< Luka 19 >

1 In vnide, in šel je skozi Jeriho.
Yesu akaingia Yeriko, naye alikuwa anapita katikati ya huo mji.
2 In glej, mož po imenu Zahej, in ta je bil starešina mitarjem, in bil je bogat,
Tazama, palikuwa na mtu mmoja mkuu wa watoza ushuru naye alikuwa tajiri, jina lake Zakayo.
3 In rad bi bil videl Jezusa, kdo da je; pa ni mogel za voljo ljudstva, ker je bil majhne postave.
Yeye alikuwa akijitahidi kumwona Yesu ni mtu wa namna gani. Lakini kutokana na umati mkubwa wa watu hakuweza kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo.
4 In poletel je naprej, in zlezel je na murvo, da bi ga videl: ker je imel todi mimo iti.
Kwa hiyo akatangulia mbio mbele ya umati wa watu akapanda juu ya mkuyu ili amwone Yesu, kwa sababu angeipitia njia ile.
5 In Jezus, ko pride na to mesto, ozrè se gor, in ugleda ga, in reče mu: Zahej, snidi hitro! kajti danes moram v tvojej hiši ostati.
Yesu alipofika pale chini ya huo mkuyu, akatazama juu, akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, kwa maana leo nitakuwa mgeni nyumbani kwako!”
6 Pa snide hitro in ga radosten sprejme.
Hivyo Zakayo akashuka upesi, akamkaribisha Yesu nyumbani kwake kwa furaha kubwa.
7 In vsi so, ko so to videli, godrnjali, govoreč: Pri grešnem človeku se je navrnil!
Watu wote walipoona hivyo, wakaanza kunungʼunika wakisema, “Amekwenda kuwa mgeni wa ‘mtu mwenye dhambi.’”
8 Pristopivši pa Zahej, reče Gospodu: Glej, polovico premoženja svojega, Gospod, dajem ubogim; in če sem koga ogoljufal, povrnil mu bom čvetero.
Lakini Zakayo akasimama na kumwambia Bwana, “Tazama, Bwana! Sasa hivi nusu ya mali yangu ninawapa maskini, nami kama nimemdhulumu mtu yeyote kitu chochote, nitamrudishia mara nne ya hicho kiwango.”
9 Jezus mu pa reče: Danes je prišlo zveličanje tej hiši, ker je tudi ta sin Abrahamov.
Ndipo Yesu akamwambia, “Leo, wokovu umeingia nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Abrahamu.
10 Kajti prišel je sin človečji iskat in zveličat, kar se je izgubilo.
Kwa maana Mwana wa Adamu amekuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
11 Ko so pa to poslušali, pristavi in pové priliko, zato, ker je bil blizu Jeruzalema, in so mislili, da se bo kraljestvo Božje precej razodelo.
Walipokuwa wanasikiliza haya, Yesu akaendelea kuwaambia mfano, kwa sababu alikuwa anakaribia Yerusalemu na watu walikuwa wakidhani ya kuwa Ufalme wa Mungu ulikuwa unakuja saa iyo hiyo.
12 In reče: Neki človek imenitnega rodú je šel v daljno deželo, da si vzeme kraljestvo, in da se vrne.
Hivyo akawaambia: “Mtu mmoja mwenye cheo kikubwa alisafiri kwenda nchi ya mbali ili akapokee madaraka ya kuwa mfalme, kisha arudi.
13 In poklicavši deset hlapcev, dá jim deset mošenj, in reče jim: Kupčujte, dokler se ne vrnem.
Hivyo akawaita kumi miongoni mwa watumishi wake, na akawapa kila mmoja fungu la fedha. Akawaambia, ‘Fanyeni biashara na fedha hizi mpaka nitakaporudi.’
14 Meščani njegovi so ga pa sovražili, ter pošljejo poslance za njim, govoreč: Nečemo, da bi nam ta kraljeval.
“Lakini raiya wa nchi yake walimchukia wakapeleka ujumbe na kusema, ‘Hatutaki huyu mtu awe mfalme wetu.’
15 In zgodí se, ko je bil kraljestvo prejel in se je vrnil, pa reče, naj mu pokličejo te hlapce, kterim je bil dal srebro, da bi zvedel, kaj je kdo prikupčeval.
“Hata hivyo alirudi akiwa amekwisha kupokea mamlaka ya ufalme, akawaita wale watumishi wake aliokuwa amewaachia fedha, ili afahamu ni faida kiasi gani kila mmoja wao aliyopata kwa kufanya biashara.
