< Luka 22 >

1 Bližal se je pa praznik presnih kruhov, kteri se imenuje Velika noč.
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 In gledali so véliki duhovni in pismarji, kako bi ga umorili; kajti bali so se ljudstva.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 Pa vnide satan v Juda s priimkom Iškarijana, kteri je bil iz števila dvanajsterih;
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 Ter odide, in dogovorí se z vélikimi duhovni in starešinami tempeljna, kako jim ga bo izdal.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 In razveselé se, in obrekó mu dati denarja.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 In obrekel se je, in iskal je pripravnega časa, da jim ga izdá brez ljudstva.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 Pride pa dan presnih kruhov, ko je bilo treba velikonočno jagnje klati.
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 Ter pošlje Petra in Janeza, govoreč: Pojdita, pripravita nam velikonočno jagnje, da jemo.
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 Ona mu pa rečeta: Kje hočeš, da pripraviva?
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 A on jima reče: Glej, ko vnideta v mesto, srečal vaju bo človek, kteri ponese vrč vode; pojdita za njim v hišo, v ktero vnide,
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 In recita hišnemu gospodarju: Učenik ti pravi: Kje je gostilnica, kjer bom jedel velikonočno jagnje z učenci svojimi?
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 In on vama bo pokazal veliko izbo pogrnjeno; tam pripravita.
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 Ter odideta in najdeta, kakor jima je bil rekel; in pripravita velikonočno jagnje.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 In ko pride čas, sede za mizo, in dvanajsteri aposteljni ž njim.
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 In reče jim: Željno sem hrepenel jesti to velikonočno jagnje z vami, predno bom trpel;
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 Kajti pravim vam, da ga ne bom več jedel, dokler se v kraljestvu Božjem ne dopolni.
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 In vzemši kelih, zahvali, in reče: Vzemite ga, in razdelite med seboj.
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 Kajti pravim vam, da ne bom pil od trtnega rodú, dokler ne pride kraljestvo Božje.
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 In vzemši kruh, zahvali, in prelomivši, dá jim govoreč: To je telo moje, ktero se za vas daje; to delajte za moj spomin.
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 Ravno tako tudi kelih po večerji, govoreč: Ta kelih je nova zaveza po krvi mojej, ktera se za vas prelija.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 In glej, roka izdajalca mojega je z menoj na mizi.
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 In sin človečji gre, kakor je odločeno; ali gorjé človeku, kteri ga izdaja.
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 In oni začnó iskati med seboj, kdo od njih bi bil, kteri bo to storil.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 Vname se pa tudi prepir med njimi, kdo od njih da meni, da je veči.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 On jim pa reče: Kralji narodov tem gospodujejo, a kteri imajo oblast, imenujejo se dobrotniki.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 Vi pa ne tako: nego kdor je največi med vami, bodi kakor najmanji; in kdor je vodnik, bodi kakor služabnik.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 Kajti kdo je veči: kdor sedí za mizo, ali kdor streže? Ali ne ta, kdor sedí za mizo? In jaz sem med vami, kakor kdor streže.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 A vi ste, kteri ste prebili z menoj v izkušnjavah mojih.
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 In jaz vam bom zapustil kraljestvo, kakor ga je meni oče moj zapustil,
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 Da boste jedli in pili za mizo mojo v kraljestvu mojem, in boste sedeli na prestolih in sodili dvanajstere rodove Izraelove.
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 Reče pa Gospod: Simon! Simon! glej, satan vas je poželel, da bi vas presejal, kakor pšenico;
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 Ali jaz sem za te molil, naj ne izgine vera tvoja: in ti, kedar se spreobrneš, utrdi brate svoje.
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 On mu pa reče: Gospod, pripravljen sem s teboj iti v ječo in na smrt.
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 A on mu reče: Pravim ti, Peter! nocoj ne bo zapel petelin, dokler trikrat ne utajiš, da me poznaš.
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 In reče jim: Ko sem vas poslal brez mošnje in torbe in obutala, ali vam je česa zmanjkalo? Oni pa rekó: Ničesar.
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 Reče jim torej: Ali sedaj, kdor ima mošnjo, vzeme naj jo, ravno tako tudi torbo; a kdor nima, prodá naj suknjo svojo, in kupi meč.
