< لاویان 18 >

و خداوند موسی را خطاب کرده، گفت: ۱ 1
Bwana akamwambia Mose,
«بنی‌اسرائیل را خطاب کرده، به ایشان بگو: من یهوه خدای شما هستم. ۲ 2
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
مثل اعمال زمین مصر که در آن ساکن می‌بودید عمل منمایید، و مثل اعمال زمین کنعان که من شما را به آنجا داخل خواهم کرد عمل منمایید، و برحسب فرایض ایشان رفتار مکنید. ۳ 3
Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao.
احکام مرا بجاآورید و فرایض مرا نگاه دارید تا در آنها رفتارنمایید، من یهوه خدای شما هستم. ۴ 4
Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
پس فرایض و احکام مرا نگاه دارید، که هر آدمی که آنها را بجاآورد در آنها زیست خواهد کرد، من یهوه هستم. ۵ 5
Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.
هیچ‌کس به احدی از اقربای خویش نزدیکی ننماید تا کشف عورت او بکند. من یهوه هستم. ۶ 6
“‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.
عورت پدر خود یعنی مادر خود را کشف منما؛ او مادر توست. کشف عورت او مکن. ۷ 7
“‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
عورت زن پدر خود را کشف مکن. آن عورت پدر تو است. ۸ 8
“‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.
عورت خواهر خود، خواه دختر پدرت، خواه دختر مادرت چه مولود در خانه، چه مولودبیرون، عورت ایشان را کشف منما. ۹ 9
“‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
عورت دختر پسرت و دختر دخترت، عورت ایشان را کشف مکن، زیرا که اینها عورت تو است. ۱۰ 10
“‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.
عورت دختر زن پدرت که از پدر تو زاییده شده باشد، او خواهر تو است کشف عورت او رامکن. ۱۱ 11
“‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.
عورت خواهر پدر خود را کشف مکن، او از اقربای پدر تو است. ۱۲ 12
“‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.
عورت خواهرمادر خود را کشف مکن، او از اقربای مادر تواست. ۱۳ 13
“‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
عورت برادر پدر خود را کشف مکن، وبه زن او نزدیکی منما. او (به منزله ) عمه تو است. ۱۴ 14
“‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.
عورت عروس خود را کشف مکن، او زن پسرتو است. عورت او را کشف مکن. ۱۵ 15
“‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
عورت زن برادر خود را کشف مکن. آن عورت برادر تواست. ۱۶ 16
“‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.
عورت زنی را با دخترش کشف مکن. ودختر پسر او یا دختر دختر او را مگیر، تا عورت او را کشف کنی. اینان از اقربای او می‌باشند و این فجور است. ۱۷ 17
“‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.
و زنی را با خواهرش مگیر، تاهیوی او بشود، و تا عورت او را با وی مادامی که او زنده است، کشف نمایی. ۱۸ 18
“‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
و به زنی درنجاست حیضش نزدیکی منما، تا عورت او راکشف کنی. ۱۹ 19
“‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.
و با زن همسایه خود همبسترمشو، تا خود را با وی نجس سازی. ۲۰ 20
“‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.
و کسی ازذریت خود را برای مولک از آتش مگذران و نام خدای خود را بی‌حرمت مساز. من یهوه هستم. ۲۱ 21
“‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.
و با ذکور مثل زن جماع مکن، زیرا که این فجور است. ۲۲ 22
“‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.
و با هیچ بهیمه‌ای جماع مکن، تاخود را به آن نجس سازی، و زنی پیش بهیمه‌ای نایستد تا با آن جماع کند، زیرا که این فجوراست. ۲۳ 23
“‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.
«به هیچ کدام از اینها خویشتن را نجس مسازید، زیرا به همه اینها امتهایی که من پیش روی شما بیرون می‌کنم، نجس شده‌اند. ۲۴ 24
“‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi.
وزمین نجس شده است، و انتقام گناهش را از آن خواهم کشید، و زمین ساکنان خود را قی خواهدنمود. ۲۵ 25
Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake.
پس شما فرایض و احکام مرا نگاه دارید، و هیچ کدام از این فجور را به عمل نیاورید، نه متوطن و نه غریبی که در میان شما ماواگزیند. ۲۶ 26
Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya,
زیرا مردمان آن زمین که قبل از شمابودند، جمیع این فجور را کردند، و زمین نجس شده است. ۲۷ 27
kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi.
مبادا زمین شما را نیز قی کند، اگرآن را نجس سازید، چنانکه امتهایی را که قبل ازشما بودند، قی کرده است. ۲۸ 28
Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.
زیرا هر کسی‌که یکی از این فجور را بکند، همه کسانی که کرده باشند، از میان قوم خود منقطع خواهند شد. ۲۹ 29
“‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
پس وصیت مرا نگاه دارید، و از این رسوم زشت که قبل از شما به عمل آورده شده است عمل منمایید، و خود را به آنها نجس مسازید. من یهوه خدای شما هستم.» ۳۰ 30
Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’”

< لاویان 18 >