16 Pa pride prvi, govoreč: Gospod, mošnja tvoja je pridobila deset mošenj.
“Wa kwanza akaja na kusema, ‘Bwana, kutokana na fedha uliyoniachia, nimepata faida mara kumi zaidi.’
17 In reče mu: Dobro, vrli hlapec! ker si bil v najmanjem zvest, iméj oblast nad desetémi mesti.
“Yule bwana akamjibu, ‘Umefanya vizuri mtumishi mwema! Kwa sababu umekuwa mwaminifu katika wajibu mdogo sana, nakupa mamlaka juu ya miji kumi.’
18 In pride drugi, govoreč: Gospod, mošnja tvoja je napravila pet mošenj.
“Wa pili naye akaja. Akasema, ‘Bwana, fedha yako imeleta faida mara tano zaidi.’
19 In tudi temu reče: Tudi ti bodi nad petémi mesti.
“Bwana wake akajibu, ‘Nakupa mamlaka juu ya miji mitano.’
20 In drugi pride, govoreč: Gospod, glej, tu je mošnja tvoja, ktero sem imel v prtu spravljeno.
“Kisha akaja yule mtumishi mwingine, akasema, ‘Bwana, hii hapa fedha yako. Niliitunza vizuri kwenye kitambaa.
21 Kajti bal sem se te, ker si trd človek: jemlješ, česar nisi položil; žanješ, česar nisi posejal.
Nilikuogopa, kwa sababu wewe ni mtu mgumu. Unachukua ambapo hukuweka kitu, na unavuna mahali ambapo hukupanda kitu.’
22 Pa mu reče: Sodil te bom po tvojih besedah, hudobni hlapec! Vedel si, da sem trd človek, in jemljem, česar nisem položil, in žanjem, česar nisem posejal;
“Bwana wake akamjibu, ‘Nitakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, wewe mtumishi mwovu! Kama ulifahamu kwamba mimi ni mtu mgumu, nichukuaye mahali ambapo sikuweka kitu na kuvuna mahali ambapo sikupanda,
23 In za kaj nisi dal srebra mojega kupcu, da bi ga bil, kedar bi se bil vrnil, prejel z dobičkom?
kwa nini basi hukuweka fedha zangu kwa watoa riba, ili nitakaporudi nichukue iliyo yangu na riba yake?’
24 Ter reče tém, kteri so stali pred njim: Vzemite mu mošnjo, in dajte tistemu, kteri jih ima deset.
“Ndipo akawaambia wale waliokuwa wamesimama karibu, ‘Mnyangʼanyeni fungu lake la fedha, mkampe yule mwenye kumi.’
25 (Pa mu rekó: Gospod, deset mošenj ima!)
“Wakamwambia, ‘Bwana, mbona; tayari anayo mafungu kumi!’
26 Pravim vam namreč, da vsakemu, kdor ima, dalo se bo; a kdor nima, odvzelo mu se bo tudi to, kar ima.
“Akawajibu, ‘Nawaambia kwamba kila aliye na kitu, ataongezewa. Lakini yule asiye na kitu, hata alicho nacho atanyangʼanywa.
27 A tiste sovražnike moje, kteri niso hoteli, da bi jim kraljeval, pripeljite sêm, in posekajte jih pred menoj.
Lakini wale adui zangu ambao hawakutaka mimi niwe mfalme juu yao. Waleteni hapa mkawaue mbele yangu.’”
28 In ko je bil to povedal, šel je dalje, gredoč gor v Jeruzalem.
Baada ya Yesu kusema haya, alitangulia kupanda kwenda Yerusalemu.
29 In zgodí se, ko se približa Betfagi in Betaniji, pri gori, ktera se imenuje Oljska, pošlje dva izmed učencev svojih,
Naye alipokaribia Bethfage na Bethania kwenye mlima uitwao Mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili, akawaambia,
30 Govoreč: Pojdita v vas, ki je nasproti, v kterej bosta našla, kedar vnideta, žrebe privezano, na ktero se ni nikoli noben človek usedel: odvežita ga, in pripeljita sèm.
“Nendeni katika kijiji kilichoko mbele yenu. Na mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana-punda amefungwa hapo, ambaye hajapandwa na mtu bado. Mfungueni, mkamlete hapa.
