< Job 29 >

1 Addidit quoque Iob, assumens parabolam suam, et dixit:
Ayubu akaendelea na kusema,
2 Quis mihi tribuat, ut sim iuxta menses pristinos secundum dies, quibus Deus custodiebat me?
Ee, ningekuwa kama nilivyokuwa miezi iliyopita wakati Mungu aliponiagalia,
3 Quando splendebat lucerna eius super caput meum, et ad lumen eius ambulabam in tenebris?
taa yake ilipowaka kichwani pangu, na pale nilipotembea gizani kwa nuru yake.
4 Sicut fui in diebus adolescentiæ meæ, quando secreto Deus erat in tabernaculo meo?
Ee, kwamba ningekuwa kama nilivyokuwa katika siku za ujana wangu uhusiano wangu na Mungu ulivyokuwa mzuri,
5 Quando erat Omnipotens mecum: et in circuitu meo pueri mei?
wakati Mwenyezi alipokuwa pamoja nami, na wanangu walipokuwa karibu nami,
6 Quando lavabam pedes meos butyro, et petra fundebat mihi rivos olei?
wakati maisha yangu yalipokuwa yamejawa na utele, na mwamba uliponichuruzishia chemichemi za mafuta.
7 Quando procedebam ad portam civitatis, et in platea parabant cathedram mihi?
Nilipokwenda langoni mwa mji, nilipokaa katika eneo la mji,
8 Videbant me iuvenes, et abscondebantur: et senes assurgentes stabant.
vijana waliniona na walikaa mbali kwa kuniheshimu, na wazee waliinuka na kusimama kwa ajili yangu.
9 Principes cessabant loqui, et digitum superponebant ori suo.
Wana wa mfalme waliacha kuongea nilipofika; wangeweka mkono wao katika vinywa vyao.
10 Vocem suam cohibebant duces, et lingua eorum gutturi suo adhærebat.
Sauti za waheshimiwa zililazimishwa, na ndimi zao hazikuweza kuongea vinywani mwao.
11 Auris audiens beatificabat me, et oculus videns testimonium reddebat mihi.
Kwani baada ya kunisikia, wangenibariki; waliponiona, wangeniona na kuniheshimu
12 Eo quod liberassem pauperem vociferantem, et pupillum, cui non esset adiutor.
kwa maana nilikuwa nikiwasaidia masikini waliokuwa wakiteseka, na yatima, asiye na msaada.
13 Benedictio perituri super me veniebat, et cor viduæ consolatus sum.
Baraka zao waliokuwa karibu kuangamia zilinipata; niliufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha.
14 Iustitia indutus sum: et vestivi me, sicut vestimento et diademate, iudicio meo.
Nilijivika utakatifu, nao ulinifunika; haki yangu ilikuwa kama kanzu na kilemba.
15 Oculus fui cæco, et pes claudo.
Niliwasaidia vipofu; niliwasaidia walemavu.
16 Pater eram pauperum: et causam quam nesciebam, diligentissime investigabam.
Niliwasaidia wahitaji; niliwasaidia hata wasionijua.
17 Conterebam molas iniqui, et de dentibus illius auferebam prædam.
Nilimnyamazisha mwovu; nilimpokonya manusura kutoka katika meno yake.
18 Dicebamque: In nidulo meo moriar, et sicut palma multiplicabo dies.
Kisha nilisema nitakufa mahali salama; nitazizidisha siku zangu kama mchanga.
19 Radix mea aperta est secus aquas, et ros morabitur in messione mea.
Mizizi yangu imeenea majini, na umande kukaa usiku wote katika matawi yangu.
20 Gloria mea semper innovabitur, et arcus meus in manu mea instaurabitur.
Heshima yangu ni mpya daima, na nguvu za upinde wangu zipo katika mkono wangu kila wakati.
21 Qui me audiebant, expectabant sententiam, et intenti tacebant ad consilium meum.
Watu walinisikiliza; walinisubiri; walisikiliza ushauri wangu.
22 Verbis meis addere nihil audebant, et super illos stillabat eloquium meum.
Nilipo maliza kuongea hawakunena tena, maneno yangu yaliwatia nguvu kama mvua.
23 Expectabant me sicut pluviam, et os suum aperiebant quasi ad imbrem serotinum.
Waliningoja kama kungoja mvua; waliyathamini maneno yangu, kama walivyotamani mvua iliyokawia.
24 Siquando ridebam ad eos, non credebant, et lux vultus mei non cadebat in terram.
Niliwafurahia bila wao kutarajia; hawakukataa uzuri wa uso wangu.
25 Si voluissem ire ad eos, sedebam primus: cumque sederem quasi rex, circumstante exercitu, eram tamen mœrentium consolator.
Nilikuwa kama mfalme wao na kuwachagulia cha kufanya; nilikuwa kama mfalme katika jeshi lake, kama awafarijiye waombolezaji mazishini.

< Job 29 >