojos son como los párpados del alba.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 De su boca salen hachas de fuego, y proceden centellas de fuego.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 De sus narices sale humo, como de una olla, o caldero que hierve.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Su aliento enciende los carbones, y de su boca sale llama.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 En su cerviz mora la fortaleza, y delante de él es deshecho el trabajo.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Las partes de su carne están pegadas entre sí: está firme su carne en él, y no se mueve.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Su corazón es firme como una piedra, y fuerte como la muela de debajo.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 De su grandeza tienen temor los fuertes, y de sus desmayos se purgan.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Cuando alguno le alcanzare, ni espada, ni lanza, ni dardo, ni coselete, durará contra él.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 El hierro estima por pajas, y el acero por leño podrido.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Saeta no le hace huir: las piedras de honda se le tornan armas.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Toda arma tiene por hojarascas, y del blandeamiento de la pica se burla,
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Por debajo tiene agudas conchas: imprime su agudez en el suelo.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Hace hervir como una olla la profunda mar; y tórnala como una olla de ungüento.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 En pos de sí hace resplandecer la senda, que parece que la mar es cana.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 No hay sobre la tierra su semejante, hecho para nada temer.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Menosprecia toda cosa alta, es rey sobre todos los soberbios.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Job 41 >