< 2 Korinčanom 1 >

1 Pavel, po Božji volji apostol Jezusa Kristusa, in naš brat Timótej Božji cerkvi, ki je v Korintu, z vsemi svetimi, ki so po vsej Ahaji:
Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, na kwa waumini wote walioko katika mkoa wote wa Akaya.
2 ›Milost bodi vam in mir od Boga, našega Očeta in od Gospoda Jezusa Kristusa.‹
Neema na iwe kwenu na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
3 Blagoslovljen bodi Bog, celó Oče našega Gospoda Jezusa Kristusa, Oče usmiljenj in Bog vse tolažbe,
Na asifiwe Mungu na Baba wa Bwana Yesu Kristo. Yeye ni Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote.
4 ki nas tolaži v vsaki naši stiski, da bomo sposobni tolažiti te, ki so v kakršnikoli težavi, s tolažbo, s katero smo mi sami potolaženi od Boga.
Mungu hutufariji sisi katika mateso yetu yote, ili kwamba tuweze kuwafariji wale walio katika mateso. Tunawafariji wengine kwa faraja ileile ambayo Mungu alitumia kutufariji sisi.
5 Kajti kakor so Kristusova trpljenja obilna v nas, tako je obilna tudi naša tolažba po Kristusu.
Kwa kuwa kama vile mateso ya Kristo huongezeka kwa ajili yetu, vile vile faraja yetu huongezeka kupitia Kristo.
6 Če pa smo stiskani, je to za vašo tolažbo in rešitev duš, ki je učinkovita v prestajanju istih trpljenj, ki jih tudi mi prenašamo; ali če smo potolaženi, je to zaradi vaše tolažbe in rešitve duš.
Lakini kama tunataabishwa, ni kwa ajili ya faraja yenu na wokovu wenu. Na kama tunafarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu. Faraja yenu inafanya kazi kikamilifu mnaposhiriki mateso kwa uvumilivu kama sisi pia tunavyoteseka.
7 In naše upanje o vas je neomajno, vedoč, da kakor ste udeleženci trpljenj, tako boste postali tudi tolažbe.
Na ujasiri wetu juu yenu ni thabiti. Tunajua kwamba kama vile ambavyo mnashiriki mateso, vile vile mnashiriki faraja.
8 Kajti nočemo, bratje, da bi bili vi nevedni o naši težavi, ki je k nam prišla v Aziji, da smo bili stiskani preko mere, nad močjo, tako zelo, da smo obupali celó nad življenjem.
Kwa kuwa hatutaki ninyi muwe wajinga, ndugu, kuhusu matatizo tuliyokuwa nayo huko Asia. Tulionewa zaidi ya vile tuwezavyo kubeba, kana kwamba hatukuwa hata na tumaini la kuishi tena.
9 Toda v sebi smo imeli smrtno obsodbo, da ne bi zaupali vase, temveč v Boga, ki obuja mrtve;
Kweli, tulikuwa na hukumu ya kifo juu yetu. Lakini hiyo ilikuwa ni kutufanya sisi tusiweke tumaini juu yetu wenyewe, badala yake tuweke tumaini katika Mungu, afufuaye wafu.
10 ki nas je osvobodil iz tako velike smrti in še osvobaja; v katerega zaupamo, da nas bo še osvobajal.
Alituokoa sisi kutoka hayo maafa ya mauti, na atatuokoa tena. Tumeweka ujasiri wetu katika yeye ya kwamba atatuokoa tena.
11 Tudi vi skupaj pomagate z molitvijo za nas, da bi bila lahko zaradi daru, podarjenega nam, s pomočjo mnogih oseb, dana zahvala z naše strani.
Atafanya hivi kama vile ninyi pia mtusaidiavyo kwa maombi yenu. Hivyo wengi watatoa shukurani kwa niaba yetu kwa ajili ya upendeleo wa neema tuliyopewa sisi kupitia maombi ya wengi.
12 Kajti naše veselje je to, pričevanje naše vesti, da smo se v svetu vedli s preprostostjo in pobožno iskrenostjo, ne z meseno modrostjo, temveč z Božjo milostjo in bolj obilno posebej do vas.
