< عبرانیان 2 >

لهذا لازم است که به دقت بلیغ تر آنچه راشنیدیم گوش دهیم، مبادا که از آن ربوده شویم. ۱ 1
Kwa hiyo, imetupasa kuwa waangalifu sana kuhusu kile tulichosikia, ili tusije tukakiacha.
زیرا هر گاه کلامی که بوساطت فرشتگان گفته شد برقرار گردید، بقسمی که هر تجاوز وتغافلی را جزای عادل می‌رسید، ۲ 2
Kwa kuwa kama ujumbe ulionenwa na malaika ulikuwa imara, na kila uasi na kutokutii kulipata adhabu ya haki,
پس ما چگونه رستگار گردیم اگر از چنین نجاتی عظیم غافل باشیم؟ که در ابتدا تکلم به آن از خداوند بود و بعدکسانی که شنیدند، بر ما ثابت گردانیدند؛ ۳ 3
je, sisi tutapaje kupona kama tusipojali wokovu mkuu namna hii? Wokovu huu, ambao mwanzo ulitangazwa na Bwana, ulithibitishwa kwetu na wale waliomsikia.
درحالتی که خدا نیز با ایشان شهادت می‌داد به آیات و معجزات و انواع قوات و عطایای روح‌القدس برحسب اراده خود. ۴ 4
Pia Mungu aliushuhudia kwa ishara, maajabu na kwa miujiza mbalimbali, na karama za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake.
زیرا عالم آینده‌ای را که ذکر آن را می‌کنیم مطیع فرشتگان نساخت. ۵ 5
Mungu hakuuweka ulimwengu ujao ambao tunanena habari zake chini ya malaika.
لکن کسی در موضعی شهادت داده، گفت: «چیست انسان که او را بخاطرآوری یا پسر انسان که از او تفقد نمایی؟ ۶ 6
Lakini kuna mahali mtu fulani ameshuhudia akisema: “Mwanadamu ni kitu gani hata unamfikiria, binadamu ni nani hata unamjali?
او را ازفرشتگان اندکی پست‌تر قرار دادی و تاج جلال واکرام را بر سر او نهادی و او را بر اعمال دستهای خود گماشتی. ۷ 7
Umemfanya chini kidogo kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
همه‌چیز را زیر پایهای اونهادی.» پس چون همه‌چیز را مطیع او گردانید، هیچ‌چیز را نگذاشت که مطیع او نباشد. لکن الان هنوز نمی بینیم که همه‌چیز مطیع وی شده باشد. ۸ 8
nawe umeweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Kwa kuweka vitu vyote chini yake, Mungu hakuacha kitu chochote ambacho hakukiweka chini ya mwanadamu. Lakini kwa sasa, hatuoni kwamba kila kitu kiko chini yake.
اما او را که اندکی از فرشتگان کمتر شد می‌بینیم، یعنی عیسی را که به زحمت موت تاج جلال واکرام بر سر وی نهاده شد تا به فیض خدا برای همه ذائقه موت را بچشد. ۹ 9
Lakini twamwona Yesu, aliyefanywa chini kidogo kuliko malaika, sasa akiwa amevikwa taji ya utukufu na heshima kwa sababu alistahimili mauti, ili kwamba kwa neema ya Mungu apate kuonja mauti kwa ajili ya kila mtu.
زیرا او را که بخاطروی همه و از وی همه‌چیز می‌باشد، چون فرزندان بسیار را وارد جلال می‌گرداند، شایسته بود که رئیس نجات ایشان را به دردها کامل گرداند. ۱۰ 10
Ili kuwaleta wana wengi katika utukufu, ilifaa kwamba Mungu, ambaye ni kwa ajili yake na kupitia kwake kila kitu kimekuwepo, amkamilishe mwanzilishi wa wokovu wao kwa njia ya mateso.
زانرو که چون مقدس کننده و مقدسان همه از یک می‌باشند، از این جهت عار ندارد که ایشان را برادر بخواند. ۱۱ 11
Yeye awafanyaye watu kuwa watakatifu, pamoja na hao ambao hufanywa watakatifu, wote hutoka katika jamaa moja. Hivyo Yesu haoni aibu kuwaita ndugu zake.
چنانکه می‌گوید: «اسم تو را به برادران خود اعلام می‌کنم و در میان کلیساتو را تسبیح خواهم خواند.» ۱۲ 12
Yeye husema, “Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; mbele ya kusanyiko nitaimba sifa zako.”
و ایض: «من بروی توکل خواهم نمود.» و نیز: «اینک من وفرزندانی که خدا به من عطا فرمود.» ۱۳ 13
Tena, “Nitaweka tumaini langu kwake.” Tena anasema, “Niko hapa, pamoja na watoto ambao Mungu amenipa.”
پس چون فرزندان در خون و جسم شراکت دارند، او نیز همچنان در این هر دو شریک شد تابوساطت موت، صاحب قدرت موت یعنی ابلیس را تباه سازد، ۱۴ 14
Basi kwa kuwa watoto wana nyama na damu, yeye pia alishiriki katika ubinadamu wao, ili kwa kifo chake, apate kumwangamiza huyo mwenye nguvu za mauti, yaani ibilisi,
و آنانی را که از ترس موت، تمام عمر خود را گرفتار بندگی می‌بودند، آزاد گرداند. ۱۵ 15
na kuwaweka huru wale waliokuwa utumwani maisha yao yote kwa sababu ya kuogopa mauti.
زیرا که در حقیقت فرشتگان را دستگیری نمی نماید بلکه نسل ابراهیم را دستگیری می‌نماید. ۱۶ 16
Kwa kuwa ni dhahiri kwamba hakuja kusaidia malaika, bali uzao wa Abrahamu.
از این جهت می‌بایست در هر امری مشابه برادران خود شود تا در امور خدا رئیس کهنه‌ای کریم و امین شده، کفاره گناهان قوم رابکند. ۱۷ 17
Kwa sababu hii ilibidi afanane na ndugu zake kwa kila hali, ili apate kuwa Kuhani Mkuu mwenye huruma na mwaminifu katika kumtumikia Mungu, ili pia apate kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi za watu.
زیرا که چون خود عذاب کشیده، تجربه دید استطاعت دارد که تجربه شدگان را اعانت فرماید. ۱۸ 18
Kwa kuwa yeye mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.

< عبرانیان 2 >