31 In če vaju kdo vpraša: Po kaj odvezujeta? povejta mu tako: Gospod ga potrebuje.
Kama mtu akiwauliza, ‘Mbona mnamfungua?’ Mwambieni, ‘Bwana anamhitaji.’”
32 In poslanca odideta in najdeta, kakor jima je bil rekel.
Wale waliotumwa wakaenda, wakakuta kila kitu kama vile Yesu alivyokuwa amewaambia.
33 Ko sta pa žrebe odvezovala, rekó jima gospodarji njegovi: Kaj odvezujeta žrebe?
Walipokuwa wanamfungua yule mwana-punda, wenyewe wakawauliza, “Mbona mnamfungua huyo mwana-punda?”
34 Ona pa rečeta: Gospod ga potrebuje.
Wale wanafunzi wakajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 In pripeljeta k Jezusu; in položivši svoja oblačila na žrebe, posadé Jezusa.
Wakamleta kwa Yesu, nao baada ya kutandika mavazi yao juu ya huyo mwana-punda, wakampandisha Yesu juu yake.
36 Ko je pa šel, pogrinjali so oblačila svoja na pot.
Alipokuwa akienda akiwa amempanda, watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 In ko se je uže bližal strmcu Oljske gore, začne vsa množica učencev radostna Boga hvaliti z močnim glasom za vse čudeže, ktere so videli,
Alipokaribia mahali yanapoanzia materemko ya Mlima wa Mizeituni, umati wote wa wafuasi wake wakaanza kumsifu Mungu kwa furaha kwa sauti kuu kwa ajili ya matendo yote ya miujiza waliyoyaona. Wakasema:
38 Govoreč: Blagoslovljen kralj, kteri gre v imenu Gospodovem! Mir na nebu, in slava na višavah!
“Amebarikiwa Mfalme ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amani mbinguni na utukufu huko juu sana.”
39 In nekteri Farizeji izmed ljudstva mu rekó: Učenik, popréti učencem svojim!
Baadhi ya Mafarisayo waliokuwamo miongoni mwa ule umati wa watu wakamwambia, “Mwalimu, waamuru wanafunzi wako wanyamaze.”
40 In odgovarjajoč, reče jim: Pravim vam, da če ti umolkneje, vpilo bo kamenje.
Yesu akawajibu, “Nawaambia ninyi, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapiga kelele.”
41 In ko se približa in ugleda mesto, razjoka se nad njim,
Alipokaribia Yerusalemu na kuuona mji, aliulilia,
42 Govoreč: Ko bi pač tudi ti vedelo, vsaj ta dan tvoj, kaj je za mir tvoj: ali sedaj je skrito pred očmí tvojimi.
akisema, “Laiti ungalijua hata wewe leo yale ambayo yangeleta amani, lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Prišli bodo namreč nate dnevi, ko te bodo obdali sovražniki tvoji z nasipi, in te bodo oblegali, in stiskali te od vseh stranî;
Hakika siku zinakujia, ambazo adui zako watakuzingira, nao watakuzunguka pande zote na kukuzuilia ndani.
44 In razbili bodo tebe in otroke tvoje v tebi, in ne kamena na kamenu ne bodo pustili v tebi: za to, ker nisi poznalo časa, v kterim si bilo obiskano.
Watakuponda chini, wewe na watoto walioko ndani ya kuta zako. Nao hawataacha hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu hukutambua wakati wa kujiliwa kwako.”
45 In ko vnide v tempelj, začne izganjati tiste, kteri so prodajali v njem in kupovali,
Ndipo akaingia eneo la Hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza vitu humo.
46 Govoreč jim: Pisano je: "Dom moj je dom molitve;" a vi ste naredili iz njega "jamo razbojniško".
Naye akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa ‘pango la wanyangʼanyi.’”
47 In učil je vsak dan v tempeljnu; a véliki duhovni in pismarji in prvaki ljudski so iskali, da bi ga pogubili;
Kila siku alikuwa akifundisha Hekaluni. Lakini viongozi wa makuhani, walimu wa sheria na viongozi wa watu walikuwa wakitafuta njia ili kumuua.
48 In niso nahajali, kaj bi mu storili: kajti ljustvo se ga je držalo vse, poslušajoč ga.
Lakini hawakupata nafasi kwa sababu watu wote walimfuata wakiyasikiliza maneno yake kwa usikivu mwingi.

< Luka 19 >