< لوقا 2 >

و در آن ایام حکمی از اوغسطس قیصرصادر گشت که تمام ربع مسکون را اسم نویسی کنند. ۱ 1
Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
و این اسم نویسی اول شد، هنگامی که کیرینیوس والی سوریه بود. ۲ 2
(Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
پس همه مردم هر یک به شهر خود برای اسم نویسی می‌رفتند. ۳ 3
Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
و یوسف نیز از جلیل از بلده ناصره به یهودیه به شهر داود که بیت لحم نام داشت، رفت. زیرا که او از خاندان و آل داود بود. ۴ 4
Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
تا نام او بامریم که نامزد او بود و نزدیک به زاییدن بود، ثبت گردد. ۵ 5
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
و وقتی که ایشان در آنجا بودند، هنگام وضع حمل او رسیده، ۶ 6
Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
پسر نخستین خود رازایید. و او را در قنداقه پیچیده، در آخورخوابانید. زیرا که برای ایشان در منزل جای نبود. ۷ 7
naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
و در آن نواحی، شبانان در صحرا بسرمی بردند و در شب پاسبانی گله های خویش می‌کردند. ۸ 8
Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
ناگاه فرشته خداوند بر ایشان ظاهرشد و کبریایی خداوند بر گرد ایشان تابید و بغایت ترسان گشتند. ۹ 9
Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
فرشته ایشان را گفت: «مترسید، زیرا اینک بشارت خوشی عظیم به شما می‌دهم که برای جمیع قوم خواهد بود. ۱۰ 10
Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
که امروز برای شما در شهر داود، نجات‌دهنده‌ای که مسیح خداوند باشد متولد شد. ۱۱ 11
Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
و علامت برای شمااین است که طفلی در قنداقه پیچیده و در آخورخوابیده خواهید یافت.» ۱۲ 12
Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
در همان حال فوجی از لشکر آسمانی با فرشته حاضر شده، خدا راتسبیح‌کنان می‌گفتند: ۱۳ 13
Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
«خدا را در اعلی علیین جلال و بر زمین سلامتی و در میان مردم رضامندی باد.» ۱۴ 14
“Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
و چون فرشتگان از نزد ایشان به آسمان رفتند، شبانان با یکدیگر گفتند: «الان به بیت لحم برویم و این چیزی را که واقع شده و خداوند آن را به ما اعلام نموده است ببینیم.» ۱۵ 15
Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
پس به شتاب رفته، مریم و یوسف و آن طفل رادر آخور خوابیده یافتند. ۱۶ 16
Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
چون این را دیدند، آن سخنی را که درباره طفل بدیشان گفته شده بود، شهرت دادند. ۱۷ 17
Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
و هر‌که می‌شنید از آنچه شبانان بدیشان گفتند، تعجب می‌نمود. ۱۸ 18
Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
امامریم در دل خود متفکر شده، این همه سخنان رانگاه می‌داشت. ۱۹ 19
Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
و شبانان خدا را تمجید وحمدکنان برگشتند، به‌سبب همه آن اموری که دیده و شنیده بودند چنانکه به ایشان گفته شده بود. ۲۰ 20
Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
و چون روز هشتم، وقت ختنه طفل رسید، او را عیسی نام نهادند، چنانکه فرشته قبل از قرارگرفتن او در رحم، او را نامیده بود. ۲۱ 21
Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
و چون ایام تطهیر ایشان برحسب شریعت موسی رسید، او رابه اورشلیم بردند تا به خداوند بگذرانند. ۲۲ 22
Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
چنانکه در شریعت خداوند مکتوب است که هر ذکوری که رحم را گشاید، مقدس خداوندخوانده شود. ۲۳ 23
(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
و تا قربانی گذرانند، چنانکه درشریعت خداوند مقرر است، یعنی جفت فاخته‌ای یا دو جوجه کبوتر. ۲۴ 24
na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
و اینک شخصی شمعون نام در اورشلیم بود که مرد صالح و متقی و منتظر تسلی اسرائیل بود و روح‌القدس بر وی بود. ۲۵ 25
Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
و از روح‌القدس بدو وحی رسیده بود که، تا مسیح خداوند را نبینی موت را نخواهی دید. ۲۶ 26
Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
پس به راهنمایی روح، به هیکل درآمد وچون والدینش آن طفل یعنی عیسی را آوردند تا رسوم شریعت را بجهت او بعمل آورند، ۲۷ 27
Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
او رادر آغوش خود کشیده و خدا را متبارک خوانده، گفت: ۲۸ 28
ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
«الحال‌ای خداوند بنده خود را رخصت می‌دهی، به سلامتی برحسب کلام خود. ۲۹ 29
“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
زیراکه چشمان من نجات تو را دیده است، ۳۰ 30
Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
که آن راپیش روی جمیع امت‌ها مهیا ساختی. ۳۱ 31
ulioweka tayari machoni pa watu wote,
نوری که کشف حجاب برای امت‌ها کند و قوم تواسرائیل را جلال بود.» ۳۲ 32
nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
و یوسف و مادرش ازآنچه درباره او گفته شد، تعجب نمودند. ۳۳ 33
Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
پس شمعون ایشان را برکت داده، به مادرش مریم گفت: «اینک این طفل قرار داده شد، برای افتادن وبرخاستن بسیاری از آل اسرائیل و برای آیتی که به خلاف آن خواهند گفت. ۳۴ 34
Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
و در قلب تو نیزشمشیری فرو خواهد رفت، تا افکار قلوب بسیاری مکشوف شود.» ۳۵ 35
ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
و زنی نبیه بود، حنا نام، دختر فنوئیل ازسبط اشیر بسیار سالخورده، که از زمان بکارت هفت سال با شوهر بسر برده بود. ۳۶ 36
Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
و قریب به هشتاد و چهار سال بود که او بیوه گشته ازهیکل جدا نمی شد، بلکه شبانه‌روز به روزه ومناجات در عبادت مشغول می‌بود. ۳۷ 37
Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
او درهمان ساعت در‌آمده، خدا را شکر نمود ودرباره او به همه منتظرین نجات در اورشلیم، تکلم نمود. ۳۸ 38
Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
و چون تمامی رسوم شریعت خداوند را به پایان برده بودند، به شهر خود ناصره جلیل مراجعت کردند. ۳۹ 39
Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
و طفل نمو کرده، به روح قوی می‌گشت و از حکمت پر شده، فیض خدا بروی می‌بود. ۴۰ 40
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
و والدین او هر ساله بجهت عید فصح، به اورشلیم می‌رفتند. ۴۱ 41
Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
و چون دوازده ساله شد، موافق رسم عید، به اورشلیم آمدند. ۴۲ 42
Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
وچون روزها را تمام کرده مراجعت می‌نمودند، آن طفل یعنی عیسی، در اورشلیم توقف نمودو یوسف و مادرش نمی دانستند. ۴۳ 43
Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
بلکه چون گمان می‌بردند که او در قافله است، سفریکروزه کردند و او را در میان خویشان وآشنایان خود می‌جستند. ۴۴ 44
Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
و چون او را نیافتند، در طلب او به اورشلیم برگشتند. ۴۵ 45
Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
و بعد ازسه روز، او را در هیکل یافتند که در میان معلمان نشسته، سخنان ایشان را می‌شنود و ازایشان سوال همی کرد. ۴۶ 46
Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
و هر‌که سخن او رامی شنید، از فهم و جوابهای او متحیرمی گشت. ۴۷ 47
Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
چون ایشان او را دیدند، مضطرب شدند. پس مادرش به وی گفت: «ای فرزند چرا با ماچنین کردی؟ اینک پدرت و من غمناک گشته تو را جستجو می‌کردیم.» ۴۸ 48
Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
او به ایشان گفت: «از بهر‌چه مرا طلب می‌کردید، مگرندانسته‌اید که باید من در امور پدر خود باشم؟» ۴۹ 49
Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
ولی آن سخنی را که بدیشان گفت، نفهمیدند. ۵۰ 50
Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
پس با ایشان روانه شده، به ناصره آمد و مطیع ایشان می‌بود و مادر او تمامی این امور را درخاطر خود نگاه می‌داشت. ۵۱ 51
Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
و عیسی درحکمت و قامت و رضامندی نزد خدا و مردم ترقی می‌کرد. ۵۲ 52
Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

< لوقا 2 >