< Galacjan 1 >

1 Paweł, apostoł nie od ludzi ani przez człowieka, ale przez Jezusa Chrystusa i Boga Ojca, który go wskrzesił z martwych;
Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
2 I wszyscy bracia, którzy są ze mną, do kościołów Galacji:
na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
3 Łaska wam i pokój od Boga Ojca i naszego Pana Jezusa Chrystusa;
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
4 Który wydał samego siebie za nasze grzechy, aby nas wyrwać z obecnego złego świata według woli Boga i Ojca naszego; (aiōn g165)
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
5 Któremu chwała na wieki wieków. Amen. (aiōn g165)
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
6 Dziwię się, że tak szybko dajecie się odwieść od tego, który was powołał ku łasce Chrystusa, do innej ewangelii;
Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
7 Która nie jest inną; są tylko pewni [ludzie], którzy was niepokoją i chcą wypaczyć ewangelię Chrystusa.
ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
8 Lecz choćbyśmy nawet my albo anioł z nieba głosił wam ewangelię [inną] od tej, którą wam głosiliśmy, niech będzie przeklęty.
Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
9 Jak powiedzieliśmy przedtem, tak i teraz znowu mówię: Gdyby wam ktoś głosił ewangelię [inną] od tej, którą przyjęliście, niech będzie przeklęty.
Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
10 Czy teraz bowiem chcę pozyskać ludzi, czy Boga? Albo czy staram się przypodobać ludziom? Gdybym nadal ludziom chciał się przypodobać, nie byłbym sługą Chrystusa.
Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
11 A oznajmiam wam, bracia, że głoszona przeze mnie ewangelia nie jest według człowieka.
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
12 Nie otrzymałem jej bowiem ani nie nauczyłem się jej od człowieka, ale przez objawienie Jezusa Chrystusa.
Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
13 Słyszeliście bowiem o moim dawniejszym postępowaniu w judaizmie, że ponad miarę prześladowałem kościół Boży i niszczyłem go;
Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
14 I wyprzedzałem w judaizmie wielu moich rówieśników z mojego narodu, będąc bardzo gorliwym zwolennikiem moich ojczystych tradycji.
Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
15 Lecz gdy upodobało się Bogu, który mnie odłączył w łonie mojej matki i powołał swoją łaską;
Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
16 Aby objawić swego Syna we mnie, abym głosił go wśród pogan, natychmiast, nie radząc się ciała i krwi;
alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
17 Ani nie udając się do Jerozolimy, do tych, którzy przede mną byli apostołami, poszedłem do Arabii, po czym znowu wróciłem do Damaszku.
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
18 Potem, trzy lata później, udałem się do Jerozolimy, aby zobaczyć się z Piotrem, u którego przebywałem piętnaście dni.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
19 A spośród apostołów nie widziałem żadnego innego poza Jakubem, bratem Pana.
Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 [Oświadczam] przed Bogiem, że w tym, co do was piszę, nie kłamię.
Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
21 Potem udałem się w okolice Syrii i Cylicji;
Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
22 A nie byłem osobiście znany kościołom Judei, które są w Chrystusie.
Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
23 Słyszeli tylko: ten, który kiedyś nas prześladował, teraz głosi wiarę, którą przedtem niszczył.
Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
24 I chwalili Boga z mojego powodu.
Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

< Galacjan 1 >