< בראשית 11 >

ויהי כל הארץ שפה אחת ודברים אחדים 1
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
ויהי בנסעם מקדם וימצאו בקעה בארץ שנער וישבו שם 2
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
ויאמרו איש אל רעהו הבה נלבנה לבנים ונשרפה לשרפה ותהי להם הלבנה לאבן והחמר היה להם לחמר 3
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
ויאמרו הבה נבנה לנו עיר ומגדל וראשו בשמים ונעשה לנו שם פן נפוץ על פני כל הארץ 4
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
וירד יהוה לראת את העיר ואת המגדל אשר בנו בני האדם 5
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
ויאמר יהוה הן עם אחד ושפה אחת לכלם וזה החלם לעשות ועתה לא יבצר מהם כל אשר יזמו לעשות 6
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
הבה נרדה ונבלה שם שפתם--אשר לא ישמעו איש שפת רעהו 7
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
ויפץ יהוה אתם משם על פני כל הארץ ויחדלו לבנת העיר 8
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
על כן קרא שמה בבל כי שם בלל יהוה שפת כל הארץ ומשם הפיצם יהוה על פני כל הארץ 9
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
אלה תולדת שם--שם בן מאת שנה ויולד את ארפכשד שנתים אחר המבול 10
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
ויחי שם אחרי הולידו את ארפכשד חמש מאות שנה ויולד בנים ובנות 11
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
וארפכשד חי חמש ושלשים שנה ויולד את שלח 12
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
ויחי ארפכשד אחרי הולידו את שלח שלש שנים וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות 13
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ושלח חי שלשים שנה ויולד את עבר 14
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
ויחי שלח אחרי הולידו את עבר שלש שנים וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות 15
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי עבר ארבע ושלשים שנה ויולד את פלג 16
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
ויחי עבר אחרי הולידו את פלג שלשים שנה וארבע מאות שנה ויולד בנים ובנות 17
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי פלג שלשים שנה ויולד את רעו 18
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
ויחי פלג אחרי הולידו את רעו תשע שנים ומאתים שנה ויולד בנים ובנות 19
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי רעו שתים ושלשים שנה ויולד את שרוג 20
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
ויחי רעו אחרי הולידו את שרוג שבע שנים ומאתים שנה ויולד בנים ובנות 21
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי שרוג שלשים שנה ויולד את נחור 22
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
ויחי שרוג אחרי הולידו את נחור--מאתים שנה ויולד בנים ובנות 23
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי נחור תשע ועשרים שנה ויולד את תרח 24
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
ויחי נחור אחרי הולידו את תרח תשע עשרה שנה ומאת שנה ויולד בנים ובנות 25
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
ויחי תרח שבעים שנה ויולד את אברם את נחור ואת הרן 26
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
ואלה תולדת תרח--תרח הוליד את אברם את נחור ואת הרן והרן הוליד את לוט 27
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
וימת הרן על פני תרח אביו בארץ מולדתו באור כשדים 28
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
ויקח אברם ונחור להם נשים שם אשת אברם שרי ושם אשת נחור מלכה בת הרן אבי מלכה ואבי יסכה 29
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
ותהי שרי עקרה אין לה ולד 30
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
ויקח תרח את אברם בנו ואת לוט בן הרן בן בנו ואת שרי כלתו אשת אברם בנו ויצאו אתם מאור כשדים ללכת ארצה כנען ויבאו עד חרן וישבו שם 31
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
ויהיו ימי תרח חמש שנים ומאתים שנה וימת תרח בחרן 32
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< בראשית 11 >