< Job 26 >

1 Y respondió Job, y dijo:
Kisha Ayubu akajibu:
2 ¿En qué ayudaste al que no tiene fuerza? ¿salvaste con brazo al que no tiene fortaleza?
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 ¿En qué aconsejaste al que no tiene ciencia? ¿y mostraste asaz [tu] sabiduría?
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 ¿A quién has anunciado palabras? ¿y cúyo es el espíritu que sale de ti?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 Cosas inanimadas son formadas debajo de las aguas, y de sus moradas.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 El sepulcro es descubierto delante de él, y el infierno no tiene cobertura. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 Extiende al aquilón sobre vacío: cuelga la tierra sobre nada.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Las aguas ata en sus nubes, y las nubes no se rompen debajo de ellas.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 El aprieta la faz de su trono, y extiende sobre él su nube.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 El cercó con término la superficie de las aguas hasta que se acabe la luz y las tinieblas.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Las columnas del cielo tiemblan, y se espantan de su reprensión.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 El rompe la mar con su potencia, y con su entendimiento hiere [su] hinchazón.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 Su Espíritu adornó los cielos: su mano crió la serpiente rolliza.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 He aquí, estas son partes de sus caminos: ¿y cuán poco es lo que habemos oído de él? porque el estruendo de sus fortalezas ¿quién lo entenderá?
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >