< 1-я Паралипоменон 4 >

1 Сыновья Иуды: Фарес, Есром, Харми, Хур и Шовал.
Wana wa Yuda walikuwa: Peresi, Hesroni, Karmi, Huri na Shobali.
2 Реаия, сын Шовала, родил Иахафа; Иахаф родил Ахума и Лагада: от них племена Цорян.
Reaya mwana wa Shobali akamzaa Yahathi, Yahathi akawazaa Ahumai na Lahadi. Hizi ndizo zilizokuwa koo za Wasorathi.
3 И сии сыновья Етама: Изреель, Ишма и Идбаш, и сестра их, по имени Гацлелпони,
Hawa ndio waliokuwa wana wa Etamu: Yezreeli, Ishma na Idbashi. Dada yao aliitwa Haselelponi.
4 Пенуел, отец Гедора, и Езер, отец Хуша. Вот сыновья Хура, первенца Ефрафы, отца Вифлеема.
Penueli akamzaa Gedori, naye Ezeri akamzaa Husha. Hawa walikuwa wazao wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi, na baba yake Bethlehemu.
5 У Ахшура, отца Фекои, были две жены: Хела и Наара.
Ashuri baba yake Tekoa alikuwa na wake wawili, Hela na Naara.
6 И родила ему Наара Ахузама, Хефера, Фимни и Ахашфари; это сыновья Наары.
Hawa walikuwa wazao wa Naara: Ahuzamu, Heferi, Temeni na Haahashtari.
7 Сыновья Хелы: Цереф, Цохар и Ефнан.
Wana wa Hela walikuwa: Serethi, Sohari, Ethnani,
8 Коц родил: Анува и Цовева и племена Ахархела, сына Гарумова.
na Kosi ambaye aliwazaa Anubi, Sobeba na jamaa zote za Aharheli mwana wa Harumu.
9 Иавис был знаменитее своих братьев. Мать дала ему имя Иавис, сказав: я родила его с болезнью.
Yabesi aliheshimiwa kuliko ndugu zake. Mama yake alimwita Yabesi, akisema, “Nilimzaa kwa huzuni.”
10 И воззвал Иавис к Богу Израилеву и сказал: о, если бы Ты благословил меня Твоим благословением, распространил пределы мои, и рука Твоя была со мною, охраняя меня от зла, чтобы я не горевал!... И Бог ниспослал ему, чего он просил.
Yabesi akamlilia Mungu wa Israeli akisema, “Ee Mungu, laiti ungenibariki kweli kweli na kuipanua mipaka yangu! Mkono wako na uwe pamoja nami, uniepushe na uovu ili nisidhurike!” Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba.
11 Хелув же, брат Шухи, родил Махира; он есть отец Ештона.
Kelubu, nduguye Shuha, akamzaa Mehiri, naye Mehiri akamzaa Eshtoni.
12 Ештон родил Беф-Рафу, Пасеаха и Техинну, отца города Нааса брата Селома Кенезиина и Ахазова; это жители Рехи.
Eshtoni akawazaa Beth-Rafa, Pasea na Tehina. Tehina alikuwa baba wa Iri-Nahashi. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Reka.
13 Сыновья Кеназа: Гофониил и Сераия. Сын Гофониила: Хафаф.
Wana wa Kenazi walikuwa: Othnieli na Seraya. Wana wa Othnieli walikuwa: Hathathi na Meonathai.
14 Меонофай родил Офру, а Сераия родил Иоава, родоначальника долины плотников, потому что они были плотники.
Meonathai akamzaa Ofra. Seraya akamzaa Yoabu, baba wa Ge-Harashimu. Liliitwa hivyo kwa sababu watu walioishi humo walikuwa mafundi.
15 Сыновья Халева, сына Иефонниина: Ир, Ила и Наам. Сын Илы: Кеназ.
