< Yohana 5 >

1 Baadae pabile ni sikukuu ya Ayahudi, ni Yesu aboi kuyenda Yerusalemu.
Baada ya hapo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, na Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
2 Kolyo Yerusalemu pabile ni birika pa'nnyango wa ngondolo, lyabile likemelwa kwa lugha ya Baebrania Bethzatha, nalo lyabile ni matao matano.
Na kule Yerusalemu palikuwa na birika kwenye mlango wa kondoo, lililokuwa likiitwa kwa lugha ya Kiebrania Bethzatha, nalo lina matao matano.
3 Idadi ngolo ya atamwe babile, ipofu, iwete, au babile batipooza babile bagonjite mu'matao ago. (Uzingatie: Maneno ga mstari wa 3 kabaonekana kwaa mu'nakala inoite ya kale. “Batikugasubiri mase kutibuliwa.”)
Idadi kubwa ya wagonjwa ilikuwemo, vipofu, viwete, au waliopooza walikuwa wamelala katika matao hayo. (Zingatia: Maneno ya mstari wa 3 hayaonekani katika nakala nzuri za kale. “Wakisubiri maji kutibuliwa.”) Kwa hakikia wakati fulani malaika alishuka ndani ya Bwana na kuyatibua maji.
4 Kwa hakika muda fulani malaika auluka nkati ya Ngwana ni kuyatibua mase. Kwa nyoo. yolo ywabile wa kwanza kujingya nkati yake baada ya mase kutibuliwa apangilwe nkoti bokana na chochote chabile kintabile kwa muda woo.
Kwahiyo, yule ambaye alikuwa wa kwanza kuingia ndani ya baada ya maji kutibuliwa alifanywa mzima kutokana na chochote kilichokuwa kimemshika kwa wakati huo.
5 Ni mundu yumo ywabile ntamwe kwa miaka thelathini na minane abile nkati ya matao.
Na mtu mmoja aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka thelathini na minane alikuwa ndani ya matao.
6 Yesu paamweni agonjike nkati ya matao ni baada ya kutanga kuwa agonjike kwa muda mrefu Yesu kammakiya, “Je wapala kuwa nkoto.”
Yesu alipomwona amelala ndani ya matao na baada ya kutambua kuwa amelala pale kwa muda mrefu Yesu alimwambia, “Je unataka kuwa mzima?”
7 Yolo ntamwe kannyangwa, “Ngwana nabile kwaa na mundu, wa kunibeka mu'birika muda yabile yatitibulilwa. Muda kabanijaribu jingya mundu ywenge atikuntangulia.”
Yule mgonjwa akamjibu, “Bwana sina mtu, wa kuniweka katika birika wakati maji yanapotibuliwa. Wakati ninapojaribu kuingia mtu mwingine hunitangulia.”
8 Yesu aamkiye, “Uluka ulipotwe litandiko lyako na uyende.”
Yesu akamwambia, “Inuka na uchukue godoro lako na uende.”
9 Mara yolo mundu aponywile, alitweti kindanda sake no yenda. Lelo labibe lisoba lya sabato.
Mara yule mtu akaponywa, akachukua kintanda chake na akaenda. Na siku hiyo ilikuwa siku ya Sabato.
10 Nga Ayahudi bammakiuye, yolo mundu ywaponywile, “leno ni lisoba lya sabato, ni halalli kwaa kupotwa litandiko lyako.”
Hivyo Wayahudi wakamwambia yule mtu aliyeponywa, “Leo ni siku ya Sabato, na hauruhusiwi kubeba godoro lako.”
11 Kayangwa, ywembe ywaniponyile animakiye, “Tola litandiko lyako no uyende.”
Akajibu, yeye aliyeniponya ndiye aliyeniambia, “Chukua godoro lako na uende.”
12 Kabanlaluya, “Nyai ywakumakiye,'tola litandiko lyako no uyende.”
Wakauliza, “Ni nani aliyekuambia 'Chukua godoro lako na uende?'''
13 Ingawa, yolo ywaponywile antangite kwaa mana Yesu aboi kwa siri. Kwa mana pabile ni bandu banyansima.
Ingawa, yule aliyeponywa hakumjua, kwa sababu Yesu alikuwa ameondoka kwa siri. Kwa kuwa kulikuwa na watu wengi katika sehemu hiyo.
14 Baada ya ago Yesu amkolile yolo mundu mu'lihekalu ni kummakiya, “Linga upangite nkoto! kana upange sambi kae kana likupate likowe libaya muno.”
Baada ya hapo Yesu alimkuta yule mtu hekaluni na akamwambia, “Tazama, umepona! “Usitende dhambi tena usije ukapatwa na jambo baya zaidi.”
