< Псалми 78 >

1 Чуј, народе мој, наук мој, пригни ухо своје к речима уста мојих.
Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 Отварам за причу уста своја, казаћу старе приповетке.
Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
3 Шта слушасмо и дознасмо, и што нам казиваше оци наши,
Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
4 Нећемо затајити од деце њихове, нараштају позном јавићемо славу Господњу и силу Његову и чудеса која је учинио.
Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
5 Сведочанство подиже у Јакову, и у Израиљу постави закон, који даде оцима нашим да га предаду деци својој;
Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
6 Да би знао потоњи нараштај, деца која ће се родити, па и они да би казивали својој деци.
Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
7 Да полажу на Бога надање своје, и не заборављају дела Божијих, и заповести Његове да држе;
Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
8 И да не буду као оци њихови, род неваљао и упоран, род који не беше чврст срцем својим, нити веран Богу духом својим.
Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
9 Синови Јефремови наоружани, који стрељају из лука, вратише се натраг, кад беше бој.
Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
10 Не сачуваше завет Божји, и по закону Његовом не хтеше ходити.
Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
11 Заборавише дела Његова, и чудеса, која им је показао,
Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
12 Како пред очима њиховим учини чудеса у земљи мисирској, на пољу Соану;
Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
13 Раздвоји море, и проведе их, од воде начини зид;
Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
14 И води их дању облаком, и сву ноћ светлим огњем;
Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
15 Раскида стене у пустињи, и поји их као из велике бездане;
Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
16 Изводи потоке из камена, и води воду рекама.
Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
17 Али они још једнако грешише Њему, и гневише Вишњег у пустињи.
Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
18 И кушаше Бога у срцу свом, иштући јела по вољи својој,
Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
19 И викаше на Бога, и рекоше: "Може ли Бог зготовити трпезу у пустињи?"
Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
20 Ево! Он удари у камен, и потече вода, и реке устадоше; може ли и хлеба дати? Хоће ли и меса поставити народу свом?
Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
21 Господ чу и разљути се, и огањ се разгоре на Јакова, и гнев се подиже на Израиља.
Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
22 Јер не вероваше Богу и не уздаше се у помоћ Његову.
kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
23 Тада заповеди облацима одозго, и отвори врата небеска,
Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
24 И пусти, те им подажде мана за јело, и хлеб небески даде им.
Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
25 Хлеб анђеоски јеђаше човек; посла им јела до ситости.
Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
26 Пусти небом устоку, и наведе силом својом југ;
Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
27 И као прахом засу их месом, и као песком морским птицама крилатим;
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
28 Побаца их сред логора њиховог, око шатора њихових.
Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
29 И наједоше се и даде им шта су желели.
Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
30 Али их још и не прође жеља, још беше јело у устима њиховим,
Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31 Гнев се Божји подиже на њих и помори најјаче међу њима, и младиће у Израиљу поби.
Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32 Преко свега тога још грешише, и не вероваше чудесима Његовим.
Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33 И пусти, те дани њихови пролазише узалуд, и године њихове у страху.
Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34 Кад их убијаше, онда притецаху к Њему, и обраћаху се и искаху Бога;
Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35 И помињаху да је Бог одбрана њихова, и Вишњи Избавитељ њихов.
Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36 Ласкаху Му устима својим, и језиком својим лагаху Му.
Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37 А срце њихово не беше Њему верно, и не беху тврди у завету Његовом.
Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38 Али Он беше милостив, и покриваше грех, и не помори их, често заустављаше гнев свој, и не подизаше све јарости своје.
Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39 Опомињаше се да су тело, ветар, који пролази и не враћа се.
Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40 Колико Га пута расрдише у пустињи, и увредише у земљи где се не живи!
Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41 Све наново кушаше Бога, и Свеца Израиљевог дражише.
Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42 Не сећаше се руке Његове и дана, у који их избави из невоље,
Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43 У који учини у Мисиру знаке своје и чудеса своја на пољу Соану;
alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44 И проврже у крв реке њихове и потоке њихове, да не могоше пити.
Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45 Посла на њих бубине да их кољу, и жабе да их море.
Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46 Летину њихову даде црву, и муку њихову скакавцима.
Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47 Винограде њихове поби градом, и смокве њихове сланом.
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
48 Граду предаде стоку њихову, и стада њихова муњи.
Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
49 Посла на њих огњени гнев свој, јарост, срдњу и мржњу, чету злих анђела.
Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
50 Равни стазу гневу свом, не чува душе њихове од смрти, и живот њихов предаде помору.
Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
51 Поби све првенце у Мисиру, први пород по колибама Хамовим.
Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
52 И поведе народ свој као овце, и води их као стадо преко пустиње.
Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
53 Води их поуздано, и они се не бојаше, а непријатеље њихове затрпа море.
Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
54 И доведе их на место светиње своје, на ову гору, коју задоби десница Његова.
Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
55 Одагна испред лица њиховог народе; жребом раздели њихово достојање, и по шаторима њиховим насели колена Израиљева.
Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
56 Али они кушаше и срдише Бога Вишњег и уредбе Његове не сачуваше.
Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
57 Одусташе и одвргоше се, као и оци њихови, слагаше као рђав лук.
Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
58 Увредише Га висинама својим, и идолима својим раздражише Га.
Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59 Бог чу и разгневи се и расрди се на Израиља веома.
Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60 Остави насеље своје у Силому, шатор, у коме живљаше с људима.
Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61 И оправи у ропство славу своју и красоту своју у руке непријатељеве.
Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62 И предаде мачу народ свој, и на достојање своје запламте се.
Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63 Младиће његове једе огањ, и девојкама његовим не певаше сватовских песама;
Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64 Свештеници његови падаше од мача, и удовице његове не плакаше.
Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
65 Најпосле, као иза сна пробуди се Господ, прену се као јунак кад се напије вина.
Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
66 И поби непријатеље своје с леђа, вечној срамоти предаде их.
Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
67 И не хте шатор Јосифов, и колено Јефремово не изабра.
Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
68 Него изабра колено Јудино, гору Сион, која Му омиле.
Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
69 И сагради светињу своју као горње своје станове, и као земљу утврди је довека.
Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
70 И изабра Давида, слугу свог, и узе га од торова овчијих,
Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
71 И од дојилица доведе га да пасе народ Његов, Јакова, и наследство Његово, Израиља.
Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
72 И он их пасе чистим срцем, и води их мудрим рукама.
Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.

< Псалми 78 >