Kalebu mwana wa Yefune alikuwa na wana watatu: Iru, Ela na Naamu. Naye mwana wa Ela alikuwa: Kenazi.
16 Сыновья Иегаллелела: Зиф, Зифа, Фирия и Асареел.
Wana wa Yahaleleli walikuwa: Zifu, Zifa, Tiria na Asareli.
17 Сыновья Езры: Иефер, Меред, Ефер и Иалон; Иефер же родил Мерома, Шаммая и Ишбаха, отца Ешфемои.
Wana wa Ezra walikuwa: Yetheri, Meredi, Eferi na Yaloni. Mmojawapo wa wake zake Meredi aliwazaa: Miriamu, Shamai na Ishba aliyekuwa baba yake Eshtemoa.
18 И жена его Иудия родила Иереда, отца Гедора, и Хевера, отца Сохо, и Иекуфиила, отца Занаоха. Это сыновья Бифьи, дочери фараоновой, которую взял Меред.
Meredi alikuwa na mke mwingine Myahudi ambaye aliwazaa: Yeredi baba wa Gedori, Heberi baba wa Soko na Yekuthieli baba wa Zanoa. Hawa walikuwa watoto wa Bithia binti Farao, ambaye Meredi alikuwa amemwoa.
19 Сыновья жены его Годии, сестры Нахама, отца Кеилы: Гарми и Ешфемоа - Маахатянин.
Wana wa mke wa Hodia aliyekuwa dada yake Nahamu walikuwa: baba yake Keila, Mgarmi na Eshtemoa, Mmaakathi.
20 Сыновья Симеона: Амнон, Ринна, Бенханан и Филон. Сыновья Ишия: Зохеф и Бензохеф.
Wana wa Shimoni walikuwa: Amnoni, Rina, Ben-Hanani na Tiloni. Wazao wa Ishi walikuwa: Zohethi na Ben-Zohethi.
21 Сыновья Силома, сына Иудина: Ир, отец Лехи, и Лаеда, отец Мареши, и семейства выделывавших виссон, из дома Ашбеи,
Wana wa Shela, mwana wa Yuda, walikuwa: Eri baba yake Leka, Laada baba yake Maresha na jamaa za wafumaji nguo za kitani safi waliokuwa wakiishi huko Beth-Ashbea,
22 и Иоким, и жители Хозевы, и Иоаш и Сараф, которые имели владение в Моаве, и Иашувилехем; но это события древние.
Yokimu, watu walioishi Kozeba, Yoashi na Sarafi waliotawala huko Moabu na Yashubi-Lehemu. (Taarifa hizi ni za zamani sana.)
23 Они были горшечники, и жили при садах и в огородах; у царя для работ его жили они там.
Hawa walikuwa wafinyanzi walioishi Netaimu na Gedera; waliishi huko wakimtumikia mfalme.
24 Сыновья Симеона: Немуил, Иамин, Иарив, Зерах и Саул.
Wazao wa Simeoni walikuwa: Nemueli, Yamini, Yaribu, Zera na Shauli.
25 Шаллум сын его; его сын Мивсам; его сын Мишма.
Mwana wa Shauli alikuwa Shalumu, Shalumu akamzaa Mibsamu, na Mibsamu akamzaa Mishma.
26 Сыновья Мишмы: Хаммуил, сын его; его сын Закур; его сын Шимей.
Wazao wa Mishma walikuwa: Hamueli aliyemzaa Zakuri, Zakuri akamzaa Shimei.
27 У Шимея было шестнадцать сыновей и шесть дочерей; у братьев же его сыновей было немного, и все племя их не так было многочисленно, как племя сынов Иуды.
Shimei alikuwa na wana kumi na sita, na binti sita, lakini ndugu zake hawakuwa na watoto wengi, hivyo ukoo wao wote haukuwa na watu wengi kama ukoo wa Yuda.
