< Первое послание к Тимофею 6 >

1 Елицы суть под игом раби, своих господий всякия чести да сподобляют, да имя Божие не хулится и учение.
Watumwa wote wanapaswa kuwaheshimu wakuu wao ili kusiwe na sababu ya watu kulitukana jina la Mungu na mafundisho yetu.
2 Имущии же верных господий да не нерадят о них, понеже братия суть: но паче да работают, зане верни суть и возлюблени, иже благодать восприемлющии. Сия учи и моли.
Watumwa ambao wakuu wao ni Wakristo wasiwadharau kwani ni ndugu zao. Badala yake, wanapaswa kuwatumikia hata vizuri zaidi, maana hao wanaopata faida kutokana na kazi yao ni waumini ambao wanawapenda. Unapaswa kufundisha na kuhubiri mambo haya.
3 Аще ли кто инако учит и не приступает к здравым словесем Господа нашего Иисуса Христа и учению, еже по благоверию,
Mtu yeyote anayefundisha kinyume cha mambo haya, na ambaye hakubaliani na maneno ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo na mafundisho ya dini,
4 разгордеся, ничтоже ведый, но недугуяй о стязаниих и словопрениих, от нихже бывает зависть, рвение, хулы, непщевания лукава,
huyo amejaa majivuno na wala hajui chochote. Ni mtu wa kupenda ubishi na magombano juu ya maneno matupu, na hiyo husababisha wivu, ugomvi, matusi, shuku mbaya,
5 беседы злыя растленных человеков умом и лишенных истины, непщующих приобретение быти благочестие. Отступай от таковых.
na ubishi usio na kikomo kutoka kwa watu ambao akili zao zimeharibika, na ambao hawana tena ukweli. Wanadhani dini ni njia ya kujipatia utajiri.
6 Есть же снискание велие благочестие с доволством.
Kweli dini humfanya mtu awe tajiri sana, ikiwa anatosheka na vitu alivyo navyo.
7 Ничтоже бо внесохом в мир сей: яве, яко ниже изнести что можем.
Maana hatukuleta kitu chochote hapa duniani, wala hatutachukua chochote.
8 Имеюще же пищу и одеяние, сими доволни будем.
Kwa hiyo basi, kama tunacho chakula na mavazi, tunapaswa kuridhika navyo.
9 А хотящии богатитися впадают в напасти и сеть, и в похоти многи несмысленны и вреждающыя, яже погружают человеки во всегубителство и погибель:
Lakini wale wanaotaka kutajirika huanguka katika majaribu, na kunaswa katika mtego wa tamaa nyingi mbaya za kipumbavu, ambazo huwavuta mpaka kwenye uharibifu na maangamizi.
10 корень бо всем злым сребролюбие есть, егоже нецыи желающе заблудиша от веры, и себе пригвоздиша болезнем многим.
Kwa maana kupenda sana fedha ni chanzo cha uovu wote. Watu wengine wametamani sana kupata fedha hata wakatangatanga mbali na imani, na wameivunja mioyo yao kwa huzuni nyingi.
11 Ты же, о, человече Божий, сих бегай: гони же правду, благочестие, веру, любовь, терпение, кротость:
Lakini wewe, mtu wa Mungu, jiepushe na mambo hayo. Zingatia uadilifu, uchaji wa Mungu, imani, mapendo, subira na unyenyekevu.
12 подвизайся добрым подвигом веры, емлися за вечную жизнь, в нюже и зван был еси, и исповедал еси доброе исповедание пред многими свидетели. (aiōnios g166)
Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi. (aiōnios g166)
13 Завещаваю ти пред Богом оживляющим всяческая, и Христом Иисусом свидетелствовавшим при Понтийстем Пилате доброе исповедание:
Mbele ya Mungu anayevipa vitu vyote uhai, na mbele ya Yesu Kristo aliyetoa ushahidi na kukiri ukweli mbele ya Pontio Pilato,
14 соблюсти тебе заповедь нескверну и незазорну, даже до явления Господа нашего Иисуса Христа,
nakuamuru ushike maagizo yako na kuyatii kwa uaminifu mpaka Siku ile atakapotokea Bwana wetu Yesu Kristo.
15 еже во своя времена явит блаженный и един сильный, Царь царствующих и Господь господствующих,
Kutokea kwake kutafanyika wakati ufaao uliopangwa na Mungu mwenye heri na aliye Mtawala pekee, Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
16 един имеяй безсмертие и во свете живый неприступнем, Егоже никтоже видел есть от человек, ниже видети может: емуже честь и держава вечная. Аминь. (aiōnios g166)
Yeye peke yake anaishi milele, katika mwanga usioweza kukaribiwa na mtu. Hakuna mtu aliyepata kumwona au awezaye kumwona. Kwake iwe heshima na uwezo wa milele! Amina. (aiōnios g166)
17 Богатым в нынешнем веце запрещай не высокомудрствовати, ниже уповати на богатство погибающее, но на Бога жива, дающаго нам вся обилно в наслаждение: (aiōn g165)
Waamuru watu walio matajiri katika mambo ya maisha ya sasa, wasijivune, wasiweke tumaini lao katika mali isiyoweza kutegemewa; bali wamtegemee Mungu, ambaye kwa ukarimu hutupatia vitu vyote tuvifurahie. (aiōn g165)
18 благое делати, богатитися в делех добрых, благоподатливым быти, общителным,
Waamuru watende mema, wawe matajiri katika matendo mema, na wawe wakarimu na walio tayari kuwashirikisha wengine mali zao.
19 сокровищующе себе основание добро в будущее, да приимут вечную жизнь.
Kwa namna hiyo watajiwekea hazina ambayo itakuwa kwao msingi imara kwa wakati ujao. Hapo wataweza kujipatia uzima ambao ni uzima wa kweli.
20 О, Тимофее, предание сохрани, уклоняяся скверных суесловий и прекословий лжеименнаго разума:
Timotheo, tunza salama yote yale uliyokabidhiwa. Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ubishi wa kipumbavu juu ya kile wanachokiita watu wengine: “Elimu”.
21 о немже нецыи хвалящеся, о вере погрешиша. Благодать с тобою. Аминь.
Maana wengine wamejidai kuwa na hiyo elimu, na matokeo yake wamepoteza imani. Nawatakieni nyote neema!

< Первое послание к Тимофею 6 >