< اول پطرس 3 >

همچنین‌ای زنان، شوهران خود را اطاعت نمایید تا اگر بعضی نیز مطیع کلام نشوند، سیرت زنان، ایشان را بدون کلام دریابد، ۱ 1
Kadhalika enyi wake, watiini waume zenu, ili kama kunao wasioamini lile neno, wapate kuvutwa na mwenendo wa wake zao pasipo neno,
چونکه سیرت طاهر و خداترس شما را بینند. ۲ 2
kwa kuuona utakatifu na uchaji wa Mungu katika maisha yenu.
و شما رازینت ظاهری نباشد، از بافتن موی و متحلی شدن به طلا و پوشیدن لباس، ۳ 3
Kujipamba kwenu kusiwe kwa nje tu, kama vile kusuka nywele, kuvalia vitu vilivyofanyizwa kwa dhahabu na kwa mavazi.
بلکه انسانیت باطنی قلبی در لباس غیر فاسد روح حلیم و آرام که نزدخدا گرانبهاست. ۴ 4
Badala yake, kujipamba kwenu kuwe katika utu wenu wa moyoni, yaani uzuri usioharibika wa roho ya upole na utulivu, ambayo ni ya thamani sana machoni pa Mungu.
زیرا بدینگونه زنان مقدسه درسابق نیز که متوکل به خدا بودند، خویشتن رازینت می‌نمودند و شوهران خود را اطاعت می‌کردند. ۵ 5
Kwa kuwa hivi ndivyo walivyokuwa wakijipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu. Wao walikuwa ni watiifu kwa waume zao,
مانند ساره که ابراهیم را مطیع می‌بودو او را آقا می‌خواند و شما دختران او شده‌اید، اگر نیکویی کنید و از هیچ خوف ترسان نشوید. ۶ 6
kama Sara alivyomtii mumewe Abrahamu, hata akamwita bwana. Ninyi ni watoto wa Sara kama mkitenda yaliyo mema, bila kuogopa jambo lolote.
و همچنین‌ای شوهران، با فطانت با ایشان زیست کنید، چون با ظروف ضعیف تر زنانه، وایشان را محترم دارید چون با شما وارث فیض حیات نیز هستند تا دعاهای شما بازداشته نشود. ۷ 7
Vivyo hivyo ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili, nanyi wapeni heshima mkitambua ya kuwa wao ni wenzi walio dhaifu, na kama warithi pamoja nanyi wa kipawa cha neema cha uzima, ili kusiwepo na chochote cha kuzuia maombi yenu.
خلاصه همه شما یکرای و همدرد و برادردوست و مشفق و فروتن باشید. ۸ 8
Hatimaye, ninyi nyote kuweni na nia moja, wenye kuhurumiana, mkipendana kama ndugu, na mwe wasikitivu na wanyenyekevu.
و بدی بعوض بدی و دشنام بعوض دشنام مدهید، بلکه برعکس برکت بطلبید زیرا که می‌دانید برای این خوانده شده‌اید تا وارث برکت شوید. ۹ 9
Msilipe ovu kwa ovu, au jeuri kwa jeuri, bali barikini, kwa maana hili ndilo mliloitiwa ili mpate kurithi baraka.
زیرا «هرکه می‌خواهد حیات را دوست دارد و ایام نیکو بیند، زبان خود را از بدی و لبهای خود را از فریب گفتن باز بدارد؛ ۱۰ 10
Kwa maana, “Yeyote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila.
از بدی اعراض نماید و نیکویی رابه‌جا آورد؛ سلامتی را بطلبد و آن را تعاقب نماید. ۱۱ 11
Mtu huyo lazima aache uovu, akatende mema; lazima aitafute amani na kuifuatilia sana.
از آنرو که چشمان خداوند بر عادلان است وگوشهای او به سوی دعای ایشان، لکن روی خداوند بر بدکاران است.» ۱۲ 12
Kwa maana macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza maombi yao. Bali uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu.”
