< Job 41 >

1 An extrahere poteris leviathan hamo, et fune ligabis linguam eius?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 Numquid pones circulum in naribus eius, aut armilla perforabis maxillam eius?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 Numquid multiplicabit ad te preces, aut loquetur tibi mollia?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 Numquid feriet tecum pactum, et accipies eum servum sempiternum?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 Numquid illudes ei quasi avi, aut ligabis eum ancillis tuis?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 Concident eum amici, divident illum negotiatores?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 Numquid implebis sagenas pelle eius, et gurgustium piscium capite illius?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Pone super eum manum tuam: memento belli, nec ultra addas loqui.
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Ecce, spes eius frustrabitur eum, et videntibus cunctis præcipitabitur.
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Non quasi crudelis suscitabo eum: quis enim resistere potest vultui meo?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 Quis ante dedit mihi, ut reddam ei? omnia quæ sub cælo sunt, mea sunt.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 Non parcam ei, et verbis potentibus, et ad deprecandum compositis.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 Quis revelabit faciem indumenti eius? et in medium oris eius quis intrabit?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 Portas vultus eius quis aperiet? per gyrum dentium eius formido.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Corpus illius quasi scuta fusilia, compactum squamis se prementibus.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 Una uni coniungitur, et ne spiraculum quidem incedit per eas:
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 Una alteri adhærebit, et tenentes se nequaquam separabuntur.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Sternutatio eius splendor ignis, et oculi eius, ut palpebræ diluculi.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 De ore eius lampades procedunt, sicut tædæ ignis accensæ.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 De naribus eius procedit fumus, sicut ollæ succensæ atque ferventis.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Halitus eius prunas ardere facit, et flamma de ore eius egreditur.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 In collo eius morabitur fortitudo, et faciem eius præcedit egestas.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Membra carnium eius cohærentia sibi: mittet contra eum fulmina, et ad locum alium non ferentur.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Cor eius indurabitur tamquam lapis, et stringetur quasi malleatoris incus.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Cum sublatus fuerit, timebunt angeli, et territi purgabuntur.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Cum apprehenderit eum gladius, subsitere non poterit neque hasta, neque thorax:
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 Reputabit enim quasi paleas ferrum, et quasi lignum putridum, æs.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Non fugabit eum vir sagittarius, in stipulam versi sunt ei lapides fundæ.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Quasi stipulam æstimabit malleum, et deridebit vibrantem hastam.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Sub ipso erunt radii solis, et sternet sibi aurum quasi lutum.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Fervescere faciet quasi ollam profundum mare, et ponet quasi cum unguenta bulliunt.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 Post eum lucebit semita, æstimabit abyssum quasi senescentem.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 Non est super terram potestas, quæ comparetur ei, qui factus est ut nullum timeret.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Omne sublime videt, ipse est rex super universos filios superbiæ.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Job 41 >