< Job 30 >

1 Nunc autem derident me iuniores tempore, quorum non dignabar patres ponere cum canibus gregis mei:
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
2 Quorum virtus manuum mihi erat pro nihilo, et vita ipsa putabantur indigni.
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
3 Egestate et fame steriles, qui rodebant in solitudine, squallentes calamitate, et miseria.
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
4 Et mandebant herbas, et arborum cortices, et radix iuniperorum erat cibus eorum.
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
5 Qui de convallibus ista rapientes, cum singula reperissent, ad ea cum clamore currebant.
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
6 In desertis habitabant torrentium, et in cavernis terræ, vel super glaream.
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
7 Qui inter huiuscemodi lætabantur, et esse sub sentibus delicias computabant.
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
8 Filii stultorum et ignobilium, et in terra penitus non parentes.
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
9 Nunc in eorum canticum versus sum, et factus sum eis in proverbium.
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
10 Abominantur me, et longe fugiunt a me, et faciem meam conspuere non verentur.
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
11 Pharetram enim suam aperuit, et afflixit me, et frenum posuit in os meum.
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
12 Ad dexteram orientis calamitates meæ illico surrexerunt: pedes meos subverterunt, et oppresserunt quasi fluctibus semitis suis.
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
13 Dissipaverunt itinera mea, insidiati sunt mihi, et prævaluerunt, et non fuit qui ferret auxilium.
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
14 Quasi rupto muro, et aperta ianua, irruerunt super me, et ad meas miserias devoluti sunt.
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
15 Redactus sum in nihilum: abstulisti quasi ventus desiderium meum: et velut nubes pertransiit salus mea.
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
16 Nunc autem in memetipso marcescit anima mea, et possident me dies afflictionis.
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
17 Nocte os meum perforatur doloribus: et qui me comedunt, non dormiunt.
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
18 In multitudine eorum consumitur vestimentum meum, et quasi capito tunicæ succinxerunt me.
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
19 Comparatus sum luto, et assimilatus sum favillæ et cineri.
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
20 Clamo ad te, et non exaudis me: sto, et non respicis me.
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
21 Mutatus es mihi in crudelem, et in duritia manus tuæ adversaris mihi.
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
22 Elevasti me, et quasi super ventum ponens elisisti me valide.
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
23 Scio quia morti trades me, ubi constituta est domus omni viventi.
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
24 Verumtamen non ad consumptionem eorum emittis manum tuam: et si corruerint, ipse salvabis.
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
25 Flebam quondam super eo, qui afflictus erat, et compatiebatur anima mea pauperi.
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
26 Expectabam bona, et venerunt mihi mala: præstolabar lucem, et eruperunt tenebræ.
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
27 Interiora mea efferbuerunt absque ulla requie, prævenerunt me dies afflictionis.
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
28 Mœrens incedebam, sine furore, consurgens, in turba clamabam.
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
29 Frater fui draconum, et socius struthionum.
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
30 Cutis mea denigrata est super me, et ossa mea aruerunt præ caumate.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
31 Versa est in luctum cithara mea, et organum meum in vocem flentium.
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< Job 30 >