< Galačanom 3 >

1 O nespametni Galačani, kdo vas je uročil, da ne bi ubogali resnice, pred čigar očmi je bil očitno postavljen Jezus Kristus, križan med vami?
Wagalatia wajinga, ni jicho gani ovu lililowaharibu? Je Yesu Kristo hakuoneshwa kama msulubiwa mbele ya macho yenu?
2 Samo to hočem izvedeti od vas: »Ali ste prejeli Duha z deli postave ali s poslušnostjo veri?«
Mimi nataka tu kufahamu hili kutoka kwenu. Je mlimpokea Roho kwa matendo ya sheria au kwa kuamini kile mlichosikia?
3 Ali ste tako nespametni? Ali ste, začenši z Duhom, sedaj popolni v mesu?
Je, ninyi ni wajinga kiasi hiki? Je mlianza katika Roho ili mmalize katika mwili?
4 Ali ste toliko stvari pretrpeli zaman? Če bi bile vendarle zaman.
Je mliteseka kwa mambo mengi bure, kama kweli yalikuwa ya bure?
5 On torej, ki vam daje Duha in med vami dela čudeže, ali jih dela po delih postave ali po poslušnosti veri?
Je yeye atoaye Roho kwenu na kutenda matendo ya nguvu kati yenu hufanya kwa matendo ya sheria au kwa kusikia pamoja na imani?
6 Celó kakor je Abraham veroval Bogu in mu je bilo to šteto za pravičnost.
Abraham “Alimwamini Mungu akahesabiwa kuwa mwenye haki”.
7 Spoznajte torej, da so Abrahamovi otroci tisti, ki so iz vere.
Kwa namna ile ile eleweni kwamba, wale ambao wanaamini ni watoto wa Abrahamu.
8 In ker je pismo slutilo, da bo Bog pogane opravičil po veri, je poprej oznanjalo evangelij Abrahamu, rekoč: ›V tebi bodo blagoslovljeni vsi narodi.‹
Andiko lilitabiri kwamba Mungu angewahesabia haki watu wa mataifa kwa njia ya imani. Injili ilihubiriwa kwanza kwa Abrahamu: “katika wewe mataifa yote yatabarikiwa”.
9 Tako so torej tisti, ki so iz vere, blagoslovljeni z zvestim Abrahamom.
Ili baadaye wale ambao wana imani wabarikiwe pamoja na Abrahamu, ambaye alikuwa na imani.
10 Kajti kolikor jih je iz del postave, so pod prekletstvom, kajti pisano je: ›Preklet je vsak, kdor ne vztraja v vseh stvareh, ki so pisane v knjigi postave, da jih izvrši.‹
Wale ambao wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu ambaye hashikamani na mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria, kuyatenda yote.”
11 Toda očitno je to, da v Božjih očeh noben človek ni opravičen s postavo, kajti: ›Pravični bo živel iz vere.‹
Sasa ni wazi kwamba Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria, kwa kuwa “Mwenye haki ataishi kwa imani”.
12 Postava pa ni iz vere, temveč: ›Človek, ki jih izvršuje, bo živel po njih.‹
Sheria haitokani na imani, lakini badala yake “Ambaye hufanya mambo haya katika sheria, ataishi kwa sheria.”
13 Kristus nas je odkupil od prekletstva postave, ko je za nas postal prekletstvo, kajti pisano je: ›Preklet je vsak, kdor visi na drevesu.‹
Kristo alitukomboa sisi kutoka katika laana ya sheria wakati alipofanyika laana kwa ajili yetu. Kwa kuwa imeandikwa, “Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti.”
14 Da bi Abrahamov blagoslov lahko po Jezusu Kristusu prešel na pogane, da bi mi po veri lahko prejeli obljubo Duha.
Lengo lilikuwa kwamba, baraka ambazo zilikuwa kwa Ibrahimu zingekuja kwa watu wa mataifa katika Kristo Yesu, ili kwamba tuweze kupokea ahadi ya Roho kupitia imani.
15 Bratje, govorim po človeških običajih: »Čeprav je to samo človeška zaveza, vendar če je potrjena, je noben človek ne razveljavlja ali dodaja k njej.«
Ndugu, ninazungumza kwa namna ya kibinadamu. Hata wakati ambapo agano la kibinadamu limekwisha kuwekwa imara, hakuna awezaye kupuuza au kuongezea.
