< Иов 26 >

1 И отвечал Иов и сказал:
Kisha Ayubu akajibu:
2 как ты помог бессильному, поддержал мышцу немощного!
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 Какой совет подал ты немудрому и как во всей полноте объяснил дело!
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 Кому ты говорил эти слова, и чей дух исходил из тебя?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 Рефаимы трепещут под водами, и живущие в них.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Преисподняя обнажена пред Ним, и нет покрывала Аваддону. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 Он распростер север над пустотою, повесил землю ни на чем.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Он заключает воды в облаках Своих, и облако не расседается под ними.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Он поставил престол Свой, распростер над ним облако Свое.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 Черту провел над поверхностью воды, до границ света со тьмою.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Столпы небес дрожат и ужасаются от грозы Его.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 Силою Своею волнует море и разумом Своим сражает его дерзость.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 От духа Его - великолепие неба; рука Его образовала быстрого скорпиона.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Вот, это части путей Его; и как мало мы слышали о Нем! А гром могущества Его кто может уразуметь?
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Иов 26 >