و اگر برای نیکویی غیور هستید، کیست که به شما ضرری برساند؟ ۱۳ 13
Basi, ni nani atakayewadhuru mkiwa wenye juhudi katika kutenda mema?
بلکه هرگاه برای عدالت زحمت کشیدید، خوشابحال شما. پس ازخوف ایشان ترسان و مضطرب مشوید. ۱۴ 14
Lakini mmebarikiwa hata kama ikiwalazimu kuteseka kwa ajili ya haki. “Msiogope vitisho vyao, wala msiwe na wasiwasi.”
بلکه خداوند مسیح را در دل خود تقدیس نمایید وپیوسته مستعد باشید تا هرکه سبب امیدی را که دارید از شما بپرسد، او را جواب دهید، لیکن باحلم و ترس. ۱۵ 15
Bali mtakaseni Kristo kuwa Bwana mioyoni mwenu. Siku zote mwe tayari kumjibu mtu yeyote atakayewauliza kuhusu sababu ya tumaini lililomo ndani yenu. Lakini fanyeni hivyo kwa upole na kwa heshima,
و ضمیر خود را نیکو بدارید تاآنانی که بر سیرت نیکوی شما در مسیح طعن می‌زنند، در همان چیزی که شما را بد می‌گویندخجالت کشند، ۱۶ 16
mkizitunza dhamiri zenu ziwe safi, ili wale wasemao mabaya dhidi ya mwenendo wenu mzuri katika Kristo waaibike kwa ajili ya masingizio yao.
زیرا اگر اراده خدا چنین است، نیکوکار بودن و زحمت کشیدن، بهتر است ازبدکردار بودن. ۱۷ 17
Kwa maana ni afadhali kupata mateso kwa ajili ya kutenda mema, kama kuteseka huko ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kuteseka kwa kutenda maovu.
زیرا که مسیح نیز برای گناهان یک بار زحمت کشید، یعنی عادلی برای ظالمان، تا ما را نزد خدا بیاورد؛ در حالیکه بحسب جسم مرد، لکن بحسب روح زنده گشت، ۱۸ 18
Kwa kuwa Kristo naye aliteswa mara moja tu kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili ya wasio haki, ili awalete ninyi kwa Mungu. Mwili wake ukauawa, lakini akafanywa hai katika Roho.
و به آن روح نیز رفت و موعظه نمود به ارواحی که درزندان بودند، ۱۹ 19
Baada ya kufanywa hai, alikwenda na kuzihubiria roho zilizokuwa kifungoni:
که سابق نافرمانبردار بودندهنگامی که حلم خدا در ایام نوح انتظار می‌کشید، وقتی که کشتی بنا می‌شد، که در آن جماعتی قلیل یعنی هشت نفر به آب نجات یافتند، ۲۰ 20
roho hizo ambazo zamani hazikutii, wakati ule uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja katika siku za Noa, wakati wa kujenga safina, ambamo watu wachache tu, yaani watu wanane, waliokolewa ili wasiangamie kwa gharika.
که نمونه آن یعنی تعمید اکنون ما را نجات می‌بخشد (نه دور کردن کثافت جسم بلکه امتحان ضمیر صالح به سوی خدا) بواسطه برخاستن عیسی مسیح، ۲۱ 21
Nayo maji hayo ni kielelezo cha ubatizo ambao sasa unawaokoa ninyi pia: si kwa kuondoa uchafu kwenye mwili, bali kama ahadi ya dhamiri safi kwa Mungu, kwa njia ya ufufuo wa Yesu Kristo.
که به آسمان رفت و بدست راست خدا است وفرشتگان و قدرتها و قوات مطیع او شده‌اند. ۲۲ 22
Yeye ameingia mbinguni na amekaa mkono wa kuume wa Mungu; nao malaika, mamlaka na nguvu zote wametiishwa chini yake.

< اول پطرس 3 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark