< Псалтирь 102 >

1 Молитва страждущего, когда он унывает и изливает пред Господом печаль свою. Господи! услышь молитву мою, и вопль мой да придет к Тебе.
Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana. Ee Bwana, usikie maombi yangu, kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.
2 Не скрывай лица Твоего от меня; в день скорби моей приклони ко мне ухо Твое; в день, когда воззову к Тебе, скоро услышь меня;
Usinifiche uso wako ninapokuwa katika shida. Unitegee sikio lako, ninapoita, unijibu kwa upesi.
3 ибо исчезли, как дым, дни мои, и кости мои обожжены, как головня;
Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi, mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.
4 сердце мое поражено, и иссохло, как трава, так что я забываю есть хлеб мой;
Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani, ninasahau kula chakula changu.
5 от голоса стенания моего кости мои прильпнули к плоти моей.
Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu, nimebakia ngozi na mifupa.
6 Я уподобился пеликану в пустыне; я стал как филин на развалинах;
Nimekuwa kama bundi wa jangwani, kama bundi kwenye magofu.
7 не сплю и сижу, как одинокая птица на кровле.
Nilalapo sipati usingizi, nimekuwa kama ndege mpweke kwenye paa la nyumba.
8 Всякий день поносят меня враги мои, и злобствующие на меня клянут мною.
Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki, wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.
9 Я ем пепел, как хлеб, и питье мое растворяю слезами,
Ninakula majivu kama chakula changu na nimechanganya kinywaji changu na machozi
10 от гнева Твоего и негодования Твоего, ибо Ты вознес меня и низверг меня.
kwa sababu ya ghadhabu yako kuu, kwa maana umeniinua na kunitupa kando.
11 Дни мои - как уклоняющаяся тень, и я иссох, как трава.
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
12 Ты же, Господи, вовек пребываешь, и память о Тебе в род и род.
Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13 Ты восстанешь, умилосердишься над Сионом, ибо время помиловать его, - ибо пришло время;
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
14 ибо рабы Твои возлюбили и камни его, и о прахе его жалеют.
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15 И убоятся народы имени Господня, и все цари земные - славы Твоей.
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16 Ибо созиждет Господь Сион и явится во славе Своей;
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
17 призрит на молитву беспомощных и не презрит моления их.
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
18 Напишется о сем для рода последующего, и поколение грядущее восхвалит Господа,
Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19 ибо Он приникнул со святой высоты Своей, с небес призрел Господь на землю,
“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
20 чтобы услышать стон узников, разрешить сынов смерти,
kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21 дабы возвещали на Сионе имя Господне и хвалу Его - в Иерусалиме,
Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
22 когда соберутся народы вместе и царства для служения Господу.
wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
23 Изнурил Он на пути силы мои, сократил дни мои.
Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
24 Я сказал: Боже мой! не восхити меня в половине дней моих. Твои лета в роды родов.
Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25 В начале Ты, Господи, основал землю, и небеса - дело Твоих рук;
Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26 они погибнут, а Ты пребудешь; и все они, как риза, обветшают, и, как одежду, Ты переменишь их, и изменятся;
Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
27 но Ты - тот же, и лета Твои не кончатся.
Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
28 Сыны рабов Твоих будут жить, и семя их утвердится пред лицем Твоим.
Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”

< Псалтирь 102 >