< مکاشفهٔ یوحنا 11 >

و نی‌ای مثل عصا به من داده شد و مراگفت: «برخیز و قدس خدا و مذبح وآنانی را که در آن عبادت می‌کنند پیمایش نما. ۱ 1
Ndipo nikapewa mwanzi uliokuwa kama ufito wa kupimia, nikaambiwa, “Nenda ukapime hekalu la Mungu pamoja na madhabahu, nawe uwahesabu wale waabuduo humo.
وصحن خارج قدس را بیرون انداز و آن را مپیمازیرا که به امت‌ها داده شده است و شهر مقدس راچهل و دو ماه پایمال خواهند نمود. ۲ 2
Lakini usiupime ua wa nje wa Hekalu, uache, kwa sababu ua huo wamepewa watu wa Mataifa. Hao wataukanyagakanyaga mji mtakatifu kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
و به دوشاهد خود خواهم داد که پلاس در بر کرده، مدت هزار و دویست و شصت روز نبوت نمایند.» ۳ 3
Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”
اینانند دو درخت زیتون و دو چراغدان که در حضور خداوند زمین ایستاده‌اند. ۴ 4
Hawa ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili vya taa visimamavyo mbele za Bwana Mungu wa dunia yote.
و اگر کسی بخواهد بدیشان اذیت رساند، آتشی از دهانشان بدر شده، دشمنان ایشان را فرو می‌گیرد؛ و هر‌که قصد اذیت ایشان دارد، بدینگونه باید کشته شود. ۵ 5
Kama mtu yeyote akitaka kuwadhuru, moto hutoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao. Hivi ndivyo impasavyo kufa mtu yeyote atakayetaka kuwadhuru.
اینها قدرت به بستن آسمان دارند تا در ایام نبوت ایشان باران نبارد و قدرت بر آبها دارند که آنها را به خون تبدیل نمایند و جهان را هر گاه بخواهند، به انواع بلایا مبتلا سازند. ۶ 6
Watu hawa wanao uwezo wa kufunga anga ili mvua isinyeshe wakati wote watakapokuwa wanatoa unabii wao. Nao watakuwa na uwezo wa kuyabadili maji kuwa damu na kuipiga dunia kwa kila aina ya mapigo mara kwa mara kama watakavyo.
و چون شهادت خود را به اتمام رسانند، آن وحش که از هاویه برمی آید، با ایشان جنگ کرده، غلبه خواهد یافت و ایشان را خواهد کشت (Abyssos g12) ۷ 7
Basi watakapokuwa wamemaliza ushuhuda wao, yule mnyama atokaye katika lile Shimo atapigana nao vita, atawashinda na kuwaua. (Abyssos g12)
وبدنهای ایشان در شارع عام شهر عظیم که به‌معنی روحانی، به سدوم و مصر مسمی است، جایی که خداوند ایشان نیز مصلوب گشت، خواهد ماند. ۸ 8
Maiti zao zitabaki katika barabara ya mji mkubwa, ambao kwa fumbo unaitwa Sodoma na Misri, ambapo pia Bwana wao alisulubiwa.
و گروهی از اقوام و قبایل و زبانها و امت‌ها، بدنهای ایشان را سه روز و نیم نظاره می‌کنند واجازت نمی دهند که بدنهای ایشان را به قبرسپارند. ۹ 9
Kwa muda wa siku tatu na nusu, watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa wataziangalia hizo maiti zao na hawataruhusu wazikwe.
و ساکنان زمین بر ایشان خوشی وشادی می‌کنند و نزد یکدیگر هدایا خواهندفرستاد، از آنرو که این دو نبی ساکنان زمین رامعذب ساختند. ۱۰ 10
Watu waishio duniani watazitazama kwa furaha maiti za hao manabii wawili na kushangilia kwa kupeana zawadi kwa sababu hao manabii waliwatesa watu waishio duniani.
و بعد از سه روز و نیم، روح حیات از خدابدیشان درآمد که بر پایهای خود ایستادند وبینندگان ایشان را خوفی عظیم فرو گرفت. ۱۱ 11
Lakini baada ya zile siku tatu na nusu, pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu ikawaingia, nao wakasimama kwa miguu yao na wote waliowaona wakaingiwa na hofu kuu.
وآوازی بلند از آسمان شنیدند که بدیشان می‌گوید: «به اینجا صعود نمایید.» پس در ابر، به آسمان بالا شدند و دشمنانشان ایشان را دیدند. ۱۲ 12
Kisha wale manabii wawili wakasikia sauti kuu kutoka mbinguni ikiwaambia, “Njooni huku juu!” Nao wakapaa mbinguni katika wingu, wakati adui zao wakiwa wanawatazama.
و در همان ساعت، زلزله‌ای عظیم حادث گشت که ده‌یک از شهر منهدم گردید و هفت هزارنفر از زلزله هلاک شدند و باقی ماندگان ترسان گشته، خدای آسمان را تمجید کردند. ۱۳ 13
Saa iyo hiyo, kukatokea tetemeko kubwa la nchi na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka. Watu elfu saba wakauawa katika tetemeko hilo, nao walionusurika wakaogopa sana, wakamtukuza Mungu wa mbinguni.
وای دوم درگذشته است. اینک وای سوم بزودی می‌آید. ۱۴ 14
Ole ya pili imekwisha kupita, tazama ole ya tatu inakuja upesi.
و فرشته‌ای بنواخت که ناگاه صداهای بلنددر آسمان واقع شد که می‌گفتند: «سلطنت جهان از آن خداوند ما و مسیح او شد و تا ابدالابادحکمرانی خواهد کرد.» (aiōn g165) ۱۵ 15
Yule malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake, pakawa na sauti kubwa mbinguni iliyosema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala milele na milele.” (aiōn g165)
و آن بیست و چهارپیر که در حضور خدا بر تختهای خود نشسته‌اند، به روی درافتاده، خدا را سجده کردند ۱۶ 16
Nao wale wazee ishirini na wanne, waliokuwa wameketi mbele za Mungu, kwenye viti vyao vya enzi, wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu,
و گفتند: «تو را شکر می‌کنیم‌ای خداوند، خدای قادرمطلق که هستی و بودی، زیرا که قوت عظیم خودرا بدست گرفته، به سلطنت پرداختی. ۱۷ 17
wakisema: “Tunakushukuru, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako, kwa kuwa umetwaa uweza wako mkuu na ukaanza kutawala.
و امت هاخشمناک شدند و غضب تو ظاهر گردید و وقت مردگان رسید تا بر ایشان داوری شود و تا بندگان خود یعنی انبیا و مقدسان و ترسندگان نام خود راچه کوچک و چه بزرگ اجرت دهی و مفسدان زمین را فاسد گردانی.» ۱۸ 18
Mataifa walikasirika nao wakati wa ghadhabu yako umewadia. Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa na kuwapa thawabu watumishi wako manabii na watakatifu wako pamoja na wale wote wanaoliheshimu Jina lako, wakubwa kwa wadogo: na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”
و قدس خدا در آسمان مفتوح گشت وتابوت عهدنامه او در قدس او ظاهر شد و برقها وصداها و رعدها و زلزله و تگرگ عظیمی حادث شد. ۱۹ 19
Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.

< مکاشفهٔ یوحنا 11 >