28 Они жили в Вирсавии, Моладе, Хацаршуале,
Waliishi Beer-Sheba, Molada, Hasar-Shuali,
29 в Билге, в Ецеме, в Фоладе,
Bilha, Esemu, Toladi,
30 в Вефуиле, в Хорме, в Циклаге,
Bethueli, Horma, Siklagi,
31 в Беф-Маркавофе, в Хацарсусиме, в Беф-Биреи и в Шаариме. Вот города их до царствования Давидова,
Beth-Markabothi, Hasar-Susimu, Beth-Biri na Shaaraimu. Hii ilikuwa miji yao mpaka wakati wa utawala wa Daudi.
32 с селами их: Етам, Аин, Риммон, Фокен и Ашан, - пять городов.
Vijiji vilivyoizunguka vilikuwa Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni na Ashani; jumla miji mitano:
33 И все селения их, которые находились вокруг сих городов до Ваала; вот места жительства их и родословия их.
pamoja na vijiji vyote kuizunguka hii miji hadi huko Baali. Haya yalikuwa makao yao, nao waliweka kumbukumbu ya ukoo wao.
34 Мешовав, Иамлех и Иосия, сын Амассии,
Meshobabu, Yamleki, Yosha mwana wa Amazia,
35 Иоил и Иегу, сын Иошиви, сына Сераии, сына Асиилова,
Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia, mwana wa Seraya, mwana wa Asieli.
36 Елиоенай, Иакова, Ишохаия, Асаия, Адиил, Ишимиил и Ванея,
Pia Elioenai, Yaakoba, Yeshohaya, Asaya, Adieli, Yesimieli, Benaya,
37 и Зиза, сын Шифия, сын Аллона, сын Иедаии, сын Шимрия, сын Шемаии.
Ziza mwana wa Shifi, mwana wa Aloni, mwana wa Yedaya, mwana wa Shimri, mwana wa Shemaya.
38 Сии поименованные были князьями племен своих, и дом отцов их разделился на многие отрасли.
Watu hawa walioorodheshwa hapa juu kwa majina walikuwa viongozi wa koo zao. Jamaa zao ziliongezeka sana,
39 Они доходили до Герары и до восточной стороны долины, чтобы найти пастбища для стад своих;
wakaenea mpaka kwenye viunga vya Gedori kuelekea mashariki mwa bonde wakitafuta malisho kwa ajili ya mifugo yao.
40 и нашли пастбища тучные и хорошие и землю обширную, спокойную и безопасную, потому что до них жило там только немного Хамитян.
Huko walipata malisho mengi mazuri, nayo nchi ilikuwa na nafasi kubwa, yenye amani na utulivu. Baadhi ya Wahamu waliishi huko zamani.
41 И пришли сии, по именам записанные, во дни Езекии, царя Иудейского, и перебили кочующих и оседлых, которые там находились, и истребили их навсегда и поселились на месте их, ибо там были пастбища для стад их.
Watu walioorodheshwa majina walikuja katika nchi hiyo wakati wa Hezekia mfalme wa Yuda. Akawashambulia Wahamu katika makao yao pamoja na Wameuni ambao walikuwako huko nao wakawaangamiza kabisa, kama ilivyo dhahiri hadi leo. Kisha wakafanya makazi yao huko kwa sababu kulikuwa na malisho mazuri kwa ajili ya mifugo yao.
42 Из них же, из сынов Симеоновых, пошли к горе Сеир пятьсот человек: Фелатия, Неария, Рефаия и Узиил, сыновья Ишия, были во главе их;
Watu wa kabila la wa Simeoni wapatao mia tano, wakiongozwa na Pelatia, Nearia, Refaya na Uzieli wana wa Ishi, wakavamia nchi ya vilima ya Seiri.
43 и побили уцелевший там остаток Амаликитян, и живут там до сего дня.
Wakawaua Waamaleki waliobaki, waliokuwa wamenusurika, nao wanaishi huko hadi leo.

< 1-я Паралипоменон 4 >