< Псалтирь 107 >

1 Аллилуия. Славьте Господа, ибо Он благ, ибо вовек милость Его!
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Так да скажут избавленные Господом, которых избавил Он от руки врага,
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 и собрал от стран, от востока и запада, от севера и моря.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Они блуждали в пустыне по безлюдному пути и не находили населенного города;
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 терпели голод и жажду, душа их истаевала в них.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он избавил их от бедствий их,
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 и повел их прямым путем, чтобы они шли к населенному городу.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 ибо Он насытил душу жаждущую и душу алчущую исполнил благами.
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 Они сидели во тьме и тени смертной, окованные скорбью и железом;
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 ибо не покорялись словам Божиим и небрегли о воле Всевышнего.
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Он смирил сердце их работами; они преткнулись, и не было помогающего.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 вывел их из тьмы и тени смертной, и расторгнул узы их.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих:
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 ибо Он сокрушил врата медные и вереи железные сломил.
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Безрассудные страдали за беззаконные пути свои и за неправды свои;
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 от всякой пищи отвращалась душа их, и они приближались ко вратам смерти.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он спас их от бедствий их;
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 послал слово Свое и исцелил их, и избавил их от могил их.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 Да приносят Ему жертву хвалы и да возвещают о делах Его с пением!
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Отправляющиеся на кораблях в море, производящие дела на больших водах,
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 видят дела Господа и чудеса Его в пучине:
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 Он речет, - и восстанет бурный ветер и высоко поднимает волны его:
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 восходят до небес, нисходят до бездны; душа их истаевает в бедствии;
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 они кружатся и шатаются, как пьяные, и вся мудрость их исчезает.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 Но воззвали к Господу в скорби своей, и Он вывел их из бедствия их.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 Он превращает бурю в тишину, и волны умолкают.
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 И веселятся, что они утихли, и Он приводит их к желаемой пристани.
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 Да славят Господа за милость Его и за чудные дела Его для сынов человеческих!
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Да превозносят Его в собрании народном и да славят Его в сонме старейшин!
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 Он превращает реки в пустыню и источники вод - в сушу,
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 землю плодородную - в солончатую, за нечестие живущих на ней.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 Он превращает пустыню в озеро, и землю иссохшую - в источники вод;
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 и поселяет там алчущих, и они строят город для обитания;
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 засевают поля, насаждают виноградники, которые приносят им обильные плоды.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 Он благословляет их, и они весьма размножаются, и скота их не умаляет.
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 Уменьшились они и упали от угнетения, бедствия и скорби,
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 Он изливает бесчестие на князей и оставляет их блуждать в пустыне, где нет путей.
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 Бедного же извлекает из бедствия и умножает род его, как стада овец.
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 Праведники видят сие и радуются, а всякое нечестие заграждает уста свои.
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 Кто мудр, тот заметит сие и уразумеет милость Господа.
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Псалтирь 107 >