Tunajivunia hili: ushuhuda wa dhamiri yetu. Kwa kuwa ni katika nia safi na usafi wa Mungu kwamba tulienenda wenyewe katika dunia. Tumefanya hivi hasa na ninyi, na sio katika hekima ya ulimwengu, lakini badala yake ni katika neema ya Mungu.
13 Kajti ne pišemo vam nobenih drugih stvari, kakor kar berete ali spoznavate; in zaupam, da boste spoznali celó do konca;
Hatuwaandikii chochote ambacho hamwezi kukisoma au kuelewa. Ninaujasiri
14 kakor ste nas tudi vi deloma spoznali, da smo mi vaše veselje, celó kakor ste tudi vi naše na dan Gospoda Jezusa.
kwamba kwa sehemu mumekwisha kutuelewa. Na ninaujasiri kwamba katika siku ya Bwana Yesu tutakuwa sababu yenu kwa ajili ya kiburi chenu, kama vile mtakavyokuwa kwetu.
15 V tem zaupanju sem bil voljan prej priti k vam, da bi vi lahko imeli dvojno korist;
Kwa sababu nilikuwa na ujasiri kuhusu hili, nilitaka kuja kwenu kwanza, ili kwamba muweze kupokea faida ya kutembelewa mara mbili.
16 in mimo vas iti v Makedonijo in iz Makedonije ponovno priti k vam in bi bil od vas pospremljen na svoji poti proti Judeji.
Nilikuwa napanga kuwatembelea wakati nikielekea Makedonia. Tena nilitaka kuwatembelea tena wakati nikirudi kutoka Makedonia, na kisha ninyi kunituma mimi wakati nikielekea Uyahudi.
17 Ko sem bil torej takih misli, ali sem uporabil lahkomiselnost? Ali stvari, ki jih nameravam, nameravam storiti glede na meso, da bo z menoj »da, « »da« in »ne, « »ne«?
Nilipokuwa nafikiria namna hii, je, nilikuwa nasitasita? Je ninapanga mambo kulingana na viwango vya kibinadamu, ili kwamba niseme “Ndiyo, ndiyo” na “Hapana, hapana” kwa wakati mmoja?
18 Toda kakor je Bog resničen, naša beseda do vas ni bila »da« in »ne.«
Lakini kama vile Mungu alivyo mwaminifu, hatusemi vyote “Ndiyo” na “Hapana.”
19 Kajti Božji Sin, Jezus Kristus, ki je bil med vami oznanjen po nas, celó po meni in Silvánu ter Timóteju, ni bil »da« in »ne, « temveč je bil v njem »da.«
Kwa kuwa mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye Silvano, Timotheo na mimi tulimtangaza miongoni mwenu, siyo “Ndiyo” na “Hapana.” Badala yake, yeye wakati wote ni “Ndiyo.”
20 Kajti vse Božje obljube so v njem »da« in v njem »Amen« v Božjo slavo po nas.
Kwa kuwa ahadi zote za Mungu ni “Ndiyo” katika yeye. Hivyo pia kupitia yeye tunasema “Amina” kwa utukufu wa Mungu.
21 Torej tisti, ki nas z vami utrjuje v Kristusu in nas je mazilil, je Bog;
Sasa ni Mungu ambaye hututhibitisha sisi pamoja nanyi katika Kristo, na alitutuma sisi.
22 ki nas je tudi zapečatil in v naša srca dal poroštvo Duha.
Aliweka muhuri juu yetu na alitupa Roho katika mioyo yetu kama dhamana ya kile ambacho angetupatia baadaye.
23 Poleg tega kličem Boga za pričo nad svojo dušo, da doslej še nisem prišel k vam v Korint, da bi vam prizanesel.
Badala yake, namsihi Mungu kunishuhudia mimi kwamba sababu iliyonifanya nisije Korintho ni kwamba nisiwalemee ninyi.
24 Ne, ker bi imeli gospostvo nad vašo vero, temveč smo pomočniki vaše radosti; kajti stojite po veri.
Hii sio kwa sababu tunajaribu kudhibiti jinsi imani yenu inavyotakiwa kuwa. Badala yake, tunafanya pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kama mnavyosimama katika imani yenu.

< 2 Korinčanom 1 >