< マタイの福音書 24 >

1 第三項 イエズスエルザレムの滅亡等を豫言し給ふ イエズス[神]殿を出でて往き給ひけるに、弟子等[神]殿の構造を示さんとて近づきしかば、
Yesu alitoka hekaluni na kwenda zake. Wanafunzi wake walimwendea na kumuonesha majengo ya hekalu.
2 答へて曰ひけるは、汝等此一切の物を見るか、我誠に汝等に告ぐ、此處には一の石も崩れずして石の上に遺されじ、と。
Laikni aliwajibu na kuwaambia, “Je, hamuyaoni mambo haya yote? Kweli nawaambia, hakuna jiwe litalobaki juu ya lingine bila kubomolewa.”
3 斯て橄欖山に坐し給へるに、弟子等竊に近づきて云ひけるは、此事等のあらんは何時なるぞ、又汝の再臨と世の終との兆は何なるぞ。 (aiōn g165)
Na alipokaa katika Mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake walimwendea kwa faragha na kusema, “Tuambie, mambo haya yatatokea lini? Kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu?” (aiōn g165)
4 イエズス答へて曰ひけるは、汝等人に惑はされじと注意せよ、
Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Iweni makini kwamba asije mtu akawapotosha.
5 其は多くの人我名を冒し來りて、我はキリストなりと云ひて、多くの人を惑はすべければなり。
Kwa kuwa wengi watakuja kwa jina langu. Watasema, 'Mimi ndiye Kristo', na watawapotosha wengi.
6 即汝等戰闘と戰闘の風説を聞かん、而も慎みて心を騒がす事勿れ、是等の事蓋あるべし、然れど終は未至らざるなり。
Mtasikia vita na taarifa za vita. Angalieni msije mkawa na wasiwasi, kwa kuwa mambo haya hayabudi kutokea; lakini ule mwisho utakuwa bado.
7 即民は民に、國は國に立逆らひ、又疫病飢饉地震處々にあらん、
Kwa kuwa taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi katika sehemu mbalimbali.
8 是皆苦の初なり。
Lakini mambo haya yote ni mwanzo tu wa uchungu wa kujifungua.
9 其時人々汝等を困難に陥入れ、又死に處し、汝等我名の為に萬民に憎まれん。
Ndipo watawatoa kwa ajili ya mateso na kuwaua. Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.
10 其時多くの人躓きて、互に反應し互に憎み、
Ndipo wengi watajikwaa na kusalitiana na watachukiana wenyewe kwa wenyewe.
11 又僞預言者多く起りて、多くの人を惑はさん、
Manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi.
12 且不義の溢れたるによりて、多數の人の愛冷えん、
Kwa sababu uovu utaongezeka, upendo wa wengi utapoa.
13 然れど終まで耐忍ぶ人は救はるべし。
Lakini atakaye vumilia mpaka mwisho, ataokolewa.
14 [天]國の此福音は、萬民に證として全世界に宣傳へられん、斯て後終は至るべし。
Hii Injili ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu mzima kama ushuhuda kwa mataifa yote. Na ndipo ule mwisho utafika.
15 然れば汝等、預言者ダニエルに託りて告げられし「最憎むべき荒廃」が聖所に厳然たるを見ば、
Kwa hiyo, mtakapoona chukizo la uharibifu, lililosemwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu [asomaye na afahamu],
16 読む人悟るべし。其時ユデアに居る人は山に遁るべし、
ndipo walioko Yuda wakimbilie milimani.
17 屋根に居る人は、其家より何物をか取出ださんとて下るべからず、
Na yule aliyeko juu ya paa la nyumba asiweze kuteremka chini kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya nyumba yake,
18 畑に居る人は、其上着を取らんとて歸るべからず。
naye aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
19 其日に當りて懐胎せる人、乳を哺まする人は禍なる哉。
Lakini ole wao ambao wana mtoto na wale ambao wananyonyesha katika siku hizo!
20 汝等の遁ぐる事の、或は冬、或は安息日に當らざらん事を祈れ。
Ombeni kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
21 其時には、世の始より曾て無く、又後にも有るまじき程の、大なる患難あるべければなり。
Kwa kuwa kutakuwa na dhiki kuu, ambayo haijawahi kuwapo tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, na wala haitakuwapo tena.
22 其日若縮められずば、救はるる人なからん、然れど其日は、選まれたる人々の為に縮めらるべし。
Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka. Lakini kwa sababu ya wateule, siku hizo zitafupishwa.
23 其時若人ありて汝等に、「看よキリストは此處に在り、彼處に在り」と云ふとも信ずること勿れ、
Kisha ikiwa mtu yeyote atawaambia 'Tazama, Kristo yuko hapa! au, 'Kristo yuko kule' msiamini maneno hayo.
24 其は僞キリスト及僞預言者起りて、大なる徴と奇蹟とを行ひ、能ふべくんば選まれたる人々をさへも惑はさんとすべければなり。
Kwa kuwa Makristo wa uongo na manabii wa uongo watakuja na kuonesha ishara kubwa na maajabu, kwa kusudi la kupotosha, kama ingewezekana hata na wateule.
