< مکاشفهٔ یوحنا 10 >

و دیدم فرشته زورآور دیگری را که ازآسمان نازل می‌شود که ابری دربر دارد، و قوس قزحی بر سرش و چهره‌اش مثل آفتاب وپایهایش مثل ستونهای آتش. ۱ 1
Kisha nikamwona malaika mwingine mwenye nguvu akishuka kutoka mbinguni. Alikuwa amevikwa wingu na upinde wa mvua juu ya kichwa chake. Uso wake ulingʼaa kama jua na miguu yake ilikuwa kama nguzo za moto.
و در دست خودکتابچه‌ای گشوده دارد و پای راست خود را بردریا و پای چپ خود را بر زمین نهاد؛ ۲ 2
Mkononi mwake alikuwa ameshika kijitabu kilichokuwa kimefunguliwa. Akauweka mguu wake wa kuume juu ya bahari na mguu wake wa kushoto akauweka juu ya nchi kavu.
و به آوازبلند، چون غرش شیر صدا کرد؛ و چون صدا کرد، هفت رعد به صداهای خود سخن‌گفتند. ۳ 3
Naye akapiga kelele kwa sauti kuu kama simba anayenguruma. Alipopiga kelele, zile radi saba zikatoa ngurumo zake.
و چون هفت رعد سخن‌گفتند، حاضر شدم که بنویسم. آنگاه آوازی از آسمان شنیدم که می‌گوید: «آنچه هفت رعد گفتند مهر کن و آنها را منویس.» ۴ 4
Nazo zile radi saba zilipotoa ngurumo, nilitaka kuanza kuandika, lakini nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Yatie muhuri hayo yaliyosemwa na hizo radi saba na usiyaandike.”
و آن فرشته‌ای را که بر دریا و زمین ایستاده دیدم، دست راست خود را به سوی آسمان بلندکرده، ۵ 5
Kisha yule malaika niliyekuwa nimemwona akiwa amesimama juu ya bahari na juu ya nchi akainua mkono wake wa kuume kuelekea mbinguni.
قسم خورد به او که تا ابدالاباد زنده است که آسمان و آنچه را که در آن است و زمین و آنچه را که در آن است و دریا و آنچه را که در آن است آفرید که «بعد از این زمانی نخواهد بود، (aiōn g165) ۶ 6
Naye akaapa kwa Yule aishiye milele na milele, aliyeumba mbingu na vyote vilivyomo, dunia na vyote viijazavyo, pamoja na bahari na vyote vilivyomo ndani yake, akasema, “Hakuna kungoja tena! (aiōn g165)
بلکه درایام صدای فرشته هفتم، چون کرنا را می‌بایدبنوازد، سر خدا به اتمام خواهد رسید، چنانکه بندگان خود انبیا را بشارت داد.» ۷ 7
Lakini katika siku zile ambazo huyo malaika wa saba atakapokaribia kuipiga hiyo tarumbeta yake, siri ya Mungu itatimizwa, kama vile alivyowatangazia watumishi wake manabii.”
و آن آوازی که از آسمان شنیده بودم، باردیگر شنیدم که مرا خطاب کرده، می‌گوید: «برو وکتابچه گشاده را از دست فرشته‌ای که بر دریا وزمین ایستاده است بگیر.» ۸ 8
Ndipo ile sauti niliyokuwa nimeisikia kutoka mbinguni ikasema nami tena ikaniambia, “Nenda, chukua kile kitabu kilichofunguliwa kilichoko mkononi mwa yule malaika aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi kavu.”
پس به نزد فرشته رفته، به وی گفتم که کتابچه را به من بدهد. او مرا گفت: «بگیر و بخور که اندرونت را تلخ خواهد نمود، لکن در دهانت چون عسل شیرین خواهد بود.» ۹ 9
Basi nikamwendea nikamwomba yule malaika anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, “Chukua na ukile. Kitakuwa kichungu tumboni mwako, lakini kinywani mwako kitakuwa kitamu kama asali.”
پس کتابچه رااز دست فرشته گرفته، خوردم که در دهانم مثل عسل شیرین بود، ولی چون خورده بودم، درونم تلخ گردید. ۱۰ 10
Hivyo nikakichukua kile kitabu kidogo kutoka mkononi mwa yule malaika nikakila. Kilikuwa kitamu kama asali kinywani mwangu, lakini baada ya kukila, tumbo langu likatiwa uchungu.
و مرا گفت که «می‌باید تو اقوام وامت‌ها و زبانها و پادشاهان بسیار را نبوت کنی.» ۱۱ 11
Kisha nikaambiwa, “Imekupasa kutoa unabii tena kuhusu makabila mengi, mataifa, lugha na wafalme.”

< مکاشفهٔ یوحنا 10 >