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 Kajti pravim vam, da se mora še to pismo izpolniti na meni: "In hudodelnikom je bil prištet." Kajti to, kar je pisano za me, dopolnjuje se.
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 Oni pa rekó: Gospod, glej tu dva meča! A on jim reče: Dosti je!
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 Ter izide in odide po navadi na Oljsko goro; šli so pa za njim tudi učenci njegovi.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 A ko pride na mesto, reče jim: Molite, da ne zajdete v izkušnjavo.
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 In on odstopi od njih za lučaj kamena, in pokleknivši na kolena, molil je,
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 Govoreč: Oče, ko bi hotel prenesti ta kelih mimo mene! ali ne moja volja, nego tvoja bodi.
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 Prikaže pa mu se angelj z neba, ter ga je krepčal.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 In ko je bil v boji, molil jo gorečneje. In bil je pót njegov kakor kaplje krví, ktere so padale na zemljo.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 In vstavši od molitve, pride k učencem svojim, in najde jih, da spé od žalosti,
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 In reče jim: Kaj spite? Vstanite! molite, da ne zajdete v izkušnjavo.
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 A ko je še govoril, glej, ljudstvo; in eden dvanajsterih, kteri se je imenoval Juda, šel je pred njim, in približa se Jezusu, da ga poljubi,
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 Jezus mu pa reče: Juda! s poljubom izdajaš sina človečjega?
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 Videč pa tí, kteri so bili okoli njega, kaj da bo, rekó mu: Gospod, ali naj udarimo z mečem?
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 In eden od njih udari hlapca vélikega duhovna, in odseka mu desno uho.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 Odgovarjajoč pa Jezus, reče: Nehajte, dotlej! In dotaknivši se ušesa njegovega, uzdravi ga.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 A vélikim duhovnom in poglavarjem tempeljna in starešinam, kteri so bili prišli nad-nj, reče Jezus: Kakor na razbojnika ste izšli nad me z meči in koli?
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 Vsak dan sem bil z vami v tempeljnu, in niste iztegnili rok na me. Ali ta je vaša ura, in oblast teme.
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 In zgrabivši ga, odženó in peljejo ga v hišo vélikega duhovna; a Peter je od daleč šel za njim.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 In ko so bili zanetili ogenj sredi dvorišča, in so vkupej sedli, sede Peter med-nje.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 Ugledavši ga pa ena dekla, da sedí pri ognji, ozrê se na-nj, in reče: Tudi ta je bil ž njim.
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 A on ga zatají, govoreč: Žena! nisem ga videl.
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 In malo po tem ga ugleda drugi, in reče: Tudi ti si izmed njih. A Peter reče: Človek! nisem.
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 In eno ura ali kaj po tem trdil je nekdo drugi, govoreč: Zares, tudi ta je bil ž njm; saj je tudi Galilejec.
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 Ali Peter reče: Človek! ne vém, kaj praviš. In precej, ko je še govoril, zapoje petelin.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 In obrnivši se Gospod, pogleda na Petra; in spomene se Peter besede Gospodove, kakor mu je bil rekel: Predno bo petelin zapel, zatajil me boš trikrat.
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 In Peter izide ven, in razjoka se britko.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 In možjé, kteri so držali Jezusa, zasmehovali so ga in bíli.
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 In zakrivši ga, bíli so ga po obrazu, in vpraševali so ga, govoreč: Prerokuj, kdo te je udaril?
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 In drugega veliko so preklinjajoč govorili zoper njega.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 In ko napoči jutro, zberó se starešine ljudstva, in véliki duhovni in pismarji, in odpeljejo ga v sodišče svoje, govoreč: Če si ti Kristus? povéj nam.
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 Pa jim rečé; Če vam povem, nikakor ne boste verovali;
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 A če tudi vprašam, ne boste mi odgovorili, in tudi izpustili me ne boste.
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 Odslej bo sin človečji sedel na desnici moči Božje.
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 Pa rekó vsi: Ti si torej sin Božji? On jim pa reče: Vi pravite, da jaz sem.
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 A oni rekó: Kaj nam je še treba prič? saj smo sami slišali iz ust njegovih.
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”

< Luka 22 >