16 Torej obljube so bile izrečene Abrahamu in njegovemu semenu. Ni rekel: ›In semenom, ‹ kakor mnogim; temveč kakor enemu: ›In tvojemu semenu, ‹ ki je Kristus.
Sasa ahadi zilisemwa kwa Ibrahim na kwa kizazi chake. Haisemi, “kwa vizazi,” kumaanisha wengi, bali badala yake kwa mmoja pekee, “kwa kizazi chako,” ambaye ni Kristo.
17 In pravim to, da zaveze, ki je bila prej potrjena od Boga v Kristusu, postava, ki je bila štiristo trideset let kasneje, ne more razveljaviti, da bi obljubo storila brez učinka.
Sasa nasema hivi, sheria ambayo ilikuja miaka 430 baadaye, haiondoi agano la nyuma lililowekwa na Mungu.
18 Kajti če je dediščina po postavi, le-ta ni več po obljubi; toda Bog jo je Abrahamu dal po obljubi.
Kwa kuwa kama urithi ungelikuja kwa njia ya sheria, usingekuwa tena umekuja kwa njia ya ahadi. Lakini Mungu aliutoa bure kwa Ibrahimu kwa njia ya ahadi.
19 Čemu potem služi postava? Dodana je bila zaradi prestopkov, dokler ne bi prišel potomec, ki mu je bila dana obljuba; in ta je bila odrejena po angelih v roko posrednika.
Kwa nini sasa sheria ilitolewa? Iliongezwa kwa sababu ya makosa, mpaka mzao wa Ibrahimu aje kwa wale ambao kwao alikuwa ameahidiwa. Sheria iliwekwa katika shinikizo kupitia malaika kwa mkono wa mpatanishi.
20 Torej posrednik ni posrednik enega, toda Bog je eden.
Sasa mpatanishi humaanisha zaidi ya mtu mmoja, bali Mungu ni mmoja peke yake.
21 Ali je potem postava zoper Božje obljube? Bog ne daj, kajti če bi bila dana postava, ki bi lahko dala življenje, bi bila pravičnost resnično po postavi.
Kwa hiyo je sheria iko kinyume na ahadi za Mungu? La hasha! Kwa kuwa kama sheria iliyokuwa imetolewa ilikuwa na uwezo wa kuleta uzima, haki ingepatikana kwa sheria.
22 Toda pismo je vse zaprlo pod greh, da bi bila lahko tem, ki verujejo, dana obljuba po veri Jezusa Kristusa.
Lakini badala yake, andiko limefunga mambo yote chini ya dhambi. Mungu alifanya hivi ili kwamba ahadi yake ya kutuokoa sisi kwa imani katika Yesu Kristo iweze kupatikana kwa wale wanao amini.
23 Toda preden je prišla vera, smo bili držani pod postavo, zaprti veri, ki naj bi se razodela kasneje.
Lakini kabla ya imani katika Kristo haijaja, tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria hadi uje ufunuo wa imani.
24 Zatorej je bila postava naša vzgojiteljica, da nas privede h Kristusu, da bi bili mi lahko opravičeni iz vere.
Kwa hiyo sheria ilifanyika kiongozi wetu hadi Kristo alipokuja, ili kwamba tuhesabiwe haki kwa imani.
25 Toda potem, ko je prišla vera, nismo več pod vzgojiteljico.
Sasa kwa kuwa imani imekuja, hatuko tena chini ya mwangalizi.
26 Kajti vi vsi ste Božji otroci po veri v Kristusa Jezusa.
Kwa kuwa ninyi nyote ni watoto wa Mungu kupitia imani katika Kristo Yesu.
27 Kajti tako veliko, kot vas je bilo krščenih v Kristusa, ste oblekli Kristusa.
Wote ambao mlibatizwa katika Kristo mmejivika Kristo.
28 Ni niti Juda niti Grka, ni niti sužnja niti svobodnega, ni niti moškega niti ženske; kajti vsi vi ste eno v Kristusu Jezusu.
Hakuna Myahudi wala Myunani, mtumwa wala huru, mwanaume wala mwanamke, kwa kuwa ninyi nyote ni mmoja katika Kristo Yesu.
29 Če pa ste Kristusovi, potem ste Abrahamovo seme in dediči glede na obljubo.
Kama ninyi ni wa Kristo, basi ni uzao wa Ibrahimu, warithi kwa mujibu wa ahadi.

< Galačanom 3 >