< فیلپیان 1 >

پولس و تیموتاوس، غلامان عیسی مسیح، به همه مقدسین در مسیح عیسی که درفیلپی می‌باشند با اسقفان و شماسان. ۱ 1
Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
فیض و سلامتی از جانب پدر ما خدا وعیسی مسیح خداوند بر شما باد. ۲ 2
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
در تمامی یادگاری شما خدای خود را شکرمی گذارم، ۳ 3
Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
و پیوسته در هر دعای خود برای جمیع شما به خوشی دعا می‌کنم، ۴ 4
Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
به‌سبب مشارکت شما برای انجیل از روز اول تا به حال. ۵ 5
kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
چونکه به این اعتماد دارم که او که عمل نیکو رادر شما شروع کرد، آن را تا روز عیسی مسیح به‌کمال خواهد رسانید. ۶ 6
Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
چنانکه مرا سزاوار است که درباره همه شما همین فکر کنم زیرا که شما رادر دل خود می‌دارم که در زنجیرهای من و درحجت و اثبات انجیل همه شما با من شریک دراین نعمت هستید. ۷ 7
Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
زیرا خدا مرا شاهد است که چقدر در احشای عیسی مسیح، مشتاق همه شماهستم. ۸ 8
Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
و برای این دعا می‌کنم تا محبت شما درمعرفت و کمال فهم بسیار افزونتر شود. ۹ 9
Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
تاچیزهای بهتر را برگزینید و در روز مسیح بی‌غش و بی‌لغزش باشید، ۱۰ 10
ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
و پر شوید از میوه عدالت که بوسیله عیسی مسیح برای تمجید و حمدخداست. ۱۱ 11
mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
اما‌ای برادران، می‌خواهم شما بدانید که آنچه بر من واقع گشت، برعکس به ترقی انجیل انجامید، ۱۲ 12
Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
بحدی که زنجیرهای من آشکارا شددر مسیح در تمام فوج خاص و به همه دیگران. ۱۳ 13
Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
و اکثر از برادران در خداوند از زنجیرهای من اعتماد به هم رسانیده، بیشتر جرات می‌کنند که کلام خدا را بی‌ترس بگویند. ۱۴ 14
Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
اما بعضی ازحسد و نزاع به مسیح موعظه می‌کنند، ولی بعضی هم از خشنودی. ۱۵ 15
Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
اما آنان از تعصب نه ازاخلاص به مسیح اعلام می‌کنند و گمان می‌برندکه به زنجیرهای من زحمت می‌افزایند. ۱۶ 16
Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
ولی اینان از راه محبت، چونکه می‌دانند که من بجهت حمایت انجیل معین شده‌ام. ۱۷ 17
Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
پس چه؟ جز اینکه به هر صورت، خواه به بهانه و خواه به راستی، به مسیح موعظه می‌شود واز این شادمانم بلکه شادی هم خواهم کرد، ۱۸ 18
Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
زیرا می‌دانم که به نجات من خواهد انجامیدبوسیله دعای شما و تایید روح عیسی مسیح، ۱۹ 19
kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
برحسب انتظار و امید من که در هیچ‌چیزخجالت نخواهم کشید، بلکه در کمال دلیری، چنانکه همیشه، الان نیز مسیح در بدن من جلال خواهد یافت، خواه در حیات و خواه در موت. ۲۰ 20
Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
زیرا که مرا زیستن مسیح است و مردن نفع. ۲۱ 21
Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
و لیکن اگر زیستن در جسم، همان ثمر کار من است، پس نمی دانم کدام را اختیار کنم. ۲۲ 22
Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
زیرادر میان این دو سخت گرفتار هستم، چونکه خواهش دارم که رحلت کنم و با مسیح باشم، زیرااین بسیار بهتر است. ۲۳ 23
Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
لیکن در جسم ماندن برای شما لازمتر است. ۲۴ 24
Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
و چون این اعتماد را دارم، می‌دانم که خواهم ماند و نزد همه شما توقف خواهم نمود بجهت ترقی و خوشی ایمان شما، ۲۵ 25
Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
تا فخر شما در مسیح عیسی در من افزوده شودبوسیله آمدن من بار دیگر نزد شما. ۲۶ 26
Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
باری بطور شایسته انجیل مسیح رفتارنمایید تا خواه آیم و شما را بینم و خواه غایب باشم، احوال شما را بشنوم که به یک روح برقرارید و به یک نفس برای ایمان انجیل مجاهده می‌کنید. ۲۷ 27
Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
و در هیچ امری از دشمنان ترسان نیستید که همین برای ایشان دلیل هلاکت است، اما شما را دلیل نجات و این از خداست. ۲۸ 28
wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
زیراکه به شما عطا شد به‌خاطر مسیح نه فقط ایمان آوردن به او بلکه زحمت کشیدن هم برای او. وشما را همان مجاهده است که در من دیدید و الان هم می‌شنوید که در من است. ۲۹ 29
Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
۳۰ 30
kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.

< فیلپیان 1 >