< یعقوب 1 >

یعقوب که غلام خدا و عیسی مسیح خداوند است، به دوازده سبط که پراکنده هستند. خوش باشید. ۱ 1
Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo: Kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika ulimwenguni: Salamu.
‌ای برادران من، وقتی که در تجربه های گوناگون مبتلا شوید، کمال خوشی دانید. ۲ 2
Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
چونکه می‌دانید که امتحان ایمان شما صبر راپیدا می‌کند. ۳ 3
kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
لکن صبر را عمل تام خود باشد تاکامل و تمام شوید و محتاج هیچ‌چیز نباشید. ۴ 4
Saburi na iwe na kazi timilifu, ili mpate kuwa wakamilifu, mmekamilishwa, bila kupungukiwa na kitu chochote.
واگر از شما کسی محتاج به حکمت باشد، سوال بکند از خدایی که هر کس را به سخاوت عطامی کند و ملامت نمی نماید و به او داده خواهدشد. ۵ 5
Kama mtu yeyote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima na amwombe Mungu, yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa.
لکن به ایمان سوال بکند و هرگز شک نکندزیرا هرکه شک کند، مانند موج دریاست که از بادرانده و متلاطم می‌شود. ۶ 6
Lakini anapoomba, lazima aamini wala asiwe na shaka, kwa sababu mtu aliye na shaka ni kama wimbi la bahari, lililochukuliwa na upepo na kutupwa huku na huku.
زیرا چنین شخص گمان نبرد که از خداوند چیزی خواهد یافت. ۷ 7
Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapata kitu chochote kutoka kwa Bwana.
مرد دودل در تمام رفتار خود ناپایدار است. ۸ 8
Yeye ni mtu mwenye nia mbili, mwenye kusitasita katika njia zake zote.
لکن برادر مسکین به‌سرافرازی خود فخربنماید، ۹ 9
Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa.
و دولتمند از مسکنت خود، زیرا مثل گل علف در گذر است. ۱۰ 10
Lakini yeye aliye tajiri afurahi kwa kuwa ameshushwa, kwa sababu atatoweka kama ua la shambani.
از آنرو که آفتاب باگرمی طلوع کرده، علف را خشکانید و گلش به زیر افتاده، حسن صورتش زایل شد. به همینطورشخص دولتمند نیز در راههای خود، پژمرده خواهد گردید. ۱۱ 11
Kwa maana jua kali lenye kuchoma huchomoza na kuliunguza, likayakausha majani, na ua lake likapukutika, nao uzuri wake huharibika. Vivyo hivyo tajiri naye atanyauka akiwa anaendelea na shughuli zake.
خوشابحال کسی‌که متحمل تجربه شود، زیرا که چون آزموده شد، آن تاج حیاتی را که خداوند به محبان خود وعده فرموده است خواهد یافت. ۱۲ 12
Heri mtu anayevumilia wakati wa majaribu, kwa sababu akiisha kushinda hilo jaribio atapewa taji la uzima Mungu alilowaahidia wale wampendao.
هیچ‌کس چون در تجربه افتد، نگوید: «خدا مرا تجربه می‌کند»، زیرا خدا هرگزاز بدیها تجربه نمی شود و او هیچ‌کس را تجربه نمی کند. ۱۳ 13
Mtu anapojaribiwa asiseme, “Ninajaribiwa na Mungu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu wala yeye hamjaribu mtu yeyote.
لکن هرکس در تجربه می‌افتد وقتی که شهوت وی او را می‌کشد و فریفته می‌سازد. ۱۴ 14
Lakini kila mtu hujaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa zake mwenyewe zilizo mbaya.
پس شهوت آبستن شده، گناه را می‌زاید و گناه به انجام رسیده، موت را تولید می‌کند. ۱۵ 15
Basi ile tamaa mbaya ikishachukua mimba, huzaa dhambi, nayo ile dhambi ikikomaa, huzaa mauti.
‌ای برادران عزیز من، گمراه مشوید! ۱۶ 16
Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike.
هر بخشندگی نیکو و هر بخشش کامل از بالا است و نازل می‌شود از پدر نورها که نزد او هیچ تبدیل و سایه گردش نیست. ۱۷ 17
Kila kitolewacho kilicho chema na kilicho kamili, hutoka juu, na hushuka kutoka kwa Baba wa mianga, ambaye kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka.
او محض اراده خود ما رابوسیله کلمه حق تولید نمود تا ما چون نوبرمخلوقات او باشیم. ۱۸ 18
Kwa mapenzi yake mwenyewe alituzaa kwa neno la kweli, kusudi tuwe kama mazao ya kwanza katika viumbe vyake vyote.
بنابراین، ای برادران عزیز من، هرکس درشنیدن تند و در گفتن آهسته و در خشم سست باشد. ۱۹ 19
Ndugu zangu wapendwa, fahamuni jambo hili: Kila mtu awe mwepesi wa kusikiliza, lakini asiwe mwepesi wa kusema wala wa kukasirika.
زیرا خشم انسان عدالت خدا را به عمل نمی آورد. ۲۰ 20
Kwa maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu.
پس هر نجاست و افزونی شر را دورکنید و با فروتنی، کلام کاشته شده را بپذیرید که قادر است که جانهای شما را نجات‌بخشد. ۲۱ 21
Kwa hiyo, ondoleeni mbali uchafu wote na uovu ambao umezidi kuwa mwingi, mkalipokee kwa unyenyekevu lile Neno lililopandwa ndani yenu ambalo laweza kuokoa nafsi zenu.
لکن کنندگان کلام باشید نه فقط شنوندگان که خود را فریب می‌دهند. ۲۲ 22
Basi kuweni watendaji wa Neno wala msiwe wasikiaji tu, huku mkijidanganya nafsi zenu.
زیرا اگر کسی کلام را بشنود و عمل نکند، شخصی را ماند که صورت طبیعی خود را در آینه می‌نگرد. ۲۳ 23
Kwa maana kama mtu ni msikiaji tu wa Neno wala hatendi kile linachosema, yeye ni kama mtu ajitazamaye uso wake kwenye kioo
زیرا خود رانگریست و رفت و فور فراموش کرد که چطورشخصی بود. ۲۴ 24
na baada ya kujiona alivyo, huenda zake na mara husahau jinsi alivyo.
لکن کسی‌که بر شریعت کامل آزادی چشم دوخت و در آن ثابت ماند، او چون شنونده فراموشکار نمی باشد، بلکه کننده عمل پس او در عمل خود مبارک خواهد بود. ۲۵ 25
Lakini yeye anayeangalia kwa bidii katika sheria kamilifu, ile iletayo uhuru, naye akaendelea kufanya hivyo bila kusahau alichosikia, bali akalitenda, atabarikiwa katika kile anachofanya.
اگرکسی از شما گمان برد که پرستنده خدا است وعنان زبان خود را نکشد بلکه دل خود را فریب دهد، پرستش او باطل است. ۲۶ 26
Kama mtu akidhani ya kuwa anayo dini lakini hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hujidanganya moyoni mwake, wala dini yake mtu huyo haifai kitu.
پرستش صاف وبی عیب نزد خدا و پدر این است که یتیمان وبیوه‌زنان را در مصیبت ایشان تفقد کنند و خود رااز آلایش دنیا نگاه دارند. ۲۷ 27
Dini iliyo safi, isiyo na uchafu, inayokubalika mbele za Mungu Baba yetu, ndiyo hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao na kujilinda usitiwe madoa na dunia.

< یعقوب 1 >