15 Mundu yolo kayenda ni kuamakiya Ayahudi kuwa Yesu nga amponyile.
Yule mtu akaenda na kuwataarifu Wayahudi kuwa Yesu ndiye aliyemponya.
16 Kwa mwanja wa makowe ago Ayahudi bantesike Yesu, kwa mana apangite makowe aga lisoba lya sabato.
Hivyo, kwa sababu ya mambo hayo Wayahudi walimtesa Yesu, kwa sababu alifanya mambo haya siku ya Sabato.
17 Yesu kaamakiya, “Tate bango apanga kazi nambeambea ni nenga napanga kazi.”
Yesu akawambia, “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami nafanya kazi.”
18 Kwa sababu yee Ayahudi kabampala muno ili kumulaga yapanga kwaa kae atekwile Sabato, ila kwa kunkema Nnongo Tate bake, kuipanga abile sawa ni Nnongo.
Kwa sababu hiyo Wayahudi walizidi kumtafuta ili wamuue sio tu kwa sababu ya kuivunja Sabato, bali kwa kumwita Mungu Baba yake, akijifanya kuwa sawa na Mungu.
19 Yesu kabayangwa, “Amini, amini, mwana aweza kwaa panga ilebe yeyoti ila chelo amweni Tate bake apangite, kwa mana chochote Tate akipangite nga mwana akipanga.
Yesu akawajibu, “Amini, amini, Mwana hawezi kufanya kitu chochote isipokuwa kile ambacho amemwona Baba yake anakifanya, kwa kuwa chochote Baba akifanyacho ndicho na Mwana atakachofanya.
20 Kwa kuwa Tate ampenda mwana, ni kunlolekeya kila kilebe akipangite ni kunlolekea makowe makolo kuliko aga ili muzidi shangala.
Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, na amwonyesha kila kitu anachokifanya na atamwonyesha mambo makubwa kuliko haya ili kwamba mzidi kushangaa.”
21 Kwa kuwa kati Tate atikwafufua bandu mu kiwo ni kuwapea ukoto, nga mwana umpeya yeyote ywampendae.
Kwa kuwa kama vile ambavyo Baba awafufuavyo wafu na kuwapa uzima, halikadhalika Mwana pia humpa yeyote ampendaye.
22 Kwa kuwa Tate amuhukumu kwaa yeyote, ila umpeya mwana hukumu yoti
Kwa kuwa Baba hamhukumu yeyote, bali amempa Mwana hukumu yote
23 ili kwamba boti bamweshimu Mwana kati yo panga Mwana atikumweshimu Tate. Ywembe ywamuheshimu kwaa Mwana amuheshimu kwaa ni Tate ywantumite.
ili kwamba wote wamuheshimu Mwana kama vile Mwana anavyomuheshimu Baba. Yeye asiyemuheshimu Mwana hamuheshimu Baba aliyemtuma.
24 Amini, amini, ywembe ywaliyowine neno lyango ni kuliaminiya abile ni ukoto wangayomoka ni aukumilwa kwaa. Badala yake, atipeta boka mu'kiwo no jingya mu'ukoto. (aiōnios g166)
Amini, amini, yeye asikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenituma anao uzima wa milele na hatahukumiwa. Badala yake, amepita kutoka mautini na kuingia uzimani. (aiōnios g166)
25 Amini, amini, naabakiya muda waisa nambeambe ubile ambapo bandu ba mu'kiwo balowa kuiyowa sauti ya Mwana wa Nnongo, ni boti baiyowine walowa tama.
Amini, amini, nawambia wakati unakuja na sasa upo ambao wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wote watakao sikia wataishi.
26 Kwa mana kati Tate abile ni ukoto nkati yake mwene,
Kwa kuwa kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake mwenyewe,
27 pia ampei Mwana kuwa ni ukoto nkati yake, Tate ampei mwana mamlaka ili ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
kadhalika amempa Mwana kuwa na uzima ndani yake, na Baba amempa Mwana mamlaka ili kwamba ahukumu kwa kuwa ni Mwana wa Adamu.
28 Kana mshangae lelo, kwa mana muda waisa ambao bandu bote baabile mu'makaburi walowa kuliyowa lilobe lyake
Msishangazwe na hili, kwa kuwa wakati unakuja ambao wafu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake
29 nabo baboite panja: kwa balo bapangite mema kwa ufufuo wa ukoto, na balo bapangite mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
nao watatoka nje: kwa waliotenda mema kwa ufufuo wa uzima, na walio tenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu.
