< Psalmorum 88 >

1 canticum psalmi filiis Core in finem pro Maeleth ad respondendum intellectus Eman Ezraitae Domine Deus salutis meae die clamavi et nocte coram te
Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
2 intret in conspectu tuo oratio mea inclina aurem tuam ad precem meam
Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
3 quia repleta est malis anima mea et vita mea in inferno adpropinquavit (Sheol h7585)
Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
4 aestimatus sum cum descendentibus in lacum factus sum sicut homo sine adiutorio
Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5 inter mortuos liber sicut vulnerati dormientes in sepulchris quorum non es memor amplius et ipsi de manu tua repulsi sunt
Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6 posuerunt me in lacu inferiori in tenebrosis et in umbra mortis
Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7 super me confirmatus est furor tuus et omnes fluctus tuos induxisti super me diapsalma
Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
8 longe fecisti notos meos a me posuerunt me abominationem sibi traditus sum et non egrediebar
Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9 oculi mei languerunt prae inopia clamavi ad te Domine tota die expandi ad te manus meas
Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
10 numquid mortuis facies mirabilia aut medici suscitabunt et confitebuntur tibi diapsalma
Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
11 numquid narrabit aliquis in sepulchro misericordiam tuam et veritatem tuam in perditione
Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
12 numquid cognoscentur in tenebris mirabilia tua et iustitia tua in terra oblivionis
Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
13 et ego ad te Domine clamavi et mane oratio mea praeveniet te
Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
14 ut quid Domine repellis orationem meam avertis faciem tuam a me
Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
15 pauper sum ego et in laboribus a iuventute mea exaltatus autem humiliatus sum et conturbatus
Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
16 in me transierunt irae tuae et terrores tui conturbaverunt me
Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
17 circuierunt me sicut aqua tota die circumdederunt me simul
Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
18 elongasti a me amicum et proximum et notos meos a miseria
Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.

< Psalmorum 88 >