< Salmi 135 >

1 Alleluia. Lodate il nome dell’Eterno. Lodatelo, o servi dell’Eterno,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 che state nella casa dell’Eterno, nei cortili della casa del nostro Dio.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Lodate l’Eterno, perché l’Eterno è buono; salmeggiate al suo nome, perché è amabile.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Poiché l’Eterno ha scelto per sé Giacobbe, ha scelto Israele per suo speciale possesso.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Sì, io conosco che l’Eterno è grande, e che il nostro Signore è al disopra di tutti gli dèi.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 L’Eterno fa tutto ciò che gli piace, in cielo e in terra, nei mari e in tutti gli abissi.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Egli fa salire i vapori dalle estremità della terra, fa i lampi per la pioggia, fa uscire il vento dai suoi tesori.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Egli percosse i primogeniti d’Egitto, così degli uomini come degli animali.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Mandò segni e prodigi in mezzo a te, o Egitto, su Faraone e su tutti i suoi servitori.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Egli percosse grandi nazioni, e uccise re potenti:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sihon, re degli Amorei, e Og, re di Basan, e tutti i regni di Canaan.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 E dette il loro paese in eredità, in eredità a Israele, suo popolo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 O Eterno, il tuo nome dura in perpetuo; la memoria di te, o Eterno, dura per ogni età.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Poiché l’Eterno farà giustizia al suo popolo, ed avrà compassione dei suoi servitori.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Gl’idoli delle nazioni sono argento e oro, opera di mano d’uomo.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Hanno bocca e non parlano; hanno occhi e non vedono;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 hanno orecchi e non odono, e non hanno fiato alcuno nella loro bocca.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Simili ad essi siano quelli che li fanno, tutti quelli che in essi confidano.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Casa d’Israele, benedite l’Eterno! Casa d’Aaronne, benedite l’Eterno!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Casa di Levi, benedite l’Eterno! Voi che temete l’Eterno, benedite l’Eterno!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Sia benedetto da Sion l’Eterno, che abita in Gerusalemme! Alleluia.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salmi 135 >