< عبرانیان 8 >

پس مقصود عمده از این کلام این است که برای ما چنین رئیس کهنه‌ای هست که درآسمانها به‌دست راست تخت کبریا نشسته است، ۱ 1
Basi jambo tunalotaka kulisema ni hili: Tunaye Kuhani Mkuu ambaye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Aliye Mkuu mbinguni,
که خادم مکان اقدس و آن خیمه حقیقی است که خداوند آن را برپا نمود نه انسان. ۲ 2
yeye ahudumuye katika patakatifu, hema la kweli lililowekwa na Bwana, wala si na mwanadamu.
زیرا که هررئیس کهنه مقرر می‌شود تا هدایا و قربانی هابگذراند؛ و از این جهت واجب است که او را نیزچیزی باشد که بگذراند. ۳ 3
Kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe sadaka na dhabihu. Vivyo hivyo, ilikuwa jambo muhimu kwa huyu Kuhani naye awe na kitu cha kutoa.
پس اگر بر زمین می بود، کاهن نمی بود چون کسانی هستند که به قانون شریعت هدایا را می‌گذرانند. ۴ 4
Kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani, kwa sababu tayari wapo watu watoao sadaka kama ilivyoelekezwa na sheria.
و ایشان شبیه و سایه چیزهای آسمانی را خدمت می‌کنند، چنانکه موسی ملهم شد هنگامی که عازم بود که خیمه را بسازد، زیرا بدو می‌گوید: «آگاه باش که همه‌چیز را به آن نمونه‌ای که در کوه به تو نشان داده شد بسازی.» ۵ 5
Wanahudumu katika patakatifu palipo mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni. Hii ndiyo sababu Mose alionywa alipokaribia kujenga hema, akiambiwa: “Hakikisha kuwa unavitengeneza vitu vyote kwa mfano ulioonyeshwa kule mlimani.”
لکن الان او خدمت نیکوتر یافته است، به مقداری که متوسط عهدنیکوتر نیز هست که بر وعده های نیکوتر مرتب است. ۶ 6
Lakini huduma aliyopewa Yesu ni bora zaidi kuliko yao, kama vile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani, nalo limewekwa misingi wa ahadi zilizo bora zaidi.
زیرا اگر آن اول بی‌عیب می‌بود، جایی برای دیگری طلب نمی شد. ۷ 7
Kwa maana kama hapakuwa na kasoro katika lile agano la kwanza, pasingekuwa na haja ya kutafuta nafasi kwa ajili ya jingine.
چنانکه ایشان را ملامت کرده، می‌گوید: «خداوند می‌گوید اینک ایامی می‌آید که با خاندان اسرائیل و خاندان یهوداعهدی تازه استوار خواهم نمود. ۸ 8
Lakini Mungu aliona kosa kwa watu, naye akasema: “Siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.
نه مثل آن عهدی که با پدران ایشان بستم، در روزی که من ایشان را دستگیری نمودم تا از زمین مصربرآوردم، زیرا که ایشان در عهد من ثابت نماندند. پس خداوند می‌گوید من ایشان را واگذاردم. ۹ 9
Agano langu halitakuwa kama lile nililofanya na baba zao nilipowashika mkono kuwaongoza watoke nchi ya Misri, kwa sababu hawakuendelea kuwa waaminifu katika agano langu, nami nikawaacha, asema Bwana.
وخداوند می‌گوید این است آن عهدی که بعد از آن ایام با خاندان اسرائیل استوار خواهم داشت که احکام خود را در خاطر ایشان خواهم نهاد و بردل ایشان مرقوم خواهم داشت و ایشان را خداخواهم بود و ایشان مرا قوم خواهند بود. ۱۰ 10
Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku zile, asema Bwana. Nitaziweka sheria zangu katika nia zao na kuziandika mioyoni mwao. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
ودیگر کسی همسایه و برادر خود را تعلیم نخواهدداد و نخواهد گفت خداوند را بشناس زیرا که همه از خرد و بزرگ مرا خواهند شناخت. ۱۱ 11
Mtu hatamfundisha tena jirani yake, wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’ kwa sababu wote watanijua mimi, tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.
زیرابر تقصیرهای ایشان ترحم خواهم فرمود وگناهانشان را دیگر به یاد نخواهم آورد.» ۱۲ 12
Kwa sababu nitasamehe uovu wao, wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”
پس چون «تازه» گفت، اول را کهنه ساخت؛ و آنچه کهنه و پیر شده است، مشرف بر زوال است. ۱۳ 13
Kwa kuliita agano hili “jipya,” Mungu amefanya lile agano la kwanza kuwa kuukuu; nacho kitu kinachoanza kuchakaa na kuwa kikuukuu kiko karibu kutoweka.

< عبرانیان 8 >