< II Koryntian 9 >

1 Lecz o posłudze na rzecz świętych nie ma potrzeby, abym wam pisał.
Hakuna haja yangu kuwaandikia kuhusu huduma hii itolewayo kwa ajili ya watakatifu.
2 Znam bowiem waszą gotowość, z powodu której wobec Macedończyków chlubię się wami, że Achaja jest gotowa od zeszłego roku, i wasza gorliwość pobudziła wielu.
Kwa kuwa ninajua mlivyo na shauku ya kusaidia, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili ya jambo hilo kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana na shauku yenu imewachochea wengi wao katika kutoa.
3 Ale posłałem braci, żeby nasza chluba z was nie okazała się pod tym względem próżna, abyście, jak mówiłem, byli przygotowani;
Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusiwe maneno matupu, bali mpate kuwa tayari kama nilivyosema mngekuwa tayari.
4 I abyśmy, jeśli przypadkiem przybyliby ze mną Macedończycy i zastali was nieprzygotowanymi, nie byli zawstydzeni my – żeby nie powiedzieć: wy – za tak śmiałe przechwalanie się.
Kwa maana kama nikija na Mmakedonia yeyote na kuwakuta hamjawa tayari, tutaona aibu kusema chochote juu yenu katika matoleo.
5 Uważałem więc za konieczne zachęcić braci, aby wcześniej udali się do was i zawczasu przygotowali przedtem obiecany wasz hojny dar, aby był gotowy jako [wyraz] hojności, a nie skąpstwa.
Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kwenu kabla yangu, wafanye mipango ya hayo matoleo ya ukarimu mliyokuwa mmeahidi, ili yawe tayari kama matoleo ya hiari wala si kama ya kutozwa kwa nguvu.
6 Lecz [mówię]: Kto skąpo sieje, skąpo też żąć będzie, a kto sieje obficie, obficie też żąć będzie.
Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.
7 Każdy jak postanowił w swym sercu, [tak niech zrobi], nie z żalem ani z przymusu, gdyż radosnego dawcę Bóg miłuje.
Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa uchoyo au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.
8 A Bóg ma moc udzielić wam obficie wszelkiej łaski, abyście, mając zawsze wszystkiego pod dostatkiem, obfitowali we wszelki dobry uczynek;
Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema.
9 Jak jest napisane: Rozrzucił, dał ubogim, jego sprawiedliwość trwa na wieki. (aiōn g165)
Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn g165)
10 A ten, który daje ziarno siewcy, niech i wam da chleba do jedzenia, i wasze ziarno rozmnoży, i zwiększy plon waszej sprawiedliwości;
Yeye ampaye mpanzi mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kuwa chakula, atawapa na kuzizidisha mbegu zenu za kupanda na kuongeza mavuno ya haki yenu.
11 [Abyście] byli wzbogaceni we wszystko ku wszelkiej hojności, która sprawia, że z naszego powodu składane jest dziękczynienie Bogu.
Mtatajirishwa kwa kila namna ili mpate kuwa wakarimu kila wakati, na kupitia kwetu, ukarimu wenu utamletea Mungu shukrani.
12 Posługiwanie bowiem w tej służbie nie tylko zaspokaja niedostatki świętych, ale też obfituje w liczne dziękczynienia składane Bogu.
Huduma hii mnayofanya si tu kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watakatifu, bali huzidi sana kwa shukrani nyingi apewazo Mungu.
13 Gdyż przez doświadczenie tej posługi chwalą Boga za to, że jesteście posłuszni wyznawanej przez siebie ewangelii Chrystusa i hojni w udzielaniu im i wszystkim [innym];
Kwa sababu ya huduma ambayo mmejithibitisha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utiifu ufuatanao na ukiri wenu wa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu wa kushiriki pamoja nao na pia wengine wote.
14 A modląc się za was, tęsknią za wami z powodu obfitującej w was łaski Bożej.
Nao katika maombi yao kwenu mioyo yao itawaonea shauku kwa sababu ya neema ipitayo kiasi mliyopewa na Mungu.
15 Bogu [niech będą] dzięki za jego niewypowiedziany dar.
Ashukuriwe Mungu kwa karama yake isiyoelezeka.

< II Koryntian 9 >