< איוב 6 >

ויען איוב ויאמר 1
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
לו--שקול ישקל כעשי והיתי (והותי) במאזנים ישאו-יחד 2
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
כי-עתה--מחול ימים יכבד על-כן דברי לעו 3
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
כי חצי שדי עמדי--אשר חמתם שתה רוחי בעותי אלוה יערכוני 4
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
הינהק-פרא עלי-דשא אם יגעה-שור על-בלילו 5
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
היאכל תפל מבלי-מלח אם-יש-טעם בריר חלמות 6
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
מאנה לנגוע נפשי המה כדוי לחמי 7
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
מי-יתן תבוא שאלתי ותקותי יתן אלוה 8
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
ויאל אלוה וידכאני יתר ידו ויבצעני 9
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
ותהי-עוד נחמתי-- ואסלדה בחילה לא יחמול כי-לא כחדתי אמרי קדוש 10
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
מה-כחי כי-איחל ומה-קצי כי-אאריך נפשי 11
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
אם-כח אבנים כחי אם-בשרי נחוש 12
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
האם אין עזרתי בי ותשיה נדחה ממני 13
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
למס מרעהו חסד ויראת שדי יעזוב 14
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
אחי בגדו כמו-נחל כאפיק נחלים יעברו 15
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
הקדרים מני-קרח עלימו יתעלם-שלג 16
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
בעת יזרבו נצמתו בחמו נדעכו ממקומם 17
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
ילפתו ארחות דרכם יעלו בתהו ויאבדו 18
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
הביטו ארחות תמא הליכת שבא קוו-למו 19
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
בשו כי-בטח באו עדיה ויחפרו 20
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
כי-עתה הייתם לא תראו חתת ותיראו 21
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
הכי-אמרתי הבו לי ומכחכם שחדו בעדי 22
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
ומלטוני מיד-צר ומיד עריצים תפדוני 23
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
הורוני ואני אחריש ומה-שגיתי הבינו לי 24
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
מה-נמרצו אמרי-ישר ומה-יוכיח הוכח מכם 25
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
הלהוכח מלים תחשבו ולרוח אמרי נואש 26
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
אף-על-יתום תפילו ותכרו על-ריעכם 27
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
ועתה הואילו פנו-בי ועל-פניכם אם-אכזב 28
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
שובו-נא אל-תהי עולה ושבי (ושבו) עוד צדקי-בה 29
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
היש-בלשוני עולה אם-חכי לא-יבין הוות 30
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

< איוב 6 >