< لوقا 3 >

و در سال پانزدهم از سلطنت طیباریوس قیصر، در وقتی که پنطیوس پیلاطس، والی یهودیه بود و هیرودیس، تیترارک جلیل وبرادرش فیلپس تیترارک ایطوریه تراخونیتس ولیسانیوس تیترارک آبلیه ۱ 1
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
و حنا و قیافا روسای کهنه بودند، کلام خدا به یحیی ابن زکریا در بیابان نازل شده، ۲ 2
nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
به تمامی حوالی اردن آمده، به تعمیدتوبه بجهت آمرزش گناهان موعظه می‌کرد. ۳ 3
Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
چنانچه مکتوب است در صحیفه کلمات اشعیای نبی که می‌گوید: «صدای ندا کننده‌ای دربیابان که راه خداوند را مهیا سازید و طرق او راراست نمایید. ۴ 4
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
هر وادی انباشته و هر کوه و تلی پست و هر کجی راست و هر راه ناهموار صاف خواهد شد ۵ 5
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
و تمامی بشر نجات خدا را خواهنددید.» ۶ 6
Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
آنگاه به آن جماعتی که برای تعمید وی بیرون می‌آمدند، گفت: «ای افعی‌زادگان، که شمارا نشان داد که از غضب آینده بگریزید؟ ۷ 7
Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
پس ثمرات مناسب توبه بیاورید و در خاطر خود این سخن را راه مدهید که ابراهیم پدر ماست، زیرا به شما می‌گویم خدا قادر است که از این سنگها، فرزندان برای ابراهیم برانگیزاند. ۸ 8
Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
و الان نیز تیشه بر ریشه درختان نهاده شده است، پس هر درختی که میوه نیکو نیاورد، بریده و در آتش افکنده می‌شود.» ۹ 9
Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
پس مردم از وی سوال نموده گفتند: «چه کنیم؟» ۱۰ 10
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
او در جواب ایشان گفت: «هر‌که دوجامه دارد، به آنکه ندارد بدهد. و هرکه خوراک دارد نیز چنین کند.» ۱۱ 11
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
و باجگیران نیز برای تعمید آمده، بدو گفتند: «ای استاد چه کنیم؟» ۱۲ 12
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
بدیشان گفت: «زیادتر از آنچه مقرر است، مگیرید.» ۱۳ 13
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
سپاهیان نیز از او پرسیده، گفتند: «ماچه کنیم؟» به ایشان گفت: «بر کسی ظلم مکنید وبر هیچ‌کس افترا مزنید و به مواجب خود اکتفاکنید.» ۱۴ 14
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
و هنگامی که قوم مترصد می‌بودند و همه در خاطر خود درباره یحیی تفکر می‌نمودندکه این مسیح است یا نه، ۱۵ 15
Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
یحیی به همه متوجه شده گفت: «من شما را به آب تعمیدمی دهم، لیکن شخصی تواناتر از من می‌آید که لیاقت آن ندارم که بند نعلین او را باز کنم. اوشما را به روح‌القدس و آتش تعمید خواهد داد. ۱۶ 16
Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
او غربال خود را به‌دست خود دارد وخرمن خویش را پاک کرده، گندم را در انبارخود ذخیره خواهد نمود و کاه را در آتشی که خاموشی نمی پذیرد خواهد سوزانید.» ۱۷ 17
Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
وبه نصایح بسیار دیگر، قوم را بشارت می‌داد. ۱۸ 18
Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
اما هیرودیس تیترارک چون به‌سبب هیرودیا، زن برادر او فیلپس و سایر بدیهایی که هیرودیس کرده بود از وی توبیخ یافت، ۱۹ 19
Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
این رانیز بر همه افزود که یحیی را در زندان حبس نمود. ۲۰ 20
Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
اما چون تمامی قوم تعمید یافته بودند وعیسی هم تعمید گرفته دعا می‌کرد، آسمان شکافته شد ۲۱ 21
Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
و روح‌القدس به هیات جسمانی، مانند کبوتری بر او نازل شد. و آوازی از آسمان در‌رسید که تو پسر حبیب من هستی که به توخشنودم. ۲۲ 22
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
و خود عیسی وقتی که شروع کرد، قریب به سی ساله بود. و حسب گمان خلق، پسر یوسف ابن هالی ۲۳ 23
Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
ابن متات، بن لاوی، بن ملکی، بن ینا، بن یوسف، ۲۴ 24
Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
ابن متاتیا، بن آموس، بن ناحوم، بن حسلی، بن نجی، ۲۵ 25
Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
ابن مات، بن متاتیا، بن شمعی، بن یوسف، بن یهودا، ۲۶ 26
Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
ابن یوحنا، بن ریسا، بن زروبابل، بن سالتیئیل، بن نیری، ۲۷ 27
Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
ابن ملکی، بن ادی، بن قوسام، بن ایلمودام، بن عیر، ۲۸ 28
Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
ابن یوسی، بن ایلعاذر، بن یوریم، بن متات، بن لاوی، ۲۹ 29
Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
ابن شمعون، بن یهودا، بن یوسف، بن یونان، بن ایلیاقیم، ۳۰ 30
Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
ابن ملیا، بن مینان، بن متاتا بن ناتان، بن داود، ۳۱ 31
Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
ابن یسی، بن عوبید، بن بوعز، بن شلمون، بن نحشون، ۳۲ 32
Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
ابن عمیناداب، بن ارام، بن حصرون، بن فارص، بن یهودا، ۳۳ 33
Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
ابن یعقوب، بن اسحق، بن ابراهیم، بن تارح، بن ناحور، ۳۴ 34
Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
ابن سروج، بن رعور، بن فالج، بن عابر، بن صالح، ۳۵ 35
Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
ابن قینان، بن ارفکشاد، بن سام، بن نوح، بن لامک، ۳۶ 36
Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
ابن متوشالح، بن خنوخ، بن یارد، بن مهللئیل، بن قینان، ۳۷ 37
Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
ابن انوش، بن شیث، بن آدم، بن الله. ۳۸ 38
Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

< لوقا 3 >