< Притчи 17 >

1 Лучше кусок сухого хлеба, и с ним мир, нежели дом, полный заколотого скота, с раздором.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Разумный раб господствует над беспутным сыном и между братьями разделит наследство.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Плавильня - для серебра, и горнило - для золота, а сердца испытывает Господь.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Злодей внимает устам беззаконным, лжец слушается языка пагубного.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Кто ругается над нищим, тот хулит Творца его; кто радуется несчастью, тот не останется ненаказанным.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Венец стариков - сыновья сыновей, и слава детей - родители их.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Неприлична глупому важная речь, тем паче знатному - уста лживые.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Подарок - драгоценный камень в глазах владеющего им: куда ни обратится он, успеет.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Прикрывающий проступок ищет любви; а кто снова напоминает о нем, тот удаляет друга.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 На разумного сильнее действует выговор, нежели на глупого сто ударов.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Возмутитель ищет только зла; поэтому жестокий ангел будет послан против него.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Лучше встретить человеку медведицу, лишенную детей, нежели глупца с его глупостью.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Кто за добро воздает злом, от дома того не отойдет зло.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 Начало ссоры - как прорыв воды; оставь ссору прежде, нежели разгорелась она.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 Оправдывающий нечестивого и обвиняющий праведного - оба мерзость пред Господом.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 К чему сокровище в руках глупца? Для приобретения мудрости у него нет разума.
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Друг любит во всякое время и, как брат, явится во время несчастья.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 Человек малоумный дает руку и ручается за ближнего своего.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 Кто любит ссоры, любит грех, и кто высоко поднимает ворота свои, тот ищет падения.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Коварное сердце не найдет добра, и лукавый язык попадет в беду.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Родил кто глупого, - себе на горе, и отец глупого не порадуется.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 Веселое сердце благотворно, как врачевство, а унылый дух сушит кости.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Нечестивый берет подарок из пазухи, чтобы извратить пути правосудия.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 Мудрость - пред лицoм у разумного, а глаза глупца - на конце земли.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Глупый сын - досада отцу своему и огорчение для матери своей.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Нехорошо и обвинять правого, и бить вельмож за правду.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Разумный воздержан в словах своих, и благоразумный хладнокровен.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 И глупец, когда молчит, может показаться мудрым, и затворяющий уста свои - благоразумным.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Притчи 17 >