< Иов 39 >

1 Знаешь ли ты время, когда рождаются дикие козы на скалах, и замечал ли роды ланей?
Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
2 можешь ли расчислить месяцы беременности их? и знаешь ли время родов их?
Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
3 Они изгибаются, рождая детей своих, выбрасывая свои ноши;
Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
4 дети их приходят в силу, растут на поле, уходят и не возвращаются к ним.
Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
5 Кто пустил дикого осла на свободу, и кто разрешил узы онагру,
Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
6 которому степь Я назначил домом и солончаки - жилищем?
ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
7 Он посмевается городскому многолюдству и не слышит криков погонщика,
Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
8 по горам ищет себе пищи и гоняется за всякою зеленью.
Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
9 Захочет ли единорог служить тебе и переночует ли у яслей твоих?
Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
10 Можешь ли веревкою привязать единорога к борозде, и станет ли он боронить за тобою поле?
Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
11 Понадеешься ли на него, потому что у него сила велика, и предоставишь ли ему работу твою?
Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
12 Поверишь ли ему, что он семена твои возвратит и сложит на гумно твое?
Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
13 Ты ли дал красивые крылья павлину и перья и пух страусу?
Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
14 Он оставляет яйца свои на земле, и на песке согревает их,
Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
15 и забывает, что нога может раздавить их и полевой зверь может растоптать их;
husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
16 он жесток к детям своим, как бы не своим, и не опасается, что труд его будет напрасен;
Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
17 потому что Бог не дал ему мудрости и не уделил ему смысла;
kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
18 а когда поднимется на высоту, посмеивается коню и всаднику его.
Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
19 Ты ли дал коню силу и облек шею его гривою?
Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
20 Можешь ли ты испугать его, как саранчу? Храпение ноздрей его - ужас;
Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
21 роет ногою землю и восхищается силою; идет навстречу оружию;
Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
22 он смеется над опасностью и не робеет и не отворачивается от меча;
Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
23 колчан звучит над ним, сверкает копье и дротик;
Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
24 в порыве и ярости он глотает землю и не может стоять при звуке трубы;
Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
25 при трубном звуке он издает голос: гу! гу! и издалека чует битву, громкие голоса вождей и крик.
Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
26 Твоею ли мудростью летает ястреб и направляет крылья свои на полдень?
Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
27 По твоему ли слову возносится орел и устрояет на высоте гнездо свое?
Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
28 Он живет на скале и ночует на зубце утесов и на местах неприступных;
Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
29 оттуда высматривает себе пищу: глаза его смотрят далеко;
Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
30 птенцы его пьют кровь, и где труп, там и он.
Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.

< Иов 39 >