< 1 تیموتاوس 1 >

پولس، رسول عیسی مسیح به حکم نجات‌دهنده ما خدا و مسیح عیسی خداوند که امید ما است، ۱ 1
Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na ya Kristo Yesu tumaini letu.
به فرزند حقیقی خود در ایمان، تیموتاوس. فیض و رحم و سلامتی از جانب خدای پدر وخداوند ما مسیح عیسی بر تو باد. ۲ 2
Kwa Timotheo, mwanangu halisi katika imani: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.
چنانکه هنگامی که عازم مکادونیه بودم، به شما التماس نمودم که در افسس بمانی تا بعضی را امر کنی که تعلیمی دیگر ندهند، ۳ 3
Kama nilivyokusihi wakati nilipokwenda Makedonia, endelea kubaki Efeso, ili kwamba upate kuwaagiza watu wasiendelee kufundisha mafundisho ya uongo
و افسانه‌ها ونسب نامه های نامتناهی را اصغا ننمایند که اینهامباحثات را نه آن تعمیر الهی را که در ایمان است پدید می‌آورد. ۴ 4
wala wasitoe muda wao kwa hadithi za kubuniwa na orodha za majina ya vizazi visivyo na mwisho, ambazo huchochea mabishano badala ya mpango wa Mungu utokanao na imani.
اما غایت حکم، محبت است ازدل پاک و ضمیر صالح و ایمان بی‌ریا. ۵ 5
Kusudi la maagizo haya ni upendo utokao katika moyo safi, dhamiri njema na imani ya kweli.
که از این امور بعضی منحرف گشته به بیهوده‌گویی توجه نموده‌اند، ۶ 6
Watu wengine wamepotoka kutoka haya na kugeukia majadiliano yasiyo na maana kwa kuwa,
و می‌خواهند معلمان شریعت بشوندو حال آنکه نمی فهمند آنچه می‌گویند و نه آنچه به تاکید اظهار می‌نمایند. ۷ 7
wanataka kuwa walimu wa sheria, lakini hawajui mambo yale wanayosema wala hayo wanayoyatumainia kwa uthabiti.
لیکن می‌دانیم که شریعت نیکو است اگرکسی آن را برحسب شریعت بکار برد. ۸ 8
Tunajua kwamba sheria ni njema ikiwa inatumika kwa halali kama ilivyokusudiwa.
و این بداند که شریعت بجهت عادل موضوع نمی شود، بلکه برای سرکشان و طاغیان و بی‌دینان وگناهکاران و ناپاکان و حرامکاران و قاتلان پدر و قاتلان مادر و قاتلان مردم ۹ 9
Lakini tunajua ya kuwa sheria si kwa ajili ya wenye haki, bali kwa ajili ya wavunja sheria na waasi, kwa ajili ya wasiomcha Mungu na wenye dhambi, wasio watakatifu na wanaokufuru; kwa wale wawauao baba zao au mama zao, kwa wauaji,
و زانیان و لواطان ومردم دزدان و دروغ‌گویان و قسم دروغ خوران وبرای هر عمل دیگری که برخلاف تعلیم صحیح باشد، ۱۰ 10
kwa wazinzi na wahanithi, kwa wale wauzao watu, na kwa waongo na waapao kwa uongo, na kwa chochote kingine kilicho kinyume na mafundisho ya kweli,
برحسب انجیل جلال خدای متبارک که به من سپرده شده است. ۱۱ 11
ambayo yanakubaliana na Injili ya utukufu wa Mungu anayehimidiwa, ambayo mimi nimewekewa amana.
و شکر می‌کنم خداوند خود مسیح عیسی را که مرا تقویت داد، چونکه امین شمرده، به این خدمتم ممتاز فرمود، ۱۲ 12
Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu, kwa sababu aliniona mwaminifu, akaniteua kwa kazi yake.
که سابق کفرگو و مضر وسقطگو بودم، لیکن رحم یافتم از آنرو که ازجهالت در بی‌ایمانی کردم. ۱۳ 13
Ingawa wakati fulani nilikuwa mwenye kukufuru, mtesaji na mwenye jeuri, lakini nilipata rehema kwa sababu nilitenda hivyo kwa kutojua na kutoamini kwangu.
اما فیض خداوندما بی‌نهایت افزود با‌ایمان و محبتی که در مسیح عیسی است. ۱۴ 14
Neema ya Bwana wetu ilimiminwa juu yangu kwa wingi, ikiambatana na imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
این سخن امین است و لایق قبول تام که مسیح عیسی به‌دنیا آمد تا گناهکاران را نجات‌بخشد که من بزرگترین آنها هستم. ۱۵ 15
Msemo huu ni wa kweli na unaostahili kukubalika, usemao kwamba: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuokoa wenye dhambi, ambao mimi ndiye niliye mbaya kuliko wote.
بلکه از این جهت بر من رحم شد تا اول درمن، مسیح عیسی کمال حلم را ظاهر سازد تا آنانی را که بجهت حیات جاودانی به وی ایمان خواهند‌آورد، نمونه باشم. (aiōnios g166) ۱۶ 16
Lakini kwa sababu hiyo nilipata rehema, ili katika mimi, niliyekuwa mwenye dhambi kuliko wote, Kristo Yesu apate kuonyesha uvumilivu wake usio na kikomo, ili niwe kielelezo kwa wale watakaomwamini na wapate uzima wa milele. (aiōnios g166)
باری پادشاه سرمدی و باقی ونادیده را، خدای حکیم وحید را اکرام و جلال تاابدالاباد باد. آمین. (aiōn g165) ۱۷ 17
Basi Mfalme wa milele, asiye na mwisho, asiyeonekana, aliye Mungu pekee, apewe heshima na utukufu milele na milele. Amen. (aiōn g165)
‌ای فرزند تیموتاوس، این وصیت را به تو می سپارم برحسب نبوتهایی که سابق بر تو شد تادر آنها جنگ نیکو کنی، ۱۸ 18
Mwanangu Timotheo, ninakupa agizo hili, kwa kadiri ya maneno ya unabii yaliyosemwa kukuhusu, ili kwa kuyafuata upate kupigana vita vizuri,
و ایمان و ضمیرصالح را نگاه داری که بعضی این را از خود دورانداخته، مر ایمان را شکسته کشتی شدند. ۱۹ 19
ukiishikilia imani na dhamiri njema, ambazo wengine wamevikataa, na hivyo wakaangamia kwa habari ya imani yao.
که از آن جمله هیمیناوس و اسکندر می‌باشند که ایشان را به شیطان سپردم تا تادیب شده، دیگرکفر نگویند. ۲۰ 20
Miongoni mwao wako Himenayo na Aleksanda, ambao nimemkabidhi Shetani ili wafundishwe wasije wakakufuru.

< 1 تیموتاوس 1 >