< Иов 32 >

1 Когда те три мужа перестали отвечать Иову, потому что он был прав в глазах своих,
Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
2 тогда воспылал гнев Елиуя, сына Варахиилова, Вузитянина из племени Рамова: воспылал гнев его на Иова за то, что он оправдывал себя больше, нежели Бога,
Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
3 а на трех друзей его воспылал гнев его за то, что они не нашли, что отвечать, а между тем обвиняли Иова.
Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
4 Елиуй ждал, пока Иов говорил, потому что они летами были старше его.
Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
5 Когда же Елиуй увидел, что нет ответа в устах тех трех мужей, тогда воспылал гнев его.
Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
6 И отвечал Елиуй, сын Варахиилов, Вузитянин, и сказал: я молод летами, а вы - старцы; поэтому я робел и боялся объявлять вам мое мнение.
Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
7 Я говорил сам себе: пусть говорят дни, и многолетие поучает мудрости.
Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
8 Но дух в человеке и дыхание Вседержителя дает ему разумение.
Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
9 Не многолетние только мудры, и не старики разумеют правду.
Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
10 Поэтому я говорю: выслушайте меня, объявлю вам мое мнение и я.
“Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
11 Вот, я ожидал слов ваших, - вслушивался в суждения ваши, доколе вы придумывали, что сказать.
Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
12 Я пристально смотрел на вас, и вот никто из вас не обличает Иова и не отвечает на слова его.
niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
13 Не скажите: мы нашли мудрость: Бог опровергнет его, а не человек.
Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
14 Если бы он обращал слова свои ко мне, то я не вашими речами отвечал бы ему.
Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
15 Испугались, не отвечают более; перестали говорить.
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16 И как я ждал, а они не говорят, остановились и не отвечают более,
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17 то и я отвечу с моей стороны, объявлю мое мнение и я,
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18 ибо я полон речами, и дух во мне теснит меня.
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19 Вот, утроба моя, как вино неоткрытое: она готова прорваться, подобно новым мехам.
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20 Поговорю, и будет легче мне; открою уста мои и отвечу.
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21 На лице человека смотреть не буду и никакому человеку льстить не стану,
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22 потому что я не умею льстить: сейчас убей меня, Творец мой.
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.

< Иов 32 >