< غلاطیان 1 >

پولس، رسول نه از جانب انسان و نه بوسیله انسان بلکه به عیسی مسیح و خدای پدر که او را از مردگان برخیزانید، ۱ 1
Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
و همه برادرانی که بامن می‌باشند، به کلیساهای غلاطیه، ۲ 2
na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
فیض و سلامتی از جانب خدای پدر وخداوند ما عیسی مسیح با شما باد؛ ۳ 3
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
که خود رابرای گناهان ما داد تا ما را از این عالم حاضر شریربحسب اراده خدا و پدر ما خلاصی بخشد، (aiōn g165) ۴ 4
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
که او را تا ابدالاباد جلال باد. آمین. (aiōn g165) ۵ 5
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
تعجب می‌کنم که بدین زودی از آن کس که شما را به فیض مسیح خوانده است، برمی گردیدبه سوی انجیلی دیگر، ۶ 6
Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
که (انجیل ) دیگر نیست. لکن بعضی هستند که شما را مضطرب می‌سازندو می‌خواهند انجیل مسیح را تبدیل نمایند. ۷ 7
ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
بلکه هرگاه ما هم یا فرشته‌ای از آسمان، انجیلی غیر از آنکه ما به آن بشارت دادیم به شما رساند، اناتیما باد. ۸ 8
Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
چنانکه پیش گفتیم، الان هم بازمی گویم: اگر کسی انجیلی غیر از آنکه پذیرفتیدبیاورد، اناتیما باد. ۹ 9
Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
آیا الحال مردم را در رای خود می‌آورم؟ یا خدا را یا رضامندی مردم را می طلبم؟ اگر تابحال رضامندی مردم رامی خواستم، غلام مسیح نمی بودم. ۱۰ 10
Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
اما‌ای برادران شما را اعلام می‌کنم ازانجیلی که من بدان بشارت دادم که به طریق انسان نیست. ۱۱ 11
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
زیرا که من آن را از انسان نیافتم ونیاموختم، مگر به کشف عیسی مسیح. ۱۲ 12
Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
زیراسرگذشت سابق مرا در دین یهود شنیده‌اید که برکلیسای خدا بینهایت جفا می‌نمودم و آن راویران می‌ساختم، ۱۳ 13
Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
و در دین یهود از اکثرهمسالان قوم خود سبقت می‌جستم و در تقالیداجداد خود بغایت غیور می‌بودم. ۱۴ 14
Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
اما چون خداکه مرا از شکم مادرم برگزید و به فیض خود مراخواند، رضا بدین داد ۱۵ 15
Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
که پسر خود را در من آشکار سازد تا در میان امت‌ها بدو بشارت دهم، در آنوقت با جسم و خون مشورت نکردم، ۱۶ 16
alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
و به اورشلیم هم نزد آنانی که قبل از من رسول بودندنرفتم، بلکه به عرب شدم و باز به دمشق مراجعت کردم. ۱۷ 17
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
پس بعد از سه سال، برای ملاقات پطرس به اورشلیم رفتم و پانزده روز با وی بسر بردم. ۱۸ 18
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
اما از سایر رسولان جز یعقوب برادر خداوندرا ندیدم. ۱۹ 19
Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
اما درباره آنچه به شما می‌نویسم، اینک در حضور خدا دروغ نمی گویم. ۲۰ 20
Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
بعد از آن به نواحی سوریه و قیلیقیه آمدم. ۲۱ 21
Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
و به کلیساهای یهودیه که در مسیح بودند صورت غیرمعروف بودم، ۲۲ 22
Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
جز اینکه شنیده بودند که «آنکه پیشتر بر ما جفا می‌نمود، الحال بشارت می‌دهد به همان ایمانی که قبل از این ویران می‌ساخت.» ۲۳ 23
Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
و خدا را در من تمجید نمودند. ۲۴ 24
Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.

< غلاطیان 1 >