< Иов 30 >

1 А ныне смеются надо мною младшие меня летами, те, которых отцов я не согласился бы поместить с псами стад моих.
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 И сила рук их к чему мне? Над ними уже прошло время.
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Бедностью и голодом истощенные, они убегают в степь безводную, мрачную и опустевшую;
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 щиплют зелень подле кустов, и ягоды можжевельника - хлеб их.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Из общества изгоняют их, кричат на них, как на воров,
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 чтобы жили они в рытвинах потоков, в ущельях земли и утесов.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Ревут между кустами, жмутся под терном.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Люди отверженные, люди без имени, отребье земли!
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Их-то сделался я ныне песнью и пищею разговора их.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Они гнушаются мною, удаляются от меня и не удерживаются плевать пред лицом моим.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Так как Он развязал повод мой и поразил меня, то они сбросили с себя узду пред лицом моим.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 С правого боку встает это исчадие, сбивает меня с ног, направляет гибельные свои пути ко мне.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 А мою стезю испортили: все успели сделать к моей погибели, не имея помощника.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Они пришли ко мне, как сквозь широкий пролом; с шумом бросились на меня.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Ужасы устремились на меня; как ветер, развеялось величие мое, и счастье мое унеслось, как облако.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 И ныне изливается душа моя во мне: дни скорби объяли меня.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 Ночью ноют во мне кости мои, и жилы мои не имеют покоя.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 С великим трудом снимается с меня одежда моя; края хитона моего жмут меня.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Он бросил меня в грязь, и я стал, как прах и пепел.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Я взываю к Тебе, и Ты не внимаешь мне, - стою, а Ты только смотришь на меня.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Ты сделался жестоким ко мне, крепкою рукою враждуешь против меня.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Ты поднял меня и заставил меня носиться по ветру и сокрушаешь меня.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Так, я знаю, что Ты приведешь меня к смерти и в дом собрания всех живущих.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Верно, Он не прострет руки Своей на дом костей: будут ли они кричать при своем разрушении?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 Не плакал ли я о том, кто был в горе? не скорбела ли душа моя о бедных?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Когда я чаял добра, пришло зло; когда ожидал света, пришла тьма.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Мои внутренности кипят и не перестают; встретили меня дни печали.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Я хожу почернелый, но не от солнца; встаю в собрании и кричу.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Я стал братом шакалам и другом страусам.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Моя кожа почернела на мне, и кости мои обгорели от жара.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 И цитра моя сделалась унылою, и свирель моя - голосом плачевным.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< Иов 30 >