< От Луки святое благовествование 10 >

1 По сих же яви Господь и инех седмьдесят, и посла их по двема пред лицем Своим во всяк град и место, аможе хотяше Сам ити:
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 глаголаше же к ним: жатва убо многа, делателей же мало: молитеся убо Господину жатве, да изведет делатели на жатву Свою.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Идите: се Аз посылаю вы яко агнцы посреде волков.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Не носите влагалища, ни пиры, ни сапог: и ни когоже на пути целуйте.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 В оньже аще дом внидете, первее глаголите: мир дому сему:
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 и аще убо будет ту сын мира, почиет на нем мир ваш: аще ли же ни, к вам возвратится:
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 в том же дому пребывайте, ядуще и пиюще, яже суть у них: достоин бо есть делатель мзды своея. Не преходите из дому в дом.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 И в оньже аще град входите, и приемлют вы, ядите предлагаемая вам:
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 и изцелите недужныя, иже суть в нем, и глаголите им: приближися на вы Царствие Божие.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 И в оньже аще град входите, и не приемлют вас, изшедше на распутия его, рцыте:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 и прах, прилепший нам от града вашего, оттрясаем вам. Обаче сие ведите, яко приближися на вы Царствие Божие:
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 глаголю вам, яко Содомляном в день той отраднее будет, неже граду тому.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Горе тебе, Хоразине, горе тебе, Вифсаидо: яко аще в Тире и Сидоне быша силы были бывшыя в ваю, древле убо во вретищи и пепеле седяще покаялися быша:
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 обаче Тиру и Сидону отраднее будет на суде, неже вама.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 И ты, Капернауме, иже до небес вознесыйся, до ада низведешися. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Слушаяй вас, Мене слушает: и отметаяйся вас, Мене отметается: отметаяйся же Мене, отметается Пославшаго Мя.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Возвратишася же седмьдесят с радостию, глаголюще: Господи, и беси повинуются нам о имени Твоем.
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Рече же им: видех сатану яко молнию с небесе спадша.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Се, даю вам власть наступати на змию и на скорпию и на всю силу вражию: и ничесоже вас вредит:
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 обаче о сем не радуйтеся, яко дуси вам повинуются: радуйтеся же, яко имена ваша написана суть на небесех.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 В той час возрадовася духом Иисус и рече: исповедаютися, Отче, Господи небесе и земли, яко утаил еси сия от премудрых и разумных, и открыл еси та младенцем: ей, Отче, яко тако бысть благоволение пред Тобою.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 И обращься ко учеником, рече: вся Мне предана быша от Отца Моего: и никтоже весть, кто есть Сын, токмо Отец: и кто есть Отец, токмо Сын, и емуже аще хощет Сын открыти.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 И обращься ко учеником, един рече: блажени очи видящии, яже видите:
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 глаголю бо вам, яко мнози пророцы и царие восхотеша видети, яже вы видите, и не видеша: и слышати, яже слышите, и не слышаша.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 И се, законник некий воста, искушая Его и глаголя: Учителю, что сотворив, живот вечный наследую? (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 Он же рече к нему: в законе что писано есть? Како чтеши?
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 Он же отвещав рече: возлюбиши Господа Бога твоего от всего сердца твоего, и от всея души твоея, и всею крепостию твоею, и всем помышлением твоим: и ближняго своего яко сам себе.
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Рече же ему: право отвещал еси: сие сотвори, и жив будеши.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 Он же хотя оправдитися сам, рече ко Иисусу: и кто есть ближний мой?
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Отвещав же Иисус рече: человек некий схождаше от Иерусалима во Иерихон, и в разбойники впаде, иже совлекше его, и язвы возложше отидоша, оставльше едва жива суща.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 По случаю же священник некий схождаше путем тем, и видев его, мимоиде.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 Такожде же и левит, быв на том месте, пришед и видев, мимоиде.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 Самарянин же некто грядый, прииде над него, и видев его, милосердова:
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 и приступль обвяза струпы его, возливая масло и вино: всадив же его на свой скот, приведе его в гостинницу и прилежа ему:
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 и наутрия изшед, иземь два сребреника, даде гостиннику и рече ему: прилежи ему: и еже аще прииждивеши, аз егда возвращуся, воздам ти.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Кто убо от тех триех ближний мниттися быти впадшему в разбойники?
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 Он же рече: сотворивый милость с ним. Рече же ему Иисус: иди, и ты твори такожде.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Бысть же ходящым им, и Сам вниде в весь некую: жена же некая именем Марфа прият Его в дом свой:
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 и сестра ей бе нарицаемая Мариа, яже и седши при ногу Иисусову, слышаше слово Его.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 Марфа же молвяше о мнозе службе, ставши же рече: Господи, не брежеши ли, яко сестра моя едину мя остави служити? Рцы убо ей, да ми поможет.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Отвещав же Иисус рече ей: Марфо, Марфо, печешися и молвиши о мнозе,
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 едино же есть на потребу. Мариа же благую часть избра, яже не отимется от нея.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< От Луки святое благовествование 10 >