< Job 40 >

1 Et adiecit Dominus, et locutus est ad Iob:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 Numquid qui contendit cum Deo, tam facile conquiescit? utique qui arguit Deum, debet respondere ei.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Respondens autem Iob Domino, dixit:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Qui leviter locutus sum, respondere quid possum? manum meam ponam super os meum.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Unum locutus sum, quod utinam non dixissem: et alterum, quibus ultra non addam.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Respondens autem Dominus Iob de turbine, dixit:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Accinge sicut vir lumbos tuos: interrogabo te: et indica mihi.
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 Numquid irritum facies iudicium meum: et condemnabis me, ut te iustificeris?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Et si habes brachium sicut Deus, et si voce simili tonas?
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 Circumda tibi decorem, et in sublime erigere, et esto gloriosus, et speciosis induere vestibus.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Disperge superbos in furore tuo, et respiciens omnem arrogantem humilia.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Respice cunctos superbos, et confunde eos, et contere impios in loco suo.
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 Absconde eos in pulvere simul, et facies eorum demerge in foveam:
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Et ego confitebor quod salvare te possit dextera tua.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Ecce, Behemoth, quem feci tecum, fœnum quasi bos comedet:
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Fortitudo eius in lumbis eius, et virtus illius in umbilico ventris eius.
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 Stringit caudam suam quasi cedrum, nervi testiculorum eius perplexi sunt.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Ossa eius velut fistulæ æris, cartilago illius quasi laminæ ferreæ.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Ipse est principium viarum Dei, qui fecit eum, applicabit gladium eius.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Huic montes herbas ferunt: omnes bestiæ agri ludent ibi.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Sub umbra dormit in secreto calami, et in locis humentibus.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Protegunt umbræ umbram eius, circumdabunt eum salices torrentis.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Ecce, absorbebit fluvium, et non mirabitur: et habet fiduciam quod influat Iordanis in os eius.
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 In oculis eius quasi hamo capiet eum, et in sudibus perforabit nares eius.
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >