< 2 تیموتاوس 2 >

پس تو‌ای فرزند من، در فیضی که در مسیح عیسی است زورآور باش. ۱ 1
Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
و آنچه به شهود بسیار از من شنیدی، به مردمان امین بسپارکه قابل تعلیم دیگران هم باشند. ۲ 2
Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
چون سپاهی نیکوی مسیح عیسی در تحمل زحمات شریک باش. ۳ 3
Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
هیچ سپاهی خود را در امور روزگار گرفتارنمی سازد تا رضایت آنکه او را سپاهی ساخت بجوید. ۴ 4
Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
و اگر کسی نیز پهلوانی کند، تاج را بدونمی دهند اگر به قانون پهلوانی نکرده باشد. ۵ 5
Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
برزگری که محنت می‌کشد، باید اول نصیبی ازحاصل ببرد. ۶ 6
Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
در آنچه می‌گویم تفکر کن زیراخداوند تو را در همه‌چیز فهم خواهد بخشید. ۷ 7
Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
عیسی مسیح را بخاطر دار که از نسل داودبوده، از مردگان برخاست برحسب بشارت من، ۸ 8
Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
که در آن چون بدکار تا به بندها زحمت می‌کشم، لیکن کلام خدا بسته نمی شود. ۹ 9
ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
و ازاین جهت همه زحمات را بخاطر برگزیدگان متحمل می‌شوم تا ایشان نیز نجاتی را که درمسیح عیسی است با جلال جاودانی تحصیل کنند. (aiōnios g166) ۱۰ 10
Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
این سخن امین است زیرا اگر با وی مردیم، با او زیست هم خواهیم کرد. ۱۱ 11
Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
و اگرتحمل کنیم، با او سلطنت هم خواهیم کرد؛ وهرگاه او را انکار کنیم او نیز ما را انکار خواهدکرد. ۱۲ 12
Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
اگر بی‌ایمان شویم، او امین می‌ماند زیراخود را انکار نمی تواند نمود. ۱۳ 13
Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
این چیزها را به یاد ایشان آور و در حضورخداوند قدغن فرما که مجادله نکنند، زیرا هیچ سود نمی بخشد بلکه باعث هلاکت شنوندگان می‌باشد. ۱۴ 14
Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
و سعی کن که خود را مقبول خداسازی، عاملی که خجل نشود و کلام خدا رابخوبی انجام دهد. ۱۵ 15
Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
و از یاوه‌گویی های حرام اعراض نما زیرا که تا به فزونی بی‌دینی ترقی خواهد کرد. ۱۶ 16
Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
و کلام ایشان، چون آکله می‌خورد و از آنجمله هیمیناوس و فلیطس می‌باشند ۱۷ 17
Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
که ایشان از حق برگشته، می‌گویندکه قیامت الان شده است و بعضی را از ایمان منحرف می‌سازند. ۱۸ 18
ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
و لیکن بنیاد ثابت خدا قائم است و این مهر را دارد که «خداوند کسان خود رامی شناسد» و «هرکه نام مسیح را خواند، ازناراستی کناره جوید.» ۱۹ 19
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
اما در خانه بزرگ نه فقطظروف طلا و نقره می‌باشد، بلکه چوبی و گلی نیز؛ اما آنها برای عزت و اینها برای ذلت. ۲۰ 20
Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
پس اگرکسی خویشتن را از اینها طاهر سازد، ظرف عزت خواهد بود مقدس و نافع برای مالک خود ومستعد برای هر عمل نیکو. ۲۱ 21
Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
اما از شهوات جوانی بگریز و با آنانی که ازقلب خالص نام خداوند را می‌خوانند، عدالت وایمان و محبت و سلامتی را تعاقب نما. ۲۲ 22
Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
لیکن ازمسائل بیهوده و بی‌تادیب اعراض نما چون می‌دانی که نزاعها پدید می‌آورد. ۲۳ 23
Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
اما بنده خدانباید نزاع کند، بلکه با همه کس ملایم و راغب به تعلیم و صابر در مشقت باشد، ۲۴ 24
Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
و با حلم مخالفین را تادیب نماید که شاید خدا ایشان راتوبه بخشد تا راستی را بشناسند. ۲۵ 25
Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
تا از دام ابلیس باز به هوش آیند که به حسب اراده او صیداو شده‌اند. ۲۶ 26
ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.

< 2 تیموتاوس 2 >