< 1 Crónicas 24 >

1 También los hijos de Aarón tuvieron sus repartimientos. Los hijos de Aarón fueron; Nadab, Abiú, Eleazar, Itamar,
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Mas Nadab y Abiú murieron antes de su padre, y no tuvieron hijos: Eleazar e Itamar tuvieron el sacerdocio.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 Y David los repartió: Sadoc era de los hijos de Eleazar, y Aquimelec de los hijos de Itamar, en su cuenta, en su ministerio.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Y los hijos de Eleazar fueron hallados muchos más, en cuanto a sus principales varones, que los hijos de Itamar; y repartiéronlos así: De los hijos de Eleazar diez y seis cabezas por las familias de sus padres: y de los hijos de Itamar por las familias de sus padres, ocho.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 Y repartiéronlos por suerte los unos con los otros: porque de los hijos de Eleazar, y de los hijos de Itamar, hubo príncipes del santuario, y príncipes de Dios.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 Y Semeías, hijo de Natanael, escriba de los Levitas, los escribió delante del rey, y de los príncipes, y delante de Sadoc el sacerdote, y de Aquimelec, hijo de Abiatar, y de los príncipes de las familias de los sacerdotes y Levitas: y a Eleazar atribuyeron una familia, y a Itamar fue atribuida otra.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 Y la primera suerte salió por Joiarib, la segunda por Jedei,
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 La tercera por Harim, la cuarta por Seorim,
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 La quinta por Melquías, la sexta por Maimán,
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 La séptima por Accos, la octava por Abías,
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 La nona por Jesúa, la décima por Sequemias,
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 La undécima por Eliasib, la duodécima por Jacim,
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 La trecena por Hopfa, la catorcena por Isbaab,
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 La quincena por Belga, la dieziseisena por Emmer,
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 La decimaséptima por Hezir, la décimaoctava por Afses,
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 La décimanona por Feceia, la vigésima por Hezeciel,
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 La veinte y una por Joaquim, la veinte y dos por Gamul,
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 La veinte y tres por Dalaiau, la veinte y cuatro por Maaziau.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Estos fueron contados en su ministerio, para que entrasen en la casa de Jehová conforme a su costumbre, debajo de la mano de Aarón su padre, de la manera que le había mandado Jehová el Dios de Israel.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 Y de los hijos de Leví que quedaron: De los hijos de Amram era Subael: y de los hijos de Subael, Jehedeias.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 Y de los hijos de Rohobias, Jesías el principal.
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 De Isaari, Salemot: e hijo de Salemot fue Jahat.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 Y su primer hijo fue Jeriau, el segundo Amarías, el tercero Jahaziel, el cuatro Jecmaam.
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 Hijo de Oziel fue Mica, e hijo de Mica fue Samir.
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 Hermano de Mica fue Jesía, e hijo de Jesía fue Zacarías.
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 Los hijos de Merari fueron Moholi, y Musi: hijo de Oziau fue Benno.
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 Los hijos de Merari de Oziau fueron Benno y Soam, Zacur y Hebri,
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 Y Eleazar de Moholi, el cual no tuvo hijos.
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 Hijo de Cis fue Jerameel.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 Los hijos de Musi fueron Moholi, Eder, y Jerimot. Estos fueron los hijos de los Levitas conforme a las casas de sus familias.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 Estos también echaron suertes contra sus hermanos los hijos de Aarón delante del rey David, y de Sadoc, y de Aquimelec, y de los príncipes de las familias de los sacerdotes, y de los Levitas, el principal de los padres contra su hermano menor.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.

< 1 Crónicas 24 >