< افسسیان 1 >

پولس به اراده خدا رسول عیسی مسیح، به مقدسینی که در افسس می‌باشند وایمانداران در مسیح عیسی. ۱ 1
Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu: Kwa watakatifu walioko Efeso, walio waaminifu katika Kristo Yesu:
فیض و سلامتی از جانب پدر ما خدا وعیسی مسیح خداوند بر شما باد. ۲ 2
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
متبارک باد خدا و پدر خداوند ما عیسی مسیح که ما را مبارک ساخت به هر برکت روحانی در جایهای آسمانی در مسیح. ۳ 3
Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki sisi kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho ndani ya Kristo.
چنانکه ما راپیش از بنیاد عالم در او برگزید تا در حضور او درمحبت مقدس و بی‌عیب باشیم. ۴ 4
Kwa maana alituchagua katika yeye kabla ya kuumbwa ulimwengu ili tuwe watakatifu na bila lawama mbele zake. Kwa upendo
که ما را از قبل تعیین نمود تا او را پسر خوانده شویم بوساطت عیسی مسیح برحسب خشنودی اراده خود، ۵ 5
alitangulia kutuchagua tuwe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo kwa furaha yake na mapenzi yake mwenyewe.
برای ستایش جلال فیض خود که ما را به آن مستفیض گردانید در آن حبیب. ۶ 6
Kwa hiyo tunamsifu Mungu kwa huruma zake kuu alizotumiminia sisi katika Mwanawe Mpendwa.
که در وی به‌سبب خون او فدیه یعنی آمرزش گناهان را به اندازه دولت فیض او یافته‌ایم. ۷ 7
Ndani yake tunao ukombozi kwa njia ya damu yake, yaani, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake
که آن را به ما به فراوانی عطا فرمود در حکمت و فطانت. ۸ 8
aliyotumiminia kwa wingi, kwa hekima yote na maarifa yote.
چونکه سر اراده خود را به ما شناسانید، برحسب خشنودی خود که در خود عزم نموده بود، ۹ 9
Naye alitujulisha siri ya mapenzi yake sawasawa na uradhi wa mapenzi yake, ambayo alikusudia katika Kristo,
برای انتظام کمال زمانها تا همه‌چیز را خواه آنچه در آسمان و خواه آنچه بر زمین است، درمسیح جمع کند، یعنی در او. ۱۰ 10
ili yapate kutimizwa wakati mkamilifu utakapowadia, yaani, kuvitia vitu vyote vya mbinguni na vya duniani pamoja, chini ya kiongozi mmoja, ndiye Kristo.
که ما نیز در وی میراث او شده‌ایم، چنانکه پیش معین گشتیم برحسب قصد او. که همه‌چیزها را موافق رای اراده خود می‌کند. ۱۱ 11
Katika Kristo sisi nasi tumepata urithi, tukisha kuchaguliwa sawasawa na kusudi la Mungu, yeye ambaye hufanya mambo yote kulingana na kusudi la mapenzi yake,
تا از ما که اول امیدوار به مسیح می‌بودیم، جلال او ستوده شود. ۱۲ 12
ili kwamba, sisi tuliokuwa wa kwanza kuweka tumaini katika Kristo, tupate kuishi kwa sifa ya utukufu wake.
و دروی شما نیز چون کلام راستی، یعنی بشارت نجات خود را شنیدید، در وی چون ایمان آوردید، از روح قدوس وعده مختوم شدید. ۱۳ 13
Ninyi pia mliingia ndani ya Kristo mliposikia Neno la kweli, Injili ya wokovu wenu. Mkiisha kuamini, ndani yake mlitiwa muhuri, yaani, Roho Mtakatifu mliyeahidiwa,
که بیعانه میراث ما است برای فدای آن ملک خاص او تا جلال او ستوده شود. ۱۴ 14
yeye ambaye ni amana yetu akituhakikishia urithi wetu hadi ukombozi wa wale walio milki ya Mungu kwa sifa ya utukufu wake.
بنابراین، من نیز چون خبر ایمان شما را درعیسی خداوند ومحبت شما را با همه مقدسین شنیدم، ۱۵ 15
Kwa sababu hii, tangu niliposikia juu ya imani yenu katika Bwana Yesu na upendo wenu kwa watakatifu wote,
باز نمی ایستم از شکر نمودن برای شما و از یاد آوردن شما در دعاهای خود، ۱۶ 16
sijaacha kumshukuru Mungu kwa ajili yenu, nikiwakumbuka katika maombi yangu.
تاخدای خداوند ما عیسی مسیح که پدر ذوالجلال است، روح حکمت و کشف را در معرفت خود به شما عطا فرماید. ۱۷ 17
Nazidi kumwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awajalieni ninyi roho ya hekima na ya ufunuo, ili mpate kumjua zaidi.
تا چشمان دل شما روشن گشته، بدانید که امید دعوت او چیست و کدام است دولت جلال میراث او در مقدسین، ۱۸ 18
Ninaomba pia kwamba macho ya mioyo yenu yatiwe nuru ili mpate kujua tumaini mliloitiwa, utajiri wa urithi wa utukufu wake kwa watakatifu
و چه مقدار است عظمت بینهایت قوت او نسبت به مامومنین برحسب عمل توانایی قوت او ۱۹ 19
na uweza wake mkuu usiolinganishwa kwa ajili yetu sisi tuaminio. Uweza huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na ile nguvu kuu mno
که درمسیح عمل کرد چون او را از مردگان برخیزانید وبه‌دست راست خود در جایهای آسمانی نشانید، ۲۰ 20
aliyoitumia katika Kristo alipomfufua kutoka kwa wafu, na akamketisha mkono wake wa kuume huko mbinguni,
بالاتر از هر ریاست و قدرت و قوت و سلطنت و هر نامی که خوانده می‌شود، نه در این عالم فقطبلکه در عالم آینده نیز. (aiōn g165) ۲۱ 21
juu sana kuliko falme zote na mamlaka, enzi na milki, na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu, bali katika ule ujao pia. (aiōn g165)
و همه‌چیز را زیر پایهای او نهاد و او را سرهمه‌چیز به کلیسا داد، ۲۲ 22
Naye Mungu ameweka vitu vyote viwe chini ya miguu yake na amemfanya yeye awe kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya Kanisa,
که بدن اوست یعنی پری او که همه را در همه پر می‌سازد. ۲۳ 23
ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake yeye aliye yote katika yote.

< افسسیان 1 >