< Psalmorum 115 >

1 Non nobis Domine, non nobis: sed nomini tuo da gloriam.
Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
2 Super misericordia tua, et veritate tua: nequando dicant Gentes: Ubi est Deus eorum?
Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
3 Deus autem noster in cælo: omnia quæcumque voluit, fecit.
Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
4 Simulacra gentium argentum, et aurum, opera manuum hominum.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
5 Os habent, et non loquentur: oculos habent, et non videbunt.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
6 Aures habent, et non audient: nares habent, et non odorabunt.
zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
7 Manus habent, et non palpabunt: pedes habent, et non ambulabunt: non clamabunt in gutture suo.
Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
8 Similes illis fiant qui faciunt ea: et omnes qui confidunt in eis.
Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
9 Domus Israel speravit in Domino: adiutor eorum et protector eorum est.
Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
10 Domus Aaron speravit in Domino: adiutor eorum et protector eorum est.
Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
11 Qui timent Dominum, speraverunt in Domino: adiutor eorum et protector eorum est.
Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
12 Dominus memor fuit nostri: et benedixit nobis: Benedixit domui Israel: benedixit domui Aaron.
Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
13 Benedixit omnibus, qui timent Dominum, pusillis cum maioribus.
Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
14 Adiiciat Dominus super vos: super vos, et super filios vestros.
Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
15 Benedicti vos a Domino, qui fecit cælum, et terram.
Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
16 Cælum cæli Domino: terram autem dedit filiis hominum.
Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
17 Non mortui laudabunt te Domine: neque omnes, qui descendunt in infernum. (questioned)
Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
18 Sed nos qui vivimus, benedicimus Domino, ex hoc nunc et usque in sæculum.
bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.

< Psalmorum 115 >