< Књига о Јову 12 >

1 А Јов одговори и рече:
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 Да, ви сте људи, и с вама ће умрети мудрост.
“Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
3 И ја имам срце као и ви, нити сам гори од вас; и у кога нема тога?
Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
4 На подсмех сам пријатељу свом, који кад зове Бога одазове му се; на подсмех је праведни и добри.
Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
5 Бачен је луч по мишљењу срећног онај који хоће да попузне.
Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
6 Мирне су колибе лупешке, и без страха су који гневе Бога, њима Бог даје све у руке.
Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
7 Запитај стоку, научиће те; или птице небеске, казаће ти.
Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
8 Или се разговори са земљом, научиће те, и рибе ће ти морске приповедити.
Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
9 Ко не зна од свега тога да је рука Господња то учинила?
Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
10 Коме је у руци душа свега живог и дух сваког тела човечијег.
Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
11 Не распознаје ли ухо речи као што грло куша јело?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
12 У старца је мудрост, и у дугом веку разум.
Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
13 У Њега је мудрост и сила, у Њега је савет и разум.
Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
14 Гле, Он разгради, и не може се опет саградити; затвори човека, и не може се отворити.
Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
15 Гле, устави воде, и пресахну; пусти их, и испреврћу земљу.
Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
16 У Њега је јачина и мудрост, Његов је који је преварен и који вара.
Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
17 Он доводи саветнике у лудило, и судије обезумљује.
Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
18 Он разрешује појас царевима, и опасује бедра њихова.
Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
19 Он доводи кнезове у лудило, и обара јаке.
Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
20 Он узима беседу речитима, и старцима узима разум.
Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
21 Он сипа срамоту на кнезове, и распасује јунаке.
Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
22 Он открива дубоке ствари испод таме, и изводи на видело сен смртни.
Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
23 Он умножава народе и затире их, расипа народе и сабира.
Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
24 Он одузима срце главарима народа земаљских, и заводи их у пустињу где нема пута,
Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
25 Да пипају по мраку без видела, и чини да тумарају као пијани.
Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.

< Књига о Јову 12 >