< 箴言 知恵の泉 1 >

1 ダビデの子、イスラエルの王ソロモンの箴言。
Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 これは人に知恵と教訓とを知らせ、悟りの言葉をさとらせ、
Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 賢い行いと、正義と公正と公平の教訓をうけさせ、
ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 思慮のない者に悟りを与え、若い者に知識と慎みを得させるためである。
Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 賢い者はこれを聞いて学に進み、さとい者は指導を得る。
Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
6 人はこれによって箴言と、たとえと、賢い者の言葉と、そのなぞとを悟る。
kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
7 主を恐れることは知識のはじめである、愚かな者は知恵と教訓を軽んじる。
Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
8 わが子よ、あなたは父の教訓を聞き、母の教を捨ててはならない。
Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9 それらは、あなたの頭の麗しい冠となり、あなたの首の飾りとなるからである。
zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10 わが子よ、悪者があなたを誘っても、それに従ってはならない。
Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11 彼らがあなたに向かって、「一緒に来なさい。われわれは待ち伏せして、人の血を流し、罪のない者を、ゆえなく伏してねらい、
Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12 陰府のように、彼らを生きたままで、のみ尽し、健やかな者を、墓に下る者のようにしよう。 (Sheol h7585)
Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni. (Sheol h7585)
13 われわれは、さまざまの尊い貨財を得、奪い取った物で、われわれの家を満たそう。
Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
14 あなたもわれわれの仲間に加わりなさい、われわれは共に一つの金袋を持とう」と言っても、
Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
15 わが子よ、彼らの仲間になってはならない、あなたの足をとどめて、彼らの道に行ってはならない。
Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;
16 彼らの足は悪に走り、血を流すことに速いからだ。
miguu ya hukimbilia mabaya na huharakisha kumwaga damu.
17 すべて鳥の目の前で網を張るのは、むだである。
Kwa kuwa haina maana kumtegea ndege mtego wakati ndege anaona.
18 彼らは自分の血を待ち伏せし、自分の命を伏してねらうのだ。
Watu hawa huvizia kujiua wenyewe—wanatega mtego kwa ajili yao wenyewe.
19 すべて利をむさぼる者の道はこのようなものである。これはその持ち主の命を取り去るのだ。
Ndivyo zilivyo njia za kila ambaye hupata utajiri kwa udhalimu; mapato ya udhalimu huondoa uhai wa wenye utajiri.
20 知恵は、ちまたに呼ばわり、市場にその声をあげ、
Hekima inalia kwa sauti mtaani, inapaza sauti katika viwanja;
21 城壁の頂で叫び、町の門の入口で語る。
katika mitaa inalia kwa sauti kuu, kwenye maingilio ya milango ya mji inasema “
22 「思慮のない者たちよ、あなたがたは、いつまで思慮のないことを好むのか。あざける者は、いつまで、あざけり楽しみ、愚かな者は、いつまで、知識を憎むのか。
Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
23 わたしの戒めに心をとめよ、見よ、わたしは自分の思いを、あなたがたに告げ、わたしの言葉を、あなたがたに知らせる。
Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
24 わたしは呼んだが、あなたがたは聞くことを拒み、手を伸べたが、顧みる者はなく、
Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
25 かえって、あなたがたはわたしのすべての勧めを捨て、わたしの戒めを受けなかったので、
Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
26 わたしもまた、あなたがたが災にあう時に、笑い、あなたがたが恐慌にあう時、あざけるであろう。
Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
27 これは恐慌が、あらしのようにあなたがたに臨み、災が、つむじ風のように臨み、悩みと悲しみとが、あなたがたに臨む時である。
hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
28 その時、彼らはわたしを呼ぶであろう、しかし、わたしは答えない。ひたすら、わたしを求めるであろう、しかし、わたしに会えない。
Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
29 彼らは知識を憎み、主を恐れることを選ばず、
Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,
30 わたしの勧めに従わず、すべての戒めを軽んじたゆえ、
hawakufuata mafundisho yangu na wakayadharau masahihisho yangu yote.
31 自分の行いの実を食らい、自分の計りごとに飽きる。
Watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa kwa matunda ya hila zao wenyewe.
32 思慮のない者の不従順はおのれを殺し、愚かな者の安楽はおのれを滅ぼす。
kwa maana wajinga hufa wanaporudi nyuma, na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.
33 しかし、わたしに聞き従う者は安らかに住まい、災に会う恐れもなく、安全である」。
Bali kila anisikilizaye ataishi kwa usalama na atapumzika salama pasipo hofu ya maafa.

< 箴言 知恵の泉 1 >