25 我預之を汝等に告げたるぞ。然れば汝等假令、「看よキリストは荒野に在り」と云はるとも出ること勿れ、
Tazameni, nimewatahadharisha kabla ya mambo hayo kutokea.
26 「看よ奥室に在り」と云はるとも信ずること勿れ、
Kwa hiyo, ikiwa watawaambia, ''Kristo yuko jangwani,' msiende huko jangwani. Au, 'Tazameni, yuko ndani ya nyumba,' msiamini maneno hayo.
27 其は電光の東より出て西にまで見ゆる如く、人の子の來るも亦然るべければなり。
Kama vile radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
28 総て屍の在る處には鷲も亦集らん。
Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.
29 此日々の患難の後、直に日晦み、月其光を與へず、星天より隕ち、天の能力総て動揺せん。
Lakini mara baada ya dhiki kuu ya siku zile, Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbinguni zitatikisika.
30 其時人の子の徴空に現れん。其時又地の民族悉く哭き、人の子が大なる能力と威光とを以て空の雲に乗り來るを見ん。
Ndipo ishara ya Mwana wa Adamu itaonekana angani, na makabila yote ya dunia wataomboleza. Watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani kwa nguvu na utukufu mkuu.
31 彼聲高き喇叭を持てる己が天使等を遣はし、天の此涯まで、四方より其選まれし人々を集めしめん。
Atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.
32 汝等無花果樹より喩を學べ、其枝既に柔ぎて葉の生ずる時、汝等は夏の近きを知る。
Jifunzeni somo kutokana na mti mtini. Mara tu tawi linapochipuka na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kinakaribia.
33 斯の如く、此一切の事を見ば、既に門に近しと知れ。
Hivyo pia, mtakapoona mambo haya yote, mnapaswa kujua kwamba amekaribia, karibu na malango.
34 我誠に汝等に告ぐ、是等の事の皆成る迄は、現代は過ぎざらん。
Kweli nawaambia, kizazi hiki hakitapita, hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.
35 天地は過ぎん、然れど我言は過ぎざるべし。
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
36 其日其時をば何人も知らず、天使すらも知らず、知り給へるは唯父獨のみ。
Lakini kuhusu siku ile na saa hakuna mtu ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, bali Baba peke yake.
37 ノエの日に於る如く、人の子の來るも亦然らん。
Kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
38 即洪水の前の頃、ノエの方舟に入る其日までも、人々飲み食ひ娶り嫁ぎして、
Kwa kuwa katika siku hizo kabla ya gharika watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa hadi siku ile ambayo Nuhu aliingia katika safina,
39 洪水來りて悉く彼等を引浚ふまで知らざりし如く、人の子の來るも亦然らん。
na hawakujua kitu chochote hadi gharika ilipokuja na kuwasomba wote - ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.
40 其時二人畑に在らんに、一人は取られ一人は遺されん。
Ndipo watu wawili watakuwa shambani- mmoja atachukuliwa, na mmoja ataachwa nyuma.
41 二人の女磨を挽き居らんに、一人は取られ一人は遺されん。
Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja - mmoja atachukuliwa, na mmoja atabaki.
42 然れば汝等警戒せよ、汝等の主の來り給ふは何れの時なるかを知らざればなり。
Kwa hiyo, kuweni macho kwa sababu hamjui ni siku gani ambayo atakuja Bwana wenu.
43 汝等之を知れ、家父若盗賊の來るべき時を知らば、必警戒して其家を穿たせじ。
Lakini mjue kwamba, ikiwa bwana mwenye nyumba angejua ni saa ipi ambayo mwizi angekuja, angekesha na asingeruhusu nyumba yake kuvamiwa.
44 然れば汝等も用意してあれ、汝等の知らざる時に人の子來るべければなり。
Kwa hiyo, pia mnapaswa kuwa tayari, kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika saa msiyoitarajia.
45 時に應じて糧を其僕等に與へさせんとて、主人が彼等の上に立てたる、忠誠怜悧なる僕を誰と思ふぞ。
Hivyo ni nani aliye mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake amempa madaraka juu ya walio katika nyumba yake, ili awape chakula kwa wakati unaofaa?
46 其主人の來らん時、然するを見出されたる僕は福なり。
Amebarikiwa mtumishi huyo, ambaye bwana wake atamkuta akifanya hivyo wakati ajapo.
47 我誠に汝等に告ぐ、主人は其凡ての所有を是に宰らしめん。
Kweli nawaambia kwamba bwana atamweka juu ya kila kitu kilicho chake.
48 然れど若彼惡しき僕、心の中に「主人の來ること遅し」と謂ひて、
Lakini kama mtumwa mwovu akisema moyoni mwake, 'Bwana wangu amekawia,'
49 其同輩に殴掛り、酒徒と酒食を共にせば、
na akaanza kuwapiga watumishi wake, na akala na kulewa vileo,
50 其僕の主人、彼が思はざる日、知らざる時に來りて、
Bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo haitarajii, na katika saa ambayo haijui.
51 之を處罰し、其報を僞善者と同じうすべし、其處には痛哭と切歯とあらん。
Bwana wake atamkata vipande viwili na kumweka katika nafasi moja sawa na wanafiki, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.

< マタイの福音書 24 >