30 Naweza kwaa kupanga chochote boka kwango mwene. Kati niyowine, nga nalowa kuhukumu na hukumu yango ni ya haki kwa mana nipalike kwaa mapenzi yango, ila mapenzi yake ywanitumile.
Siwezi kufanya kitu chochote kutoka kwangu mwenyewe. Kama nisikiavyo, ndivyo ninavyo hukumu na hukumu yangu ni ya haki kwa kuwa sitafuti mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.
31 Kati ya panga nishuhudia mwene, ushuhuda wango wabile kwaa wa kweli.
Kama nikijishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu usingelikuwa wa kweli.
32 Kwabile ni ywenge ywanishuhudia nenga na nitangite kwa hakika kuwa ushuhuda waaushudie ni wa kweli.
Kuna mwingine anayeshuhudia kuhusu mimi na ninajua kwa hakika ushuhuda anaonishuhudia ni wa kweli.
33 Mumtumile kwa Yohana ni ywembe atikwashuhudia kweli.
Mmetuma kwa Yohana naye ameishuhudia kweli.
34 Hata nyoo, ushuhuda waniupokeile uboka kwaa ka mundu. Niabaya aga ili muweze kulopolelwa.
Hatahivyo, ushuhuda ninaoupokea hautoki kwa mwanadamu. Ninayasema haya ili kwamba mweze kuokolewa.
35 Yohana abile taa yaiyaka na ng'ara, na mwabile tayari kuipuraia kwa muda nkolo bweya yake.
Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara, na mlikuwa tayari kuifurahia kwa muda kitambo nuru yake.
36 Ushuhuda wanibile nao ni nkolo kuliko wolo wa Yohana kwa kasi ambazo Tate anipei kuikamilisha, izo kazi nizipangite kwa ushuhuda kuwa Tate anitumile.
Ushuhuda nilionao ni mkuu kuliko ule wa Yohana, kwa kazi ambazo Baba amenipa kuzikamilisha, hizo kazi nizifanyazo zashuhudia kuwa Baba amenituma.
37 Tate ywanitumile ywembe mwene atikwashuhudia kuhusu nenga. Muyowine kwaa lilobe lyake wala kubonekeya liumbo lyake wakati wowote.
Baba aliyenituma yeye mwenyewe ameshuhudia kuhusu mimi. Hamjawahi kusikia sauti yake wala kuona umbo lake wakati wowote.
38 Ntopo neno lyake nkati yinu kwa mana mumwaminiye kwaa ywembe ywanitumile.
Hamna neno lake likikaa ndani yenu kwa kuwa hamumwamini yeye aliyetumwa.
39 Mugachunguza maandiko mkidhani mwabile ni ukoto wangeyomoka nkati yake, na maandiko ago yaashuhudia habari yango na (aiōnios g166)
Mnayachunguza maandiko mkidhani ndani yake mna uzima wa milele, na hayo maandiko yanashuhudia habari zangu na (aiōnios g166)
40 mukani kuisa kwango ili mpate ukoto wangeyomoka.
hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima wa milele.
41 Nenga nipokya kwaa sifa boka kwa bandu.
Sipokei sifa kutoka kwa watu,
42 Lakini nitangite kuwa ntopo upendo wa Nnongo yinu mwenga mwabene.
lakini ninajua kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu ninyi wenyewe.
43 Nenga niisile kwa lina lya Tate bango, muweza kwaa kunipokya. Kati ywenge aisa kwa lina lyake mwalowa kumpokya.
Nimekuja kwa jina la Baba yangu, hamukuweza kunipokea. Kama mwingine akija kwa jina lake mngempokea.
44 Je muweza kwaa kuamini mwenga ambao mpala kwaa sifa iboka kwa Nnongo wa pekee?
Je mnawezaje kuamini ninyi ambao mnapokea sifa kutoka kwa kila mmoja wenu lakini hamtafuti sifa itokayo kwa Mungu wa pekee?
45 Kana muwaze nenga nitabashitaki nnonge ya Tate. Ywaabashitakiya mwenga ni Musa, ambaye mwenga mubekite matumaini yinu kwake.
Msidhani mimi nitawashitaki mbele za Baba. Anayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye ninyi mmeweka matumaini yenu kwake.
46 Kati mwatikumwamini Musa, mwalowa kuniamini nenga kwa kuwa ywembe aandikile habari zangu nenga.
Kama mngekuwa mnamwamini Musa, mngeniamini mimi kwa sababu aliandika kuhusu habari zangu.
47 Muyaamini kwaa maandiko gake, mwaweza kwaa kugaamini maneno yango?
Kama hamuamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?

< Yohana 5 >