< 1-я Паралипоменон 2 >

1 Вот сыновья Израиля: Рувим, Симеон, Левий, Иуда, Иссахар, Завулон,
Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni,
2 Дан, Иосиф, Вениамин, Неффалим, Гад и Асир.
Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri.
3 Сыновья Иуды: Ир, Онан и Силом, - трое родились у него от дочери Шуевой, Хананеянки. И был Ир, первенец Иудин, не благоугоден в очах Господа, и Он умертвил его.
Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
4 И Фамарь, невестка его, родила ему Фареса и Зару. Всех сыновей у Иуды было пятеро.
Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
5 Сыновья Фареса: Есром и Хамул.
Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
6 Сыновья Зары: Зимри, Ефан, Еман, Халкол и Дара; всех их пятеро.
Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
7 Сыновья Харми: Ахар, наведший беду на Израиля, нарушив заклятие.
Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
8 Сын Ефана: Азария.
Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
9 Сыновья Есрома, которые родились у него: Иерахмеил, Арам и Хелувай.
Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
10 Арам же родил Аминадава; Аминадав родил Наассона, князя сынов Иудиных;
Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
11 Наассон родил Салмона, Салмон родил Вооза;
Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
12 Вооз родил Овида, Овид родил Иессея;
Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
13 Иессей родил первенца своего Елиава, второго - Аминадава, третьего - Самму,
Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
14 четвертого - Нафанаила, пятого - Раддая,
wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
15 шестого - Оцема, седьмого - Давида.
wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
16 Сестры их: Саруия и Авигея. Сыновья Саруии: Авесса, Иоав и Азаил, трое.
Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
17 Авигея родила Амессу; отец же Амессы - Иефер, Измаильтянин.
Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
18 Халев, сын Есрома, родил от Азувы, жены своей, и от Иериофы, и вот сыновья его: Иешер, Шовав и Ардон.
Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni.
19 И умерла Азува; и взял себе Халев жену Ефрафу, и она родила ему Хура.
Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri.
20 Хур родил Урия, Урий родил Веселиила.
Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli.
21 После Есром вошел к дочери Махира, отца Галаадова, и взял ее, будучи шестидесяти лет, и она родила ему Сегува.
Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu.
22 Сегув родил Иаира, и было у него двадцать три города в земле Галаадской.
Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi.
23 Но Гессуряне и Сирияне взяли у них селения Иаира, Кенаф и зависящие от него города, - шестьдесят городов. Все эти города сыновей Махира, отца Галаадова.
(Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi.
24 По смерти Есрома в Халев-Ефрафе, жена Есромова, Авия, родила ему Ашхура, отца Фекои.
Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa.
25 Сыновья Иерахмеила, первенца Есромова, были: первенец Рам, за ним Вуна, Орен, Оцем и Ахия.
Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya.
26 Была у Иерахмеила и другая жена, имя ее Афара; она мать Онама.
Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu.
27 Сыновья Рама, первенца Иерахмеилова, были: Маац, Иамин и Екер.
Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri.
28 Сыновья Онама были: Шаммай и Иада. Сыновья Шаммая: Надав и Авишур.
Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri.
29 Имя жене Авишуровой Авихаиль, и она родила ему Ахбана и Молида.
Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi.
30 Сыновья Надава: Селед и Афаим. И умер Селед бездетным.
Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto.
31 Сын Афаима: Иший. Сын Ишия: Шешан. Сын Шешана: Ахлай.
Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai.
32 Сыновья Иады, брата Шаммаева: Иефер и Ионафан. Иефер умер бездетным.
Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto.
33 Сыновья Ионафана: Пелеф и Заза. Это сыновья Иерахмеила.
Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli.
34 У Шешана не было сыновей, а только дочери. У Шешана был раб, Египтянин, имя его Иарха;
Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha.
35 Шешан отдал дочь свою Иархе рабу своему в жену: и она родила ему Аттая.
Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai.
36 Аттай родил Нафана, Нафан родил Завада;
Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi,
37 Завад родил Ефлала, Ефлал родил Овида;
Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi,
38 Овид родил Иеуя, Иеуй родил Азарию;
Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria,
39 Азария родил Хелеца, Хелец родил Елеасу;
Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa,
40 Елеаса родил Сисмая, Сисмай родил Саллума;
Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu,
41 Саллум родил Иекамию, Иекамия родил Елишаму.
Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama.
42 Сыновья Халева, брата Иерахмеилова: Меша, первенец его, - он отец Зифа; и сыновья Мареши, отца Хеврона.
Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni.
43 Сыновья Хеврона: Корей и Таппуах, и Рекем и Шема.
Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema.
44 Шема родил Рахама, отца Иоркеамова, а Рекем родил Шаммая.
Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai.
45 Сын Шаммая Маон, а Маон - отец Беф-Цура.
Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri.
46 И Ефа, наложница Халевова, родила Харана, Моцу и Газеза. И Харан родил Газеза.
Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi.
47 Сыновья Иегдая: Регем, Иофам, Гешан, Пелет, Ефа и Шааф.
Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu.
48 Наложница Халевова, Мааха, родила Шевера и Фирхану;
Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana.
49 она же родила Шаафа, отца Мадманны, Шеву, отца Махбены и отца Гивеи. Дочь же Халева - Ахса.
Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa.
50 Вот сыновья Халева: сын Хур, первенец Ефрафы; Шовал, отец Кириаф-Иарима;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu,
51 Салма, отец Вифлеема; Хареф, отец Бефгадера.
Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi.
52 У Шовала, отца Кириаф-Иарима, были сыновья: Гарое, Хаци, Галменюхот.
Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi,
53 Племена Кириаф-Иарима: Ифрияне, Футияне, Шумафане и Мидраитяне. От сих произошли Цоряне и Ештаоляне.
pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli.
54 Сыновья Салмы: Вифлеемляне и Нетофафяне, венец дома Иоавова и половина Менухотян - Цоряне,
Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori,
55 и племена Соферийцев, живших в Иабеце, Тирейцы, Шимейцы, Сухайцы: это Кинеяне, происшедшие от Хамафа, отца Бетрехава.
pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.

< 1-я